Riwaya:Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya Kumi na Tano
MTUNZI:ENEA FAIDY
...DORICE
alikuwa akiyatafakari maneno ya malkia wa himaya aliyokuwepo kwa wakati
ule. Alikuwa haelewi afanye nini na achague lipi kati ya kifo au
kuolewa na jini. Alijikuta yupo kwenye wakati mgumu sana mpaka akajuta
kutoroka shuleni. Alimlaani sana Doreen kwani ndiye chanzo cha matatizo
yote. Alijikuta analia bila kujua msaada wake utatoka wapi.
Akiwa
katika wimbi la mawazo alishtushwa na harufu Kali ya marashi
iliyomfanya azinduke na kumtazama mgeni wake. Alipoinua kichwa chake
alikutana tabasamu mwanana kutoka kwenye sura nzuri ya upole ya kijana
Mansoor.
"Nakupenda
Dorice.. Olewa na Mimi!" Alisema mansoor kwa sauti tamu iliyojaa huba.
Lakini sauti na maneno hayo habvikuwa kitu kwa Dorice, aliachia sonyo
Kali iliyodhihirisha chuki kuu dhidi ya Mansoor.
"Kama
kuniua niueni! Siwezi kuolewa nawewe!" Dorice alisema maneno hayo kwa
ujasiri sana bila kujali jambo hilo lingeonekanaje kwa Mansoor.
Mansoor
alihuzunika sana, akatikisa kichwa kama ilivyokuwa kawaida yake .
Akashindwa kuyazuia machozi ya damu machoni mwake lakini Dorice hakujali
hilo.
"Dorice!
Kwanini haunipendi? Au kwa sababu Mimi sio binadamu mwenzio?" Aliongea
Mansoor kwa huzuni sana lakini Dorice hakujibu kitu.
"Tafadhali niambie Dorice... Nikufanyie nini ili uamini kuwa nakupenda?" Aliuliza mansoor kwa sauti ya upole.
"Utanifanyia?"
"Ndio Dorice!"
"Naomba unirudishe duniani..."
"Nikikurudisha sasa nitakuoaje? Siwezi ishi mbali nawewe!"
"Umesema utanifanyia nikuombacho.. Umeniahidi!"
"Ndio ila hilo suala gumu... Kwanini hunipendi?"
"Nampenda
mtu mwingine.. Na ndie aliyenifanya nipate matatizo haya yote.." Dorice
alisema maneno hayo huku machozi yakimlengalenga kwani kila
alipomkumbuka Eddy alidondosha chozi na hakutaka kuamini kama Kweli Eddy
amemwacha na yupo na Doreen.
"Unampenda nani?"
"Nampenda
mtu anaitwa Eddy, siko tayari kimkosa nataka nipiganie penzi langu...
Samahani sana Mansoor... Wewe ni mzuri ila sins hisia na wewe kabisa!"
Dorice alijikuta akiropoka maneno hayo yote ili kufikisha hisia zake kwa
Mansoor. Maneno Yale yaliugusa vyema moyo wa Mansoor, alihuzunika sana
ila ilibidi akubaliane na ukweli.
"Nashukuru
kwa kuwa mkweli Dorice.. Nakupenda sana ila siwezi kukulazimisha
unipende... Hakutakuwa na mapenzi hapo.. . Naumia sana ila inabidi
nizielewe hisia zako!" Alisema Mansoor kwa sauti iliyojaa masikitiko
makubwa sana ila hakuwa na jinsi. Mansoor alikuwa ni mini mstaarabu
kupita kiasi ingawa mama take alikuwa katili tena mwenye roho mbaya
sana.
"Umenielewa Mansoor?!"
"Ndio.. Nimekuelewa sana! Ila nisimulie ilikuwaje?"
Dorice
alifuta machozi na kutabasamu kidogo ingawa bado alikuwa na maumivu ya
mapenzi kwa Eddy. Akajua ule ni msaada wa kwanza kwake kwenye eneo lile,
akaamua kumsimulia kila kitu kama ilivyokuwa kati ya yeye na Eddy na
kisa cha kutoroka.
Mansoor alihuzunika sana, akamwonea huruma sana Dorice.
"Binadamu wabaya sana..!"alisema Mansoor.
"Inaniuma sana! Nampenda sana Eddy..!"!
Mansoor alichukua kitu kama kioo, akakitazama kwa muda kisha kikamletea picha ya Doreen.
"Mh! Huyu Doreen.. Ni mtu mbaya sana .. In mtu hatari kupita kawaida..!"
Alisema Mansoor kwa mshtuko huku akimtazama Dorice. Dorice alikuwa haelewi chochote akabaki akishangaa tu.
"Doreen
ni mchawi sana.. Na kuna kitu anatafuta! Amemharibu sana Eddy... Eddy
yupo kwenye wakati mbaya na muda wowote anammaliza..!"
Maneno ya Mansoor yalimshtua Dorice
"Amemfanyaje? Nisaidie kumwokoa Eddy tafadhali..!"
"Mama hatanikubalia ila inabidi nikusaidie Dorice.. Yote ni kwasababu nakupenda.. Nitakusaidia usijali!"
Alisema Mansoor.
"Nitafurahi sana ukinisaidia Mansoor!"
"Usijali.. Ila mama ni kikwazo..!"
"Jitahidi Mansoor!"
Dorice
alichanganyikiwa sana baada ya kusikia kuwa Eddy atauliwa muda wowote
na Doreen, ilibidi azidi kumsihi Mansoor aweze kumsaidia kwa namna
yoyote ile kwani alitambua uwezo mkubwa aliokuwa nao jini yule
mstaarabu.
******
Doreen alibaki pale chini kwa muda mrefu sana akishindwa kutoka mle ndani.
Alihangaika
sana mpaka kijasho kikaanza kumtoka kwani aliziona kabisa dalili za
kufamwa, aliwaza aibu ambayo ingemkuta hakujua afanyaje.
Akiwa
katika harakati hizo za kutaka kuondoka akahisi moto mkali ukimpitia,
akapiga kelele za maumivu huku akigalagala pale chini. Chumba kizima
kilikuwa kimya sana kwani wanafunzi wote walikuwa wamelala fofofo na
hakuna aliyeweza kusikia kilio kile.
Doreen aliteseka sana na tangy aanze uchawi hakuwahi kukumbana na hali ile.
Aliona uchawi sasa ni wa mateso, kwani maumivu aliyokuwa anayapata hayana mfano.
Doreen
alijitahidi kufanya kila awezalo ili aweze kutoka ndani ya bweni lile
lakini halo ikazidi kuwa mbaya. Ghafla akasikia mtu akikohoa akajua
mwisho wake umefika. Akaanza kuropoka maneno yake ya uchawi ili aweze
kutoka hatimaye akafanikiwa. Ikawa ahueni yake ingawa mwili wote ulikuwa
unamuuma vibaya sana.
Alifika
kwenye kichaka ambacho aliacha vitu vyake, akajibwaga kama mzigo huku
akiugulia maumivu. Aligalagala pale chini kwa muda wa SAA zima hatimaye
maumivu yakapungua. Akaamua kurudi bwenini kulala.
Alinyatanyata mpaka alipokifika kitanda chake. Alilala huku akimfikiria Nadia.
"Mh! Huyu mtu si wa mchezo dah!" Alijisemea Doreen kimoyomoyo, kwa maumivu aliyoyapata hakuweza hata kuinuka kitandani.
"
Nitafanyaje Mimi? Siku zimeisha sana sasa lakini bado kitu kimoja tu,
titi la msichana mzuri! Nitapataje sasa?" Alijiuliza Doreen bila kupata
majibu.
"Enhe!
Inabidi nifanye kitu.. Nimtumie MTU..!" Doreen alipata wazo kuwa
inabidi amtumie mtu ili kupata titi hilo ili akamilishe mambo
aliyoyahitaji. Lakini asingeweza kufanya kwa usiku ule kwani alikuwa hoi
bin taabani.
Usingizi ukampitia kidogo na kwakuwa ilikuwa SAA kumi na nusu hakulala sana kengele ya kuamka ikamshtua.
Kulikuwa
tayari kumekucha. Doreen alikuwa hana nguvu kabisa mwilini na mwili
wake ulikuwa bado unamuuma hivyo akashindwa kwenda darasani kwa madai
kuwa alikuwa mgonjwa. Ila moyoni alimwogopa sana Nadia na hakutamani
hata kumwona kwani alimuonea aibu.
Wanafunzi
wote walienda darasani isipokuwa Dorice, alibaki bwenini na alitaka
kuitumia nafasi ile vizuri ili amtumie mtu kutafuta titi la msichana
mzuri wa kuvutia.
******
Wazazi wa Eddy walishika njia kutokea mkoani Iringa kuelekea pangani Tanga.
Walikuwa na matumaini mazito ya kumpata mganga mashuhuri aitwaye Tembo wa Bahari.
Hawakua
na wasiwasi wowote juu ya mganga huyo kwani tayari walikuwa wamezisikia
sifa zake kuwa yupo vizuri sana katika suala la matibabu.
Eddy alikuwa ametulia kimya ndani ya gari lile ambalo dereva alikuwa ni Mr.Alloyce.
Kila
Mara aliyakumbuka maneno ya Doreen kuwa endapo watafika kwa mganga basi
uhai wake utakuwa umefikia kikomo. Kuna wakati aliyapuuzia mawazo hayo
lakini wakati mwingine alihisi yana ukweli ndani yake, kama Doreen
aliweza kumtoa sehemu zake nyeti atashindwa kumuua? Alijiuliza Eddy.
Ukimya ulitawala ndani ya gari lakini kelele nyingi zilitawala kichwani mwa Eddy kwani mawazo yalikuwa hayakauki kichwani mwake
"Mama!" eddy aliita.
"Sema mwanangu..!"
"Nina njaa!"
"Ngoja nikupe chakula..!"
Mama Eddy alichukua hotpot na kumtolea mapaja ya kuku yaliyokaushwa vizuri pamoja na chipsi mayai zilizoshikana vizuri.
"Chukua ule.."
"Sawa! Ila nipe chakula!"
"Mh! Chakula hicho!"
"Hicho siwezi kula maana kina uchafu..!"
Alisema Eddy maneno yaliyomchanganya sana mama yake kwani kila alipotazama chakula kilikuwa kizuri tu.
"Hakuna uchafu..!"
"Upo!"
Eddy alisisitiza na Mara hiyo akaanza kuhisi kichefuchefu.
"Mama
simamisheni gari nataka nikatapike nje.."alisema Eddy. Kwa haraka
Mr.Alloyce alisimamisha gari wakamtoa nje Eddy ili akatapike.
Eneo like lilikuwa na miti mingi kwani lilikuwa pori. Eddy aliwatazama wazazi wake, kisha akasogea kando kidogo.
Akawatazama tena kwa jicho la wizi , akajiweka sawa kisha bila wazazi wake kutarajia akatimua mbio Kali kuelekea porini.
Wazazi
wake wakapigwa butwaa sana wakashindwa wafanye nini wakabaki wamezubaa
huku wakitazama kwa mshangao. Eddy alikuwa tayari amewapotea machoni
mwao kwani mbio alizokuwa akikimbia zilikuwa za MWENDOKASI.....
ITAENDELEA...........
Riwaya:Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya Kumi na Tano
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:11:00
Rating:
No comments: