Picha ya Rais Zuma wa Afrika Kusini akimbusu msichana huyu yawa gumzo

Picha ya msichana akimbusu Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma imezua utata nchini humo.

Picha hizo zilisambaa Jumatano hii baada ya msichana huyo kuziweka kwenye mitandao ya kijamii. “We will check the matter,” alisema msemaji wa serikali Bongani Ngqulunga alipoulizwa kuhusu picha hizo.

Msichana huyo mwenye miaka 19 anaitwa Lindokuhle Dlamini. Kwenye picha hizo aliandika: He is not just a blesser, we are inlove and I am grateful for all that he has done for me, much love. Xo xo.”

Blesser inamaanisha ni mtu mzima anayehonga wasichana na kuwa na uhusiano nao. Akaunti yake ya Facebook imefutwa.

Hata hivyo mtoto wa kiume wa rais huyo, Edward amedai kuwa msichana huyo ni dada yake na kwamba akaunti iliyopost picha hizo ni feki. Baadhi ya magazeti likiwemo Citizen‚ yamesema yaliambiwa na wasomaji wake kuwa ni kweli binti huyo ni mtoto wa Zuma.

Hata hivyo Makamu wa Rais wa Economic Freedom Fighters Floyd Shivambu alikosoa kwa kutweet: Okay cool? What kind of Grand Fathers and Fathers kiss their Grand Daughters & Daughters like this? Perverts??”

Serikali bado haijatoa majibu kama ilivyoahidi.
Picha ya Rais Zuma wa Afrika Kusini akimbusu msichana huyu yawa gumzo Picha ya Rais Zuma wa Afrika Kusini akimbusu msichana huyu yawa gumzo Reviewed by WANGOFIRA on 20:21:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.