RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 21 & 22 Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


Mtunzi:EDDAZARIA G.MSULWA
 ILIPOISHIA
    Nilizungumza huku nikilitazama gari la shule linalo simama na kumouna mkuu wa shule akishuka huku akiwa na mkewe wakicheka kwa furaha na kwabahati mbaya hakuniona.Nikapiga hatua za haraka  hadi alipo simama mkuu wa shule na kumgusa bega kitendo cha yeye kugeuka na kuiona sura yangu akastuka na kwa kasi ya ajabu mkono wangu wa kulia nilio ukunja ngumi ukatua kwenye shavu la mkuu wa shule na kumfaya ayumbe kwa nguvu na kumkumba mke wake na wote wakaanguka chini

ENDELEA
    Madam Mery akaniwahi kunishika shati na kuanza kuniomba niache vurugu,mkuu wa shule akanyanyuka kwa hasira na kunisogelea na kunizaba kofi lililopelekea nikazidi kupadwa na hasira,Madam Mery akaendelea kuning’ang’ania kwa nguvu zake zote ila kutokana na nguvu nilizo nazo nikajitoa mikononi mwa madam Mery na kumfwata mkuu wa shule na kuanza kumrushia ngumi zisizo na idadi na uzuri zaidi kipindi nipo mdogo baba yangu alikuwa akinifundisha mbinu za kuweza kupigana kiasi kwamba hadi ninakua mkubwa swala zima la kupigana kwangu ni lakawaida.Waalimu wa kiume waliopo eneo la shule wakaja kutuzuia japo kuwa mkuu wa shule ni mzee kidogo ila na yeye alijitahidi kunipa makonde kadhaa yaliyo niingia vizuri sehemu mbali mbali za mwili wangu
 
“Eddy nakuomba uwe mpole kumbuka hapa tupo shule”
Madam Mery alizungumza kwa upole huku nikiondolewa eneo la tukio na waalimu wapatao wanne na kwajinsi nilivyo na nguvu na iliwalazimu kutumia nguvu nyingi katika kunizuia kwenda kuendeleza ogomvi na mkuu wa shule
“Wewe kijana mshenzi sana hujafunzwa huko kwenu hadi unapigana na mume wangu na nitahakikisha shule huna wewe mpumbavu mkubwa weee”
 
Mke wa mkuu wa shule alizungumza maneno yaliyozidi kunipandasha hasira laiti angejua mumewe kitu alicho toka kukifanya jana usiku wala asinge zungumza ujinga anao uzungumza
“Sawa waalimu wangu nimewaelewa ngoja mimi niondoke zangu naombeni muniachie”
 
   Nilizungumza kwa upole na kuwafanya waalimu wa kiume walio nishika kuniachia taratibu na huku wakiniomba niondoke sehemu ya eneo la shule.Kwa haraka nikamsukuma mwalimu wa mbele yangu akaanguka chini nikapata nafasi ya kukimbilia eneo alilopo mkuu wa shule na nikamchomoa katikati ya watu wanao mpa pole na kumpiga kabali moja takatifu iliyotupeleka hadi chini ardhini na watoto wa mjini wenyewe tunaiita kabala ya mbao na kuwafanya walinzi na waalimu wa kiume kuanza kuushika mkono wangu na kuanza kuuvuta kwa nguvu ili kuyanusuru maisha ya mkuu wa shule.Wakafanikiwa kunichomoa huku mwili wangu ukiwa umejaa jasho jingi huku misuli ya mwili mzima ikiwa imetuna kiasi kwamba mtu aliyezoea kuniona kwenye mazingira ya kawaida atabisha kuniona kwenye hali ya hasira niliyo nayo sasa na atasema sio mimi
 
Mke wa mkuu wa shule akaanza kumfuta futa mumewe mchanga kwenye uso wake kiasi kwamba baadhi ya wanafunzi wakaanza kumcheka kwa jinsi anavyo tisha sura kwa kuchafuka.
 
“Oya Eddy tutakuchukulia hatua za kisheria sisi kama shule”
“Tea na wewe mwalimu wa nidhamu ninakumind kama nini sasa na wewe ingia kwenye kumi na nane zangu……Wewe unajua huu ugomvi umetokea wapi au unazungumza zungumza kumpa bichwa huyo choko wenu sifa……”
Nikasimama kwenye sehemu iliyopo juu na kuwafanya watu wote wanitazame kwa umakini huku wakinisikiliza akiwemo mkwe wa mkuu wa shule
 
“Huyo mzee wenu anahabari za kiseng* sana….Kazi yake ni kuwachukua wanafunzi wa kike na kwenda nao kwenye mahoteli makubwa na kufanya nao mapenzi.Ushahidi ninao na kama mwalimu yoyote atake bisha nitautuma kwenye wizara ya elimu tuone kama hii shule haito fungiwa”
Nilizungumza na kumuona Salome akijikatiza katikati ya wanafunzi na waalimu na kuja kupanda sehemu niliyo simama mimi huku akionekana kuwa na asira kali.Nikamtazama kwa jicho kali kiasi kwamba akatulia na kuzidi kuwafanya wanafunzi kuzidi kuongezeka wakitokea mabwenini na madarasani wakitaka kujua ni nini kinacho endelea
 
“Hapa nina gazeti linaelezea mambo ya huyo mzee aliyo yafanya jana usiku isitoshe alitaka kuniua kwa kunipiga na bastola ila kwa bahati mbaya akampiga mpenzi wangu na sasa hivi ninavyo zungumza amelazwa hospitalini”
Minong’ono ya wanafunzi ikaanza kutawala eneo tulilopo na nikaanza kazi ya kuwanyamazisha wanafunzi wezangu na kumfanya mkuu wa shule kuzidi kunitumbulia mimacho ya hasira na kila alipotaka kuondoka mke wake akawa anamzuia asiondoke
 
“Ngoja niwasomee habari ya hili gazeti na mukiwa amuamini nitawawekea video au picha za huyo mzee muone mambo mauvu anayo yafanya…….Kichwa cha habari cha hili gazeti kanasema HEAD MASTER AUA KISA MAPENZI habari ukurasa wa pili ianasema hivii….Mkuu wa shule moja jina tunalihifadhi anajiukuta akiangukia kwenye mikono ya polisi baada ya kumpiga risasi”
 
Nikapunguza sauti ya kulisoma gazeti kwani kitu kilicho andikwa kwenye gazeti kilianza kunichanganya kidogo na nikazidi kukisoma kimya kimya bila mtu kusikia
“Binti mmoja na kumuua kabisa.Muobgozaji wa filamu hiyo inayoitwa SCONGA LOVE imeshirikisha wasanii wengi maarufu kutoka nje na ndani ya mipaka ya Tanzania.Star wa filamu hiyo ambaye amecheza kama mkuu wa shule inasemekana ameweza kuziteka hisia za wasanii wezake alio wafanya nao kazi.Muandishi wetu alikutana na msanii huyo na mahojiano yalikuwa hivi”
 
Nikanyanyua macho yangu na kuwatazama wanafunzi na watu wengine wakisubiria niwasomee kilicho andikwa ndani ya gazeti hilo.Gafla sauti ya Salome ikaanza kusikika kwa sauti ya juu na kunifanya nimtazame
 
“Huu ndi mwisho wa manyanyaso ya wasichana wa kike kwenye hii shule…..Waalimu wengi hapa shule hututumia sisi kama vituliza nyeg* japo wana wake zao na wengine magirl friend zao……Mfano mzuri ni mimi.Jana asubuhi nilimuomba mwalimu wa zamu Pass(Ruhusa) ya kwenda kununua matumizi yangu binafsi kabla sijatoka getini mkuu wa shule akaomba anipe lipfti kwenye gari lake hadi mjini.Sikuwa na hiyana zaidi ya kukubali kutokana tumememzoea kama baba yetu wa kimwili na kiroho”
 
Salome alizungumza huku machozi yakimwagika na kunifanya na mimi niungane na wanafunzi wengine kumsikiliza kwa umakini wa hali ya juu
“Basi tukiwa ndani ya gari alipandisha vioo vyake vya gari lake na kuanza kunitongoza huku akidai atanipa kila nitakacho taka ikiwemo kunivujishia mitihani ya nusu mwaka kwa sisi A LEVEL……….Nilikataa na mwenzangu akazidi kuliendesha gari lake kwa kasi na sikuweza kushuka kwani hata mjini kwenyewe alinipitisha na tukafika kwenye moja ya hoteli na akanitolea bastola na kuniambia endapo nitakataa kushuka ndani ya gari ataniua.Sikuwa na ujanja zaidi ya kufanya kama alicho niagiza.Tukapitliza moja kwa moja kwenye chumba na head master akanilazimisha nifanye naye mapenzi bila kinga…….Na isitoshe aliniingilia kinyume na maumbile”
 
Mwili mzima ukafa ganzi nikabaki niemeduwaa huku wanafunzi wengie wakianza kutokwa na machozi wakimuonea haruma Salome.Ukelele mkali ukasikika katikati ya wanafunzi na ni mke wa mkuu wa shule alizidi kupiga makelela huku akiongea kichaga na kumpiga piga mumewe kwenye kifua
 
“Baba Evance mtoto wa watu umeshamuua wewe si unajijua kuwa sisi ni waadhirika ni kwanini sasa umefanya hivyo baba Evance”
Salome baada ya kuyasikia maneno ya mke wa mkuu wa shule akalegea mwili wake na kabla hajafika chini nikamnyaka na kumlaza taratibu na vilio vya wanafunzi wa kike vikaanza kutawala huku wengine wakidai wametembea na mzee huyo bila kinga na nimiongoni mwa wanafunzi walio ambukizwa virusi vya ukimwi.Waalimu wa kiume wakaanza kumchukua mwalimu mkuu na kumuingiza ndani ya gari la shule na wakaondoka kwa kasi katika eneo la shule kwani wanafunzi walianzisha vurugu za kuwarushia mawe
 
“NANI YUPO PAMOJA NAMI”
Wanafunzi karibia wote wakanyoosha vidole juu akiwemo rafiki yangu John ambaye alikuja wakati wa mwisho mwisho wa tukio na ninavyo mjua alikuwa ametoroka.Wanafuzni wakaanza kurusha mawe kwenye ofisi za waalimu na kuvunja vioo,nikamnyanyua Salome nikisaidiwa na wezake na tukamuingiza ndani ya gari langu huku  John akiingia kwenye siti ya upande wangu huku akijichekesha chekesha.Nikawasha gari na kwa kasi ya hali ya juu nikanza kufwata njia ilipo elekea gari la shule kutokana katika eneo hiko kuna njia moja tu ya kutokea.Kwa mwendo kasi wa gari langu nikaanza kuliona gari alilopanda mkuu wa shule kwa mbali likikata kona kusoto kushika njia ya kuelekea porini kwenye migomba mingi
 
“Eddy na huyo Salome tunakwenda naye wapi?”
“Huko huko”
“Huko huko wapi akitufia mtoto wa watu itakuwaje?”
“Potelea pote ila cha msingi nilazima mkuu wa shule alipe kwa hili”
“Eddy mtu mwenyewe mbona kama haemi”
“John hembu niachie kelele”
Johnalizungumza kimasihara kiasi kwamba ninaona anazidi kunichanganya,Simu yangu mfukoni ikaanza kuita na ninamba ngeni ndio inayo ingia ikanilazimu kuipokea na kuweka loudspeaker
“Eddy mume wangu uko wapi?”
Ilikuwa ni sauti ya Sheila ikizungumza kwa upole
“Baby usijali ninakuja…hii namba ni ya nani?”
“Ni namba ya nesi nimemuomba”
“Umeshakula baby?”
“Ndio mume wangu……nakuomba ndani ya dakika kumi uwe umefika hapa la sivyo nitameza vidonge nijiue kabisa”
“Mke wangu usiseme hibyo”
“Nasema hivyo kutokana nina hamu na wewe na ninahisi upo na mwanamke mwengine”
“No baby naomba usinifikirie vibaaya”
“Sawa ila fanya hivyo nakuesabia dakika mume wangu”
“Sawa”
 
Nikakata simu na kuzidi kuongeza kasi ya gari langu hadi nikafanikiwa kulipita gari alilopo mwalimu mkuu kisha nikalisimamisha gari langu gafla kitendo kilichomfanya dereva wa gari alilopanda mwalim mkuu kunikwepa na kugonga mti mkubwa uliopo pembeni ya barabara nagari lao likasimama kiasi kwamba ndani ya dakika mbili hapakuwa na mtu yoyote aliye shuka kutoka ndani ya gari lao.Nikashuka na kuitoa simu yangu na kuanza kurekodi tukio moja baada ya jengine hadi ninafika kwenye gari la shule nikamkuta dereva wa gari hilo akiomba msaada wa kutolewa ndani ya gari hilo hii nibaada ya kubanwa na mskani wa gari kwenye kifua.Kitu kilicho nishagaza sikuweza kumuona mwalimu mkuu wala waalimu wengine wa kiume walio toroka eneo la shule
 
“Mkuu wa shule yupo wapi?”
“Ni…liwas…shusha…..njiani”
“Wapi?”
“Kul…e kwenye shamb…..a la migomba”
“Fuc*”
Nikamuacha derava akiendelea kubanwa na mskani wake na nikaingia ndani ya gari huku John akifwatia kwa nyuma na kuingia ndani ya gari na kufunga mkanda
“Eddy si tungemsaidia jamaa wa watu”
“Siwezi kusaidia mijitu mipumbavu kama yeye”
“Kwa nini?”
“Hii vita yeye haimuhusu kilicho mfanya aingilie ni nini?”
“Eddy kuwa na roho ya kibinadamu yule jamaa yupo powa sana huwa……”
 
“JOHN KAMA UNATAKA KUMSAIDIA SHUKA NDANI YA GARI LANGU NA UENDE UKAMSAIDIE”
Nilizungumza kwa sauti kali iliyo jaa hasira kiasi kwamba John akastuka na kukaa kimya,Nikageuza gari na kabla sijafika umbali kutoka lilipo gari la shule lilipo pata ajali nikasimamisha gari
“Eddy nishushe nikamsaidie jamaa wa watu”
“Powa shuka”
John akashuka ndani ya gari na mimi nikaendelea na safari ya kurudi mjini huku gari nikiliendesha kwa mwendao wa kasi ili nimuwahi Sheila aliye nipa dakika la sivyo anaweza kufanya kitu kibaya cha kujiua.Kitendo cha kufika hospitli nayo simu yangu ikaita kwa namba ile aliyo nipigia Sheila kwa mara ya kwanza nikaipokea
“Eddy mume wangu hutaki kuja eheee?”
“Nipo hapa nje”
“Kweli?”
“Ndio mke wangu”
“Sawa”
 
Nikamuita nesi mmoja na kumuonyesha Salome tuliye mlaza siti ya nyuma na kumuomba amtoe na kumfanyia huduma ya kwanza.Nikapitiliza moja kwa moja hadi chumba alicholazwa Sheila na kumkuta akiwa ana wasi wasi
“Baby mbona umechelewa”
Nikaanza kumuadisia Sheila kuanzia mwanzo wa tukio hadi mwisho wa tukio lilivyo tokea ila nilimficha juu ya uwepo wa Salome kwenye hospitali hiyo
“Sasa huyo mkuu wa shule yeye yupo wapi?”
“Sijui yupo wapi na mbaya zaidi jana alipo toka kufanya tulio la kukupiga risasi polisi wakamuachia huru”
“Mmmm mume wangu ninakuomba umpotezee”
“Siwezi kufanya hivyo yule mzee anatabia chafu na isitoshe anawaambukiza wanafunzi wa kike HIV kimakusudi”
“Weeee”
 
“Ndio hapa shule wanafunzi wengi wa kike nimewaacha wakili na nahisi ametembea na wengi sana”
“Mmmm kweli huyoo si mtu wa kuacha uraiani.Sasa wewe kama wewe umeamuaje?”
“Hi video nitaituma kwa mama kisha atajua nini cha kufanya”
“Ngoja kwanza ukimtumia mama yeye akikuuliza ulifwata nini hotelini utamjibuje?”
“Nitajua cha kumuambia mimi mama yangu hana neono”
“Mmm mimi ninakushauri usimtumie ni bora ukaituma kwa huyo waziri wa elimu”
“Umesha kula?”
 
“Ndio na wamenichoma sindano ya kukausha kidonda”
“Wamekuchomea wapi hiyo sindano”
“Kwenye makalio”
“Kwahiyo wamekushika mpododo?”
“Bwana Eddy hembu acha utani wako”
“Ngoja nikachukue msosi tangu jana tulipo kule njiani hadi sasa hivi sijaweka kitu mdomoni”
“Sawa mume waangu ila usichelewe kurudi”
Nikamnyonya lipsi Sheila na kutoka nje chumba na kwenda alipo lazwa SALOME na kukuta madaktari wakimshughulikia
“Dokta amepata tazizo gani?”
“Amepata mstuko wa moyo”
“Mmmm kwahiyo itakuwaje?”
 
“Ndio tunamshuhulikia kuurudisha moyo wake kwenye hali yake ya kawaida”
“Sawa dokta kila kitakocho endelea unijulishe kwenye hii namba”
“Sawa”
Nikamuachia daktari namba yangu ya simu kisha nikatoka na kwenda kwenye mgahawa wa karibu na hospitali na nikaagiza chakula na kuanza kula taratibu huku nikitafakari ni nini nifanye juu ya ushaidi wa kumkamata mkuu wa shule.Tv(Luninga) iliyopo kwenye mgahawa Chaneli Ten ikaonyesha habari iliyo wafikia kwa wakati huo(BREAKING NEWS) na kunifanya niache kula na kuitazama kwa umakini.Nikashuhudia jinsi askari wakijitahidi kutuliza fujo zinazo endelea shuleni kwetu huku ofisi za waalimu zikiwa zinateketea kwa moto
 
“Wanafunzi bado wanaendelea kupambana na askari wa kutuliza ghasia na madai yao makubwa ni mkuu wa shule hiyo kuwaambukiza vijana wa kike wapatao kumi na sita virusi vya ugonjwa hatari wa UKIMWI kimakusudi huku akitumia nguvu katika kulifanya hilo”
 
Mtangazaji alizungumza huku kamera ikionyesha jinsi wanafunzi wa shuleni kwetu wakiwarushia mawe askari huku wengine wakiwa na mipini ya mejembe na makwanja wakiendelea kupambana na polisi
 
“Mkuu wa jeshi la polisi amewaahidi wanafunzi hao kufanya kila linalo wezekana katika kumkamata mkuu huyo wa shule ambaye hadi sasa hivi haijulikani yupo wapi.Serikali nini maana ya elimu? Wazazi wanajitolea pesa zao ili watoto wao wapate elimu iliyo bora ila mwisho wa siku hali ndio hii.Tunaiomba wizara ya elimu kuunda tume ya kuchunguza tabia za waalimu hususani katika haya mashule ya watu binafsi.Tutaendelea kuwajulisha kitakacho endelea….Nikikutangazia kutoka Mkoani Arusha mimi ni Upendo John Chanel Ten”
 
Nikasusha pumzi na kuwatazama watu waliomo kwenye mgahawa huo ni jinsi gani walivyo ichukulia hiyo taarifa ya habari na kila mmoja anaonekana kukasirishwa na kitendo cha mkuu wa shule kufanya jambo la kikatili kama hilo.Nikalipa nilicho kula na kuingia ndani ya gari na safari ya kuelekea shule ikaanza,Nikapitiiza moja kwa moja kwa Madam Mery na nikafika nyumbani kwake nikapiga honi kwa muda nikaona kupo kimya ikanilazimu kushuka kwenye gari na kuligonga geti na kwakupitia uwazi mdogo nikamuona Madam Mery akichungulia kwenye mlango wa kuingilia kwake huku wakiwa na Madam Rukia wakishauriana kuja kufungua huku wakionekana kuwa na wasi wasi.
 
“Madam ni mimi Eddy fungueni”
“Eddy yupi huyo?”
“Sasa hivi hunijui au?”
“Ahaa Eddy nakuja kukufungulia?”
Madam Rukia akatoka ndani na kuja getini na kunifungulia geti nikarudi ndani ya gari na kuliingiza gari ndani na kushuka na Madam Mery akanifwata huku akionekana kuwa na wasi wasi
“Eddy umesalimika?”
“Ndio ila sijampata mkuu wa shule”
“Sasa si utulie jamani mpenzi wangu”
“Siwezi kutulia hadi nijue muafaka wa mkuu wenu wa shule”
“Eddy jamani huoni kama unajiingiza matatizoni?”
“Maji nimeyavulia nguo acha niyaoge…..Ngoja nielekee shule”
“Shule tena?”
“Ndio”
 
“Eddy huko unapokwenda kuna vurugu nyingi na askari wanawakusanya wanafunzi wanao fanya vurugu na kuwapeleka polisi”
“Ache iwe hivyo wewe nilindie hili gari sawa”
“Eddy jamani mpenzi wangu nakuomba usiende”
“Madam mimi sasa hivi sio mpenzi wako kutokana tayari wewe umesha olewa na nimjamzito kwaiyo siwezi kuvunja kile alicho kiunganisha MUNGU”
 
“Eddy ila tambua ya kwamba ninakupenda tena sana”
Madam Mery alizungmza huku machozi yakimwagika huku akining’ang’ania mkono wangu nisiondoke
“Sory Madam ninakuomba uniachie niende na ninakuomba umpende mume wako kama ulivyo nipenda mimi ninakuomba unisamehe kwa hilo siwezi kuwa na wewe”
“Eddy Eddy ndio unaniacha?”
“Sio kama ninakuacha ila nitakuheshimu kama mwalimu wangu na si vinginevyo”
Nikauachanisha mkono wa Madam Mery kwenye mkono wangu kisha nikaanza kupiga hatua za haraka kuelekea getini
 
“EDDY TAMBUA NIMEBEBA MWANAO NA MUME WANGU NIMEACHANA NAYE BAADA YA KUJUA MIMI NINAUJAUZITO AMBAO SI WAKE”
Niksimama na kugeuka taratibu huku nikiwa ninamtazama Madam Mery anaye lia huku akiwa amekaa chini akionekana kuwa na uchungu na kunifanya nizidi kuchanganyikiwa
    
                  *****SORY MADAM*****(22)
   
    Nikapiga hatua za taratibu na kumnyanyua Madam Mery na kuanza kufuta machozi taratibu kwa kutumia kitambaa changu kisha tukaingia ndani na moja kwa moja tukapitiliza hadi chumbani kwake.Ukimya ukatawala kati yetu huku madam Mery akiendelea kulia chini chini na kichwani kwangu sikuwa na hata wazo la kulizungumza likaeleweka
“Eddy”
“Naam”
“Amini ya kwamba nina kupenda sana japo kuwa kiumri tume tofautana ila moyo wangu umeshindwa kumpenda mwanaume mwengine zaidi yako”
 
“Acha kuniongopea......nilikuona ni mtu wa maana sana kipindi mapenzi yetu yalipo anza lakini leo hii unaniambia umeolewa tena na mapicha ya harusi yako unayambandika huku ukutani”
Nilizungumza kwa sauti ya ukali kiasi kwamba Madam Mery akawa mpole pasipo kuzungumza kitu cha aina yoyote
“Tena umeona gia yako ni kuniongopea kuwa wewe ni mjamzito,Unadhani mimi nitakubali kirahisi kulea mimba ambayo sielewi mwanzo wake ni upi wala mwisho wake”
 
“Eddy najua unauchungu moyoni mwako kwa mimi kuolewa.....Ila Eddy mimi sikuwa na jinsi ya kufanya”
“Ahaaaa hukuwa na jinsi ya kufanya kwani wewe ni mtoto mdogo ambaye ulibebwa juu juu na kupelekwa kanisani na kufungishwa ndoa eheee?”
Madam Mery akazidi kulia kwa uchungu huku na mimi hasira ikianza kujaa kifuani kwangu hadi nikajikuta nikianza kutetemeka mikono
 
“Eddy am sory?(Eddy samahani)
“Samahani yako haiwezi kuchukua nafasi yoyote ndani ya moyo wangu kwasababu hujui ni jinsi gani nilivyo kuwa ninakupenda.....Leo hii unasema umeolewa na mimba ni yangu.Hainiingii akilini hata kidogo”
“Eddy naomba nikuambie ukweli”
“Ukweli kuhusu nini?”
 
“Eddy kipindi nilipo anza mahusiano na wewe nilikuwa na mpezi wangu ambaye alikuwa Uingereza kimasomo....Alirudi mwezi ulio pita na akanifanyia suprize ya kunivalisha pete ya uchumba na tukafunga ndoa ila...”
“Ila nini sasa kumbe siku zote una kazi ya kuniongopea na kumbe una bvwana wako nje ya nchi.Mbona nyinyi wanawake hampendeki mufwanye nini ili mujue munapendwa.....Wenyewe mukafanya vya kutosha ehee alafu mukajazana mimba leo hii unaniambia Eddy hii mimba ni yako.Si ndio munavyo danganyana”
 
Nilizidi kuzungumza kwa sauti ya kufoka kiasi kwamba Madam Mery akanyanyuka kwa hasira na kunipiga kibao cha shavu na kuzidi kunipandisha hasira.Nikamshika koo Madam Mery na kumuegemeza ukutani huku nikimuangalia kwa macho yaliyo jaa hasira hadi machozi yakaanza kunimwagika
“MERY NITAKUUA”
“E...ddy we..ee niue nipo...radhi kwa hilo.Mimi siku zote nilijua UMEKUFA NDIO MAANA NIKACHUKUA MAAMUZI YA KUOLEWA”
“Fuc* you”
 
   Nikamuachia madam Mery na kuanza kuvunja picha zilizo tengenezewa frame na kwahasira nikaanza kupiga ngumi ukutani hadi mikono ikaanza kuvuja damu.Madam Mery akapiga hatua moja ya kunifwata nikageuka kwa jinsi ya muonekano wangu tu ilitosha kumfanya asimame kama namba moja asipige hatue nyingine ya pili
“Usinifwate nitakuua”
 
“Eddy unajiumiza”
“Nimekuambia niache...Sasa hivi huyu unaye zungumza naye ni mfu wa Eddy ila Eddy mwenyewe amekufa mwanzo leo mwisho leo sitaki kusikia unanitafuta”
“Eddy jamani kwanini unanifanyia hivyo au kwasababu ninakupenda,kwa nini unanikatili kiasi hicho unataka huyu kiumbe huku tumboni akose baba?”

“Baba yake si huyo anaye toka uingereza.....Ni mara mia ungenidanganya basi kuwa hiyo pete uliyo ivaa nip ambo lakini kabisa unalipanua domo lako EDDY NIMEOLEWA”
Madam Mery akazidi kulia kwa uchungu na nikazidi kumuona ni muigizaji kwa maana kipindi cha mwisho kufanya naye mapenzi alilazwa hospitali kwa madai ya kuumwa ugonjwa wa malaria
“Eddy siku tuliyofanya mapenzi ndipo nilipata mimba ya huyu kiumbe chako tumboni na wala sio mimba ya mume aliye niona”
“Ahaaa kwahiyo unataka mtoto akizaliwa awe na rangi za Uingereza uingereza si ndio”
“Eddy Eddy”
‘Eddy nini...kama mimba ni ya kwangu basi mumeo kaja kamalizia ukarabati wa rangi ya mtoto”
“Eddy nyamaza sasa kumbuka mimi pia ni mwalimu wako”
“Usinge nivulia nguo kama wewe ni mwalimu wangu......Sasa ni hivi sihitaji tena uhusiano na wewe sawa?”
 
Nilizungumza kwa hasira huku nikipiga hatua za kuufwata mlango wa kutokea ndani ya chumba.Kabla sijaufikia Madam Mery akalishika shati langu kwa nyuma huku akilivuta hadi baadhi ya vifungo vikakatika nikageuka kwa hasira na kurusha ngumi iliyotua tumboni Madam Mery na kumfanya atoe ukulele mkali huku akijikunja na mikono yake ikiwa imelishika tumbo lake
“Eddy Unaniua?”
 
     Madam Mery alizungumza na kuanguka chini na damu zikaanza kumtoka mdomoni,Hasira yote nikajikuta ikiniisha na nikipiga goti moja chini na kumtazama na Madam Mery na kumkuta akihema kwa shida kama mtu mwenye ugonjwa wa pumu,Gafla mlango wa chumbani ukafunguliwa na akaingia Madam Rukia na baada ya kumuona mwenzake yupo chini akaanza kupiga makelele huku akiwa anakimbilia sebleni.Nikanyanyuka kwa haraka na kutoka nje na kumkuta Madam Rukia akiminyana kuufungua mlango wa kutoka nje.Nikamshika kiuno na kumnyanyua juu juu na kumtupa juu ya sofa
 
“Unataka kufanya nini?”
Nilizungumza kwa sauti ya juu kiasi kwamba hadi mimi mwenyewe nikajishangaa kwani katika maisha yangu sikuwahi kuzunguamza kwa sauti ya namna hiyo
“Eddy umemuua Mery”
“Acha ufala una uhakika amekufa”
“Ohooo Mama weee Eddy umeuaa ohooo majirani.......”
 
    Nikamuwai kumziba mdomo Madam Rukia anaye waita majirani wamsaidie na nikachukua vitambaa viwili vya makochi na kumsokomeza navyo mdomoni kisha nikavua mkanda na kuifunga mikono yake kwa nyuma.Kisha nikamnyanyua na kumuweka begani na kabla sijatoka njee nikasikia sauti ya Madam Mery akiomba msaada.Nikatoka hadi nje na kufungua buti ya gari na kumuingiza Madam Rukia na kwa uzuri nikakuta kamba ya manila ambayo nikaitumia kwa kumfunga miguuni 
 
“Ukileta upumbavu nitakwenda kukutupa sehemu usiyo ijua na sitaki using** sawa wewe Malaya”
 
Madam Rukia akaitika kwa kutingisha kichwa akiashiria amenielewa ninacho kizungumza,Nikaifunga buti ya gari na kurudi ndani na kumkuta Madam Mery akiburuzika chini huku akiwa amelishika tumbo lake na damu zikiendelea kumtoka mdomoni.Nikanyanyua na kumuingiza ndani ya gari nikafungua geti na kulitoa gari nje kisha nikalifunga na kurudi ndani ya gari na kumpeleka Madam Mery katika hospitali ya mkoa.Manesi wakampoke Madam Mery na kuanza kumuhudumia nikabaki nikiwa ninajilaumu kwa kitendo nilicho kifanya.
“Wewe ndio uliye mleta huyu mgonjwa?”
“Ndio”
“Nifwate ofisini”
 
Nikaongozana na Mzee mmoja aliye valia koti jeupe na tukaingia ofisini kwake na nikakaa kwenye kiti nilicho kikuta na yeye akakaa kwenye kiti chake
“Hali ya mgonjwa wako sio nzuri kwani kwa uchunguzi wa Utrasound tumegundua mfuko ake wa uzazi umepata mstuko na kupelekea mzunguko wa kiumbe kilichopo tumboni kwake kuhama kwenye njia”
“Dokta nenda kwenye point maswala hayo mengine hembu yaache.Je mgonjwa wangu atapona au haponi”
“Atapona ila itatulazimu tumfanyie upasuaji mdogo”
“Utagharimu kiasi gani cha pesa?”
“Laki saba”
“Haaa kwenye hiyo lakisaba mtoto atakuwa hai au amekufa AU kuna chenchi ambayo itarudi?”
“Hapa tunahitaji tumfanyie huo upasuaji leo hii la sivyo tunaweza kumpoteza mama na mtoto”
“Hakuna punguzo la hiyo pesa”
“Kijana hiyo ni kwa opareseni ndogo”
“Hujuanielewe wewe ninaamana kwamba hamuwezi kunipunuzia hicho kiasi cha pesa”
“Haiwezekani”
 
Nikaitoa simu mfukoni nikiwa ninafikiria jinsi ya kumpaga Sheila hadi anipatie kiasi hico cha pesa.Moyo ukanipasuka baada ya kukuta missed call kumi za namba ambayo huitumia Sheila,Nikaipiga namba ikakatwa nikapiga kwa mara ya pili ikakatwa nikapiga kwa mara ya tatu ikapokelewa
“Sheila ,mbona unanikatia simu wewe?”
 
“Samahani kaka mgonjwa wako amekunywa vidonge vingi kwa lengo la kujiua ila tunajitahidi kuyaokoa maisha yake”
“Wee......wee......nees....i imekuwaje haaad....i anywe sum...uu?”
Nilipata kugugumizi cha gafla na kuzidi kuchanganyikiwa kiasi kwamba nikatamani ardhi ipasuke na inimeze kwani likiisha tatizo hili linaanza jengine kubwa kupita la kwanza
“Hatukujua tatizo ni lipi lililo mfanya anywe vidonge vingi.Ila jitahidi uwahi kufika hapa hospitalini”
“Haaa...yaaa nesi”
 
Nikakata simu kwa haraka haraka nikaiweka mfukoni nikakumbuka nguo niliyo ivaa ambayo ni jeans inanibana ndio maana simu ikajiweka silence kutokana ni screan touch kujiminya minya kutokana na mishemishe nilizotoka kuzifanya muda mchache ulio pita.Nikatoa wallet yangu na kuchuomoa kiasi chote cha pesa kilichopo ndani ya wallet na kumuwekea daktari mezani
“Hakikisha mgonjwa wangu anapona.Kama pesa imepungua nitakuja kuilipa”
 
    Nikafungua mlango na kutoka huku nikikimbia na nikapishana na manesi wakiwabeba baadhi ya wanafunzi wa shule yetu walio jeruhiwa katika vurugu zinazo endelea shuluni kwetu.Nikaliwasha gari na kuondoka eneo hospitali kwa kasi huku kichwa changu nikihisi kitapasuka kwa mawazo makali yaliyo nizonga.Nikajikuta nikikanyaga breki gafla kwa nguvu hadi gari ikaanza kuserereka barabarani huku nikijitahidi kumkwepa muendesha baiskeli aliye jiingiza barabarani na kukuta nikimvaa dada anaye tembea pembezoni mwa barabara na kumtupa kwenye mtaro uliopo mbembezoni mwa bararabara
 
    Nikatulia kama dakika tatu nikiyasikilizia mapigo ya moyo jinsi yanavyo nidunda yakienda sambamba na mwili wangu kutetemeka.Watu wenye hasira kali wakaanza kulisonga songa gari kangu huku wakiniomba nishuke kwenye gari.Nikapiga honi na kukunyaga mafuta na kuwafanya watu watawanyike na kulikwepa gari langu huku wengi nao wakijirusha kwenye mtaro.Kwa kupitia kioo cha pembeni nikaona pikipika zikinifukuzia.
Nikaongeza mwendo na nikafanikiwa kuwapoteza kwenye macho yao na kuingia katika barabara ianyo elekea porini.Baada ya umbali wa kilomita 7 taratibu gari ikaanza kupunguza mwendo huku sauti ya kike ikiniambia niongeze mafuta haraka iwezekanavyo la sivyo gari itazimika
 
      Nikaliingiza gari kwenye kichaka na kulizima nikashuka na katika eneo zima nililopo hakuna nyumba ya aina yoyote na sijui kama kuna uwezekano wa binadamu kuishi katika eneo hili.Nikainama huku kichwa changu nikiwa nimekiweka kwenye sehemu ya juu ya gari huku machozi yakinitirikika na kwaharaka haraka nikaanza kuyakumbuka maneno ya mama alivyokuwa akiniambie nikasome.Nikaona kulilia sio suluhisho la mimi kuweza kupata msaada wa kujitoa ndani ya msitu huo kwani kuna umbali mkubwa sehemu niliyopo hadi barabarani.
Nikakumbuka nimemuweka Madam Rukia kwenye buti la gari,nikazunguka kwa hatua za taratibu zilizo jaa uvivu na nikalifungua buti la gari na kumtoa vitambaa Madam Rukia bya mdomoni
“Eddy wewe ndio umenifanyia hivyo”
“Zungumza taratibu la sivyo nitakusokomeza hii mitambara”
“Eddy una akili vizuri wewe?”
“Usinivuruge na wewe”
Nikalifunga buti la gari kwa nguvu na kuufungua mlango wa nyuma na kukaa na kumuacha madam Rukia akiniomba nimfungulie.Nikanyanyuka kwa hasira na kuulifunga buti na kumtazama madam Rukia kwa macho makali
“Eddy naomba unifungue sinto piga kelele tena”
“Ukipiga”
“Nifanye chochote unacho taka”
“Ole wako sasa unizingue nitakuacha huku huku porini”
“PORINI....!!?”
“Ndio porini kinacho kushangaza wewe ni kipi?”
“Eddy jamani mbona unaroho mbaya hivyo umeamua kweli unilete huku porini”
 
“Bwanaa wee sitaki maswali yako ya ajabu na kama unataka kukaa humu ndani ya hili buti wewe endelea kunikera”
Nikamfungua kamba ya miguu madam Rukia kisha nikamtoa kwenye buti na akasimama kwa miguu yake.Nikamfungua mikono yeke na mkanda nikuaweka ndani ya gari na Madam Rukia akaanza kushangaa shangaa
“Eddy huku ni wapi?”
“Hata mimi sijui ni wapi?”
“Umefikaje fikaje?”
“Sitaki maswali hembu niache kwanza hapa kichwa kimevurugika”
 
Madam Rukia akawa mpole na kukaa kwenye moja ya gogo la mti lililopo kwenye kichaka hichi huku sura yake ikianza kujawa na hofu na machozi yakaanza kumwagika taratibu
“Eddy ina maana Mery ndio amefariki?”
“Hajafa”
“Hajafa wakati nimemuona kabisa ahemi?”
“Nimekuambia hajafa”
Nikaito simu yangu inayoita mfukoni na kukuta ni namba anayo itumia Sheila mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio kiasi kwamba nikasita kuipokea ikaita hadi ikakata,Ikapigwa tena na kuipokea pasipo kuzungumza kitu cha aina yoyote
 
“Eddy mume wangu upo wapi?”
Sauti ya Sheila ilizungumza huku akionekana kuchangamka kiasi kwamba nikabaki nikiwa na mshangao
“Eddy mbona huzungumzi kitu chochote mume wangu?”
“Wewe nesi si ameniembai kuwa umekunywa sumu?”
“Tulikudanganya mume wangu........”
“Kwanini sasa ulinidanganya?”
“Nilipoona ninapiga simu hupokei nikajua utakuwa umekwenda shuleni kwenu kwenye vurugu ndio maana nikaamua kula mchongo na nesi”
“Huo sasa ulio ufanya wewe ni ujinga.....Unaona sasa nimejikuta nipo porini?”
Sheila akaanza kucheka huku nikisikia sauti nyingine ya nesi akicheka
 
“Mume wangu huku porini umekwenda kufanyaje au umekuwa ndege”
“Sheila kuna wakati wa utani na mwingine kuna wakati wa serious na ninavyo zungumza hivi sasa nipo kwenye msitu ambao sijui unaitwaje na gari imekata mafuta”
“Wee.......kweli mume wangu acha kunitania!!?”
“Nimesha wahi kukutania mimi?”
“Hapana mume wangu sasa ilikuwaje?”
“Bwana nilimgonga mtu barabarani ndio nikakimbikia huku porini baada ya watu kunifukuzia na laity ningekuja huko hospitalini ingekuwa ni majanga”
“Mungu wangu sasa itwakuwaje mume wangu?”
“Sijui hata itajkuwaje?”
 
“Na mimi simu yangu imepotea jana kwenye ugomvi kuna majina ya watu ambao ningekuwa nayo ingekuwa rahisi kuwasiliana nao”
“Sasas itakuwaje.......”
“Nimekumbuka tazama kwe.......”
Ukimya ukatawala kwenye sikio langu nikaitazama simu yangu na kukuta ikiwa imezima chaji
“Madam una simu hapo?”
“Sina simu zangu zote nimeziacha nyumbani kwa Mery”
Nikajaribu kuiwasha simu yangu ila ikawa ina zima kiasi kwamba ikafika hatua hata nikiwasha haionyeshi mwanga wa aina yoyote.Nikangia ndani ya gari na kukunjua siti na kujilaza nikaanza kuyafikiria maneno ya mweisho ya Sheila yana maana gani
 
“Tazama kwenye nini sasa?”
   Nikajikuta nikijiuliza swali nanikaanza kufungua kwenye kimlango kidogo kilichopo mbele ya siti ya abiria na nikakuta waya wa USB cha kushukuru Mungu unaingiliana na simu yangu.Nikaichomeka kwenye sehemu ya USB iliyopo kwenye gari na chaji ikaanza kuingia taratibu.
Gafla nikasikia vishindo vya mtu akikimbia nikanyanyuka kwa haraka na kumuona Madam Rukia akipotelea kwenye miti nikalifunga gari na funguo nikaziingiza mfukoni na nikaanza kumkimbiza
 
Kadri ninavyozidi kuongeza mwendo ndivyo jinsi Madam Rukia anavyo ongeza kasi ya kukimbia.Nikaongeza kasi ya kukimbia zaidi yake na nikafanikiwa kumnyaka na nikamlaza chini huku akijitahidi kujichomoa mikononi mwamngu huku akinipiga makofi mfululizo
 
“Mbona unaabari za ajabu wakati wewe ni mtu mzima ulikuwa unakwenda wapi?”
Mamda Mery akaendelea kunipiga makofi akiniomba nimuachie gafla nikaanza kusikia mazungumzo ya watu wakiulizana sauti ya kike inatokea wapi.Nikamziba mdomo Madam Rukia kwa kutumia kiganja changu kisha tukajificha kwenye miti iliyo banana.Watu hao wakendelea kutafuta huku na huku ila hawakutuona na baada ya muda wakaondoka zao.Madama Mery akanikumbatia huku akilia sikujua kilicho mliza
“Unalia nini?”
“Eddy nasukuru kwa kuniokoa”
“Nimekuokoa wapi?’
 
“Kwa maana kama ningekutana na hao jamaa wangenibaka”
“Una uhakika gani kama wange kubaka?”
“Nina uhakika kwani ndio kazi yao.Wanaitwa BLACK FOREST PEOLPLE”(Watu weusi wa msituni)
Nikaanza kupata wasiwasi juu ya gari nililo liacha kwenye kichaka,nikamuachia Madma Rukia na akaanza kunifwata kwa nyuma hadi tukafika kwenye gari.Nikalikuta lipo katika hali yake ya kawaida kama nilivyo liacha.Simu yangu kidogo ikawa imeingia chaji nikaiwasha na kuipiga namba aliyo itumia Sheile ila mtandaao ukaanza kusumbua
 
“Shiiti”
“Nini Eddy?”
“Network imekata kabisa”
“Labda ujaribishe kusimama pele juu ya kile kisiki”
Nikasimama juu ya jisiki cha mti ambao inaonekana ulikatwa kwa matumizi ya mbao nikaunyoosha mkono wangu juu ila mtandao haukukaa sawa na muda tayari ulisha songa sana huku baridi kali ikitawala ndani yam situ tuliopo.Hadi inafika saa moja usiku hatukuweza kupata mawasiliano kwenye simu niliyo nayo.Tukaingia ndani ya gari na kujifungia kwa ndani huku kila mmoja akiwa amejilaza kwenye siti yake akatafakari yanayo msibu
 
Madam Rukia akaanza mchezo wa kunishika shika mapaja nikajikausha huku nikimsikilizia ni nini atakacho fwatia.Akanifinya na kunifanya nigune kwa maumivu makali kisha akauchukua mkono wangua ambao kwa sasa nikaanza kuhisi maumivu makali kwenye viganja vya mikono na akinishikisha kifuani kwake na nikaanza kuyaminya maziwa yake taratibu kiasi kwamba Madam Rukia akaanza kutoa mihemo ya nguvu
 
“Tushuke kwenye gari humus into kufaidi”
    Madam Rukia akaniambia na sikuwa mbishi tukashuka kisha nikatafuta sehemu iliyo tulia ambayo sio mbali na lilipo gari.Madam Rukia akawa kama amelishwa pilipili kichaa kwa maana akaanza kazi ya kuinyonya koki yangu kwa fujo kisha akaikalia taratibu na kazi ikaanza huku kiuno chake kikiwa na kizi ya kuikatikia koki yangu.Gafla nikamziba mdomo baada ya kuanza kusikia mazungumzo mengine ya watu wanao onekana kuchoka na safari yao
“Mimi nimesema huku sipo tunapo kwenda tumepotea jamani”
 
“Hembu niacheni jamani na uzee huu mutaniua mimi”
“Mkuu hembu jitahidi tambua tumeingia kwenye hii kesi kwa ajili ya kuyaokoa maisha yako sasa unapoleta habari za kuchoka unadhani tuta kuelewaje?”
“Lakini si nana walipa?”
“Hata kama”
“Nyinyi nisindikizeni hadi mpakani mwa Tanzania na Kenya kisha niacheni nitajua wapi kwa kwenda ila na umri huu sipo tayari kabisa kuingia gerezani”
“Sasa mkuu ilikuwaje hadi yule kijana akakuona?”
“Yaani hata mimi sielewi ilikuwa kuwa vipi kwa maana ile hoteli sikudhani kama ipo siku nitakutana na mwanafunzi wangu”
 
“Mmmm alafu yule dogo anajiamini”
“Anajiamini kutokana wazazi wake ni wazito serikalini ila haki ya MUNGU nikija kumtia mikononi nitakumbukia enzi zangu za jeshini za kulenga shabaha na bunduki yaani nitahakikisha risasi zote zinamuishia mwilini mwake”
“Utampataje wakati ndio tayari umekinukisha”
“Hii dunia milima haikutani ila binadamu tutakutana tu”
Gafla nikaiminya simu yangu mfukoni hukuzuia mlio wa maesseji unaoingia na kuwafanya watu wanao zungumza kukaa kimya huku wakionekana kustushwa
“Hiyo simu ni ya nani?”
 
“Ahaa ni simu yangu ni ujumbe kutoka Voda”
Mwalimu mmoja alijibu na kuyafanya mapigo yangu ya moyo kutulia na Madam Rukia akawa anatetemeka kwa woga,Nikawachungulia na nikawaona waalimu watatu wa kiume akiwemo na mkuu wa shule akongeza idadi yao na kuwa wanne
 
Nikaitoa simu yangu taratibu na nikaiweka sinlence na kuupunguza mwanga wake na nikaisoma meseji iliyo ingia nayo pia inatoka Voda
 
“NDUGU MTEJA SAMAHANI KWA MTANDAO KUTOKUWAHEWANI KWA TAKRIBANI MASAA MATANO HII NIKUTOKANA NA SABABU ZILIZOPO NJE YA UWEZO WETU.ENDELEA KUFURAHIA VODACOM”
Nikamaliza kuusoma ujumbe wa simu ulio ingia na gafla tukasikia hatua zikija upende wetu
“Mkuu unakwenda wapi?”
 
“Ninajisaidia haja ndogo mara moja”
Mkuu wa shule na akasimama eneo tulilo jificha na Madam Rukia huku kila mmoja akiwa nguo zake amezivaa vizuri baada ya kuwasikia walimu hawa mambao walinitoroka mchana wakizungumza.Mkuu wa shule akaanza kukojoa huku akipiga mluzi akiisikilizia raha ya kukojoa na mkono wake mmoja ameshika bastola yake na gafla Madam Rukia akakohoa na kumfanya mkuu wa shule kugeuka na macho yake na yangu yakakutana huku akionekana kuto amini kuniona katika eneo hili

 ITAENDELEA....
RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 21 & 22 Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )  RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 21 & 22 Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea ) Reviewed by WANGOFIRA on 21:36:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.