Shambulizi La Kigaidi Laua Zaidi Ya Watu 75 Nchini Ufaransa
Zaidi ya watu 70 wameripotiwa kuuawa katika shambulio lililotokea katika mji wa Nice kaskazini mwa Ufaransa.
Lori
lililokuwa likienda mwendo kasi lilijiingiza katika mkusanyiko wa watu
waliokuwa wakiangalia maonesho ya fataki kuadhimisha siku ya kitaifa ya
Bastille, ambayo huja na shamra shamra kila mwaka.
Mwendesha
mashtaka katika mji wa Nice, Jean- Michel Pretre amesema lori hilo
liliendelea kutembea kilo mita mbili kabla ya polisi kumpiga risasi
dereva.
Bunduki na makombora yameripotiwa kukutwa ndani ya lori hilo. Waakazi wa mji huo wa Nice wameshauriwa kutulia majumbani.
Rais Francois Hollande amerudi mjini Paris kwa ajili ya kufanya kikao cha dharura. Hali
ya tahadhari iliyowekwa toka kutokea kwa shambulio lililofanywa na
Islamic State mjini Paris, bado iko palepale nchini Ufaransa.
CHANZO BBC
Shambulizi La Kigaidi Laua Zaidi Ya Watu 75 Nchini Ufaransa
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:29:00
Rating:
No comments: