RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 33 & 34 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )
Mtunzi:EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA....
“Duu kweli malipo ni hapa hapa duniani?”
“Kwa nini baba?”
“MAMA YAKO NI KATILI SANA TENA ZAIDI YA SANA JAPO USONI MWEKE NI MWAMA KUPITILIZA”
Maneno ya baba yakanicha mdomo wazi huku nikishangaa nisijue ni kwanini amesema mama yangu ni katili sana
ENDELEA...
Nikaendelea kumtazama baba kwa macho ya mshangao
“Mama
yako ni katili sana kiasi kwamba aliyaaribu maisha yangu kwa kiasi
kikuwa....Kipindi ambacho wewe bado hujazaliwa tulikuwa tunapendana sana
na kaka yangu na kwajinsi tulivyokuwa tunapenda tuliamini kwamba hakuna
kitu amaco kitaweza kutuchonganisha...Ila ninanakumbuka kipindi baba
yaka anaingia jeshini mimi nilifeli majaribio kutokana kipindi kile
nilikuwa ninaumwa na ugonjwa wa miguu”
“Basi
baba yako akaja kukutana na mama yako na kutokana kipindi kile sisi
tulikuwa ni fukara sana na wazazi wetu walisha fariki ikabidi kaka
ambaye nilisha zoea kumuita kurwa aliniomba nihamie kwa mama yako amaye
kwa kipindi kile alikuwa ni daktari ila kwao walikuwa ni matajiri sana
kwahiyo swala la pesa kwake lilikuwa ni la kawaida......
Nakumbuka
ilikuwa ni mwaka 1991 ambapo mama yako alianza kujiingiza kwenye mambo
ya vyama kwa maana uchaguzi ulikuwa unaelekea miaka ya mbeleni.....Mambo
mengi sana akawa ananishirikisha kama mtu wake wa karibu sana kiasi
kwamba ikafikia kipindi tukaanza mahusianao ya kimapenzi pasipo kurwa
kujua na yeye kwa kipindi kile ilikuwa ni ngumu sana kuweza kujua ukweli
kutokana alikuwa yupo kambini kwenye kambi ya jeshi Morogoro na sisi
tulikuwa tunaishi Dar es Saalam”
“Kuseme
kweli mama yako alimpenda sana kurwa na mimi alinichukulia kama
kituliza nafsi.....Ninazungumza ukweli ili uweze kumjua mama yako vizuri
na yale yote aliyo nitendea”
Nikabaki kimya huku nikiendelea kumsikiliza baba hata mat yenyewe mdomoni hayakuweza kupita sikujua ni kwanini.
“Basi
kipindi alipo gundua amepeta mimba yako na ilipo kuwa na wiki mbili
akaanza kutengeneza chuki juu yangu na kipindi kile kwa Tanzania masimu
yetu yalikuwa ni yale ya mezani hazikuwepo kama hizi za siku
hizi,Alipiga simu kambini na kumuomba kaka kuja nyumbani.Basi baada ya
kaka kuja akaanza kuniumiza moyo kwa kufanya mambo yao hadharani huku
mimi nikiwashuhudia.......Kitendo cha mama yako kutuchanganya kiliniuma
sana na nikaapia ipo siku nitamwambia Kurwa kila kitu kinacho endelea
ila kitu ambacho ninakijutia hadi leo ni kwajinsi nilivyo anza kumuambia
mama yako kwamba nitamwambia kurwa ukweli wote wa mambo tuliyo yafanya
na kipindi hicho tayari ujauzio wake ulisha anza kukua”
“Kitu
alicho anza kukifanya mama yako ni kuanza kufanya vitisho vya kutaka
kuniua na akaniomba niweze kuondoka Tanzania kama maisha yangu
ninayapenda.....Ila kutokana alikuwa na damu yangu tumboni nikawa
ninavuta subra niweze kumuona mwanangu amabaye ni wewe....na nililikuwa
na mahusiano ya kimapenzi na mwanamke mwengine ambaye alikuwa
amenihifadhi na baada ya mama yako kutambua kuwa ninamwanamke mwengine
akatua matu na wakatuvamia sehemu ambayo sisi tunaishi na yule
mwanamke....Wa...walimuua kwa kumuingiza chupa sehemu zake za siri na
kumkata maziwa na kitendo hicho kilifanyika mbele yangu”
Baba akatulia kimya huku machozi yakianza kububujika kiasi kwamba na mimi kwa mbali machozi yakaanza kunilenga lenga.
“Na
mbaya zaidi yule mwanamke alikuwa na ujauzito wangu wa mwezi mmoja na
nusu na akafariki na mwanangu tumboni na mimi wakanichoma sindano ya
sumu kiasi kwamba sehemu hii yote ya chini ya mwili wangu ikawa haifanyi
kazi,pamoja na kinywa changu kikawa kimepinda kwa na sikuweza
kuzungumza kitu cha aina yoyote...Basi ninakumbuka kuna daktari wa
kizungu alikuwa ni rafiki yangu sana aliweza kunisaidi na kwake kulikuwa
ni huku Africa kusini....basi nilipo muelezea kuhusiana na yaliyo
nikuta akaamu kunileta kuhu Afrika kusini ambapo nilifanyiwa upasuaji na
ikawalazimu kunikata miguu yote miwili na kutokana yule mzee alikuwa
na pesa sana akaamua kunichongeshea miguu ya bandia ambayo ni kama hii
unayo iona”
Baba
akanifunulia suruali yake na kuiona miguu yake ya chuma ikifanana kama
ya mwanariadha maarufu Afrika kusini ambaye naye ana miguu ya namna
hii,machozi yakaanza kunimwagika huku yakiambatana na maumivu makali ya
moyo.
“Basi
nilianza kufanya kazi kwa yule mzee na kipindi anafariki hakuwa na
mtoto wala ndugu na mali zake zote aliniridhisha mimi na ndio maana
unaniona nina mali nyingi kiasi hichi.....Hayo nileyo kueleza ni
machache ila kuna mengi sana ambayo mama yako alinifanyia ila kutaoka
upo hapa nitakuwa ninakuadisia kila muda utakavyo kuwa unakwenda”
Baba
akatoa kitambaa mfukoni mwake na kunipatia na kuanza kujifuta machozi
ambayo yananimwagika na nikabaki nikiwa sina cha kuzungumza kwani
sikuweza kuamini kama mama anaweza kumfanyia ukatili mtu aliye mbebea
damu yake tumboni.Baba akasimam na kuisogelea meze iliyo jaa mizinga ya
pombe kali kisha akachukua mzinga mmoja na akamimina kiasi cha kidogo
cha pombe kwenye glasi kisha akapiga fumba moja la pombe hiyo huku
akiikunja sura yake akionekana kuwa kitu anacho kinywa ni kikali sana
kisha akaviweka mezani na kurudi sehemu aliyokuwa amekaa kisha akashusha
pumzi nyingi
“Eddy
nilikutafuta sana mwanangu kupitia sehemu mbali mbali hususani
mitandano ya kijamii ila kitu ambacho kilikuwa ni kigumu ni kuto
kulifahamu jina lako.”
Nikaanza
kuyaamini maneno ya baba kuwa mama anaroho mbaya kutokana na jinsi
alivyokuwa akimkataa Manka na kutaka kumsweka gerezani kwa kunipiga
risasa na kitu kingine nilicho kikumbuka ni maneno ya yule dereva taksi
ambaye nilipata naye ajali.
“Haaa
huyu mama naye yupo.....Kweli Mungu hapendi dhambi kuna siku bwana
alikuwa na dereva wake sasa kwa bahati mbaya nikamchomekea kwa mbele ile
barabara ya kuingilia K.C.M.C nilikuwa namuwahisha mgonjwa
hospitalini.Ahaaaa alikwenda kunilaza polisi hadi siku anaondoka Arusha
ndio wakaniachia......Tena hao watekaji kama wanajua wamfanye wa kwanza
kufa kwa maana yule mama roho mbaya sana”
Baba
akanisogelea na kunishika bega na kuniomba ninyanyuke kisha akaniweka
vizuri shati langu na kuniomba twende nje.Akaanza kunitembeza kwenye
eneo la jumba lake la kifahari na kwaharaka haraka utajiri wa baba ni
mara tano ya utaji alio nao mama.Ila moyoni mwangu sikuweza kuiruhusu
chuki iliyopo kati ya wazazi wangu kunitawala moyoni mwangu ila chuki
yangu kwa sasa ilibaki kwa baba mkubwa ambaye amemtekana mama akisaidia
na Emmy mwanamke aliye jitambulisha kama daktari.
Baba
akanionyesha chumba changu kikubwa ambacho nitakitumia kwa kulala na
nikikubwa sana na kina vitu vingi sana vya kuvutia japo kwa mama ni
tajiri ila baba amezidi kuwa na utajiri mkubwa.Muda wa usiku wageni
ambao ni rafiki wa baba wakaanza kukusanyika kwa ajili ya sherehe na
kabla ya sherehe kuanza nikawa nipo kwenye chumba maalumu huku nikiwa na
mwana mitindo ambaye amenitengenezea suti nzuri inayo endana na mimi na
kazi hii ameifanya ndani ya msaa machache jambo ambalo limenishangaza
na hapa nikagundua kuwa wezetu wenye nchi zilizo piga hatua
wamechangamka sana kwenye utendaji wao wa kazi
“Unajionaje kijana?”
Mwanmitindo
aliniuliza baada yakuivaa suti aliyo nitengenezea huku nikiwa
nimesimama mbele ya kioo nikiwa nimependeza kiasi kwamba hata mimi
kimoyo moyo nikaanza kujisifia kabla sijasifiwa
“Imenikaa vizuri?”
“Hakuna sehemu ambayo inakupa shida kwenye kutembea au imekubana sehemu?”
“Sina kila sehemu imekaa sawa”
“Hembu tembea hadi pale mbele”
Nikapiga
hataa kama sita kisha akaniomba nigeuke na kurudi sehemu niliyo simama
awali na hadi ninafika nikasikia makofi yakipigwa na nikageuka na
kukutana na mama mke wa baba kwa sasa akiingia kwa mwendo wa madaha hadi
sehemu niliyo simama
“Unaonekena ni kijana mzuri..mtanashati eheee?”
Sikumjibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kumtazama jinsi anavyo niangalia kuanzia chini hadi juu kwa macho ya dharau
“Josh ninakuomba utoke na tunataka tuzungumze”
Mwanamitindo
akatoka na kutuacha tukiwa tumetazamana na mke wa baba na baada ya
mlango kufungwa sura yake ikabadilika na ikakusanya mikunjo migi ya
hasira.
“Huwezi
kuichukua nafasi ya mwangu mbele ya baba yako,sijui amekuokota
amekununua,amekuiba ila nitahakikisha hapati chochote kwenye uridhi huu
wa baba yako”
Mke wa baba alizungumza huku sura yake akiwa ameikunja na meno yake akiwa ameyang’ata kwa hasira
“Sikiliza wewe mwanamke hunijui sikujui sasa kama unaitaji kunijua utanijua kwa herufi kubwa sawa?”
“Hahaa
sina haja ya kukujua omba omba kama wewe usiye na wazazi na nikawaida
yenu vijana masikini kama nyinyi hapa Afrika kusini kuwaparamia watu
wenye fedha zao na kuwaona ni kama wazazi wenu sasa kama umtumwa na huyo
mama yako Malaya aliye shindwa kukulea basi kamwambie nafasi imkwisha”
Nikamtazama kwa hasira mke wa baba kiasi kwamba mwili mzima ukaanza kunitetemeka,
“Na kingine nitahakikisha humalizi wiki utakuwa umeondoka ndani ya hii nyumba”
“Etiii ehee....?”
“Na hakuna cha Etii ehee mbwa wewe uliye kosa pa kula”
Nikajikuta
nikiunyanyu mkono wangu wa kulia kwa kasi ya ajabu nikaupeleka kwenye
shavu la mke wa baba na kabla haumfikia mlango ukafunguliwa na nikamuona
baba akiingia na nikaushusha chini kwa haraka na kumstukia mke wa baba
akiangua kiliao huku akilishika shavu lake akidai nimepiga kitendo
kilicho zidi kunipandisha hasira
“Mume wangu umeamua kuniletea mwanao aje kuniadhiu mimi....Si ndio?”
Mke wa baba alizungumza kwa sauti ya kufoka na kumuona baba akiwa amenywea na taratibu akaanza kupiga hatau za kumfwata mke wake
“Pole mke wangu.....Eddy mwangu mbona upo hivyo?”
“Yaani mbele yangu unamuita huyo ngedere wako mwanao....?”
“Mke wangu huyo sio ngedere ni mwangangu”
“Wewe vipi kati ya watoto huyo unaweza kusema ni mtoto hembu muangalie anaonekana hivi hivi ni mama yake ni mbwa koko”
Maneno
machafu ya mke wa baba yakanizidi kunikasirisha hadi nikashindwa
kuizuia hasira yangu na kwaharaka nikamchomoa mikononi mwa baba ambaye
anaonekana kuwa anamdekeza mwanamke wake.Nikamvuta karibu ya sura yangu
huku nikiwa nimelishika sehemu ya kifuani kwake kwenye gauni lake alilo
livaa na nikamuona anayafumba macho yake kwa kuongopa
“Nitakuua”
Nilizungumza
kwa hasira na kumsukumia sehemu aliyoo baba na akamdaka mke wake na
wote wakajikuta wakianguka chini kisha mke wake akasimama haraka
“Niue sasa kama unaweza”
Nikapiga
hataa za haraka hadi sehemu aliyo simama na nikamtisha kama ninampiga
kofi akaikuja mikono yake akiuficha uso wake na kwakutuma mguu wangu wa
kulia nikipiga teke miguu yake yote miwili na kumrusha juu kidogo kimo
cha mbuzi na akaanguka chini kama mzigo na kuendelea kulia,nikapiga goti
kwa haraka na kuishika shingo yake na kwa haraka na kumsogelea karibu
“Usidhubutu
siku hata moja kumuambia mama yangu ni Malaya na usinifananishe na
mnyamwa wa aina yoyote na kama unataka kunifananisha nifananishe na
shetani”
“Eddy mwanangu ninakuomba utulize jazba msamehe bure tuu”
Nikaisikia sauti ya baba ikizungumza kwa upole na unyenyekevu na nikamuachia na kusimama na kumaacha akikohoa kohoa
“Baba
kumbe haya ndio maisha unayo ishi na huyu mwanamke asiye na
adamu....anakazi ya kukupelekesha kama boya.Wewe ni mwanaume unatakiwa
kumtawala mwanamke na si mwanamke kukutawala wewe”
“Mwanangu usizungumze hivyo”
Baba alizungumza huku akiinama na kutaka kumpa mke wake mkono ili amnyanyue na kwa haraka nikaiwahi mikono yao na kuichanisha
“Muache anyanyuke mwenyewe na tuone sasa kama atashindwa kunyanyuka”
Nikamsogeza
baba mbali na mke wake ambaye akanyanyuka taratibu huku sura yake ikiwa
imejaa machozi na aibu na akawa ananitazama kwa macho wiziwizi na
akaanza kupiga hatua za haraka kuelekea mlango ulipo na kabla hajaufikia
nikamuita kwa sauti ya ukali na akasimama na nikamfwata hadi sehemu
alipo simama.
“Kinacho kuliza ni nini?”
“Mmmm hakuna kitu”
“Futa machozi”
Mke
wa baba akaanza kufuta mchozi kwa kutumia gauni leke kisha akabaki
akinitazama ninavyo hisi hakuamini kama mimi ninaweza kufanya nilicho
mfanyia mbele ya mume wake
“Nenda kajiandae na kwenye sherehe ninakuhitaji nikuone na nitakaa na wewe”
“Sawa”
Mke wa baba akatoka na kuufunga mlango kwa nguvu na kunifanya nianze kucheka na baba naye akanifwatia kwa kucheka
“Baba hivi huyu mke wako unaishi naye vipi?”
“Wee
acha tuu mwanangu,Afadhali umekuja na wewe kwa maana huyu mwanamke
ananipelekesha sana yaani hadi ikifikia kipindi nikirudi nyumbani tuu
furaha yote inanipotea”
“Sasa kwanini na wewe baba unakuwa hivyo?”
“Yaani hata mimi mwenye sielewi ni kwa nini yaani akizungumza yeye huwa mimi sina la kubisha kwake”
“Kwani umeomtoa wapi?”
“Ahaa
naye ana historia yeke ndefu tuu nitakusimulia siku nyingine...sasa
hivi twende kwenye sherehe nahisi imesha anza na wanatusubiria sisi”
“Sawa baba”
Tukatoka
na baba chumbani na kukuta mwana mitindo mlangoni na baada ya kuniona
anakisimamisha na kuanza kuiziweka nguo zangu vizuri kisha akatoa viatu
vinavyoendana na suti niliyo ivaa ambayo ni ya rangi ya bluu na nikavua
viatu nilivyo vivaa na kuvaa alivyo nipa kisha tukaelekea sehemu yenye
bustani iliyo pambwa vizuri na kukutana na watu wachache ila wamevali
vizuri.Tukakaa sehemu ambayo tumeandaliwa na muongoza sherehe akaendelea
na kazi yake,Macho yangu yakawa na kazi ya kutafuta ni wapi alipo mke
wa baba na nikamuaga baba ninaelekea msalani(chooni) na akamuomba mlinzi
wake mmoja kunifikisha msalani
Nikapita
kwenye moja ya kordo na kumuona mke wa baba akiwa amekumbatiana na
jamaa mmoja huku wakiwa wananyonyana midomo yao,mlinzi naye akashuhudia
tukio hilo na nikataka kwenda ila jamaa akanizuia na kuitoa simu yake
mfukoni na kupiga picha kadhaa na tukaendelea na safari yetu huku moyoni
mwangu nikizidi kupata maumivu nikijiuliza ni kwanini baba anaishi na
mwanamke wa namna hii
Nikamaliza
haya zangu na tukarudi kwenye bustani na hatukuwaoa kwenye eneo walilo
kuwepo,Nikamkuta mke wa bab akiwa amekaa pembeni ya baba huku akicheka
akimtazama mchakeshaji anaye endelea kufanya yake.Nikajikausha huku mara
kwa mara nikimtazama kwa macho makali na nikazidi kuumia pale anavyo
mbusu busu baba machavuni na mdomoni akijifanya kama anampenda sana baba
Wakati
wa kutambulishwa ukawadia na baba akanitambulisha kama mimi ndio mridhi
wake wa pekee kitendo kilicho mchukiza mke wake japo kila nilipo
mtazama akatabasamu akiashiria kuwa anafuaha moyoni mwake.Sherehe
ikaisha huku moyoni mwangu nikitamani kumuambia baba juu ya tukio alilo
lifanya mkewe ila nikaona hatomfanya kitiu chochote.Nikaelekea chumbani
kwangu na nikaoga na kupanda kitandani na mawazo ya wapi alipo mama
yakanza kunitawala kichani kwangu
Nikanyanyuka
na kuisogelea meza iliyo na kumputer aina ya HP,nikaiwasha na kwabahati
nzuri nikakuta imeunganishwa na hudumu ya internet.Nikaingia kwenye
mtandao unao husiana na taarifa za serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania,Nikaanza kutafuta tafuta habari itakayo husiana na mama na
nikakutana na habari ya iliyo andikwa kwa maandishi makubwa ikisema
“WAZIRI WA AFYA ATOROSHWA HOSPITALINI HUKO AFRIKA KUSINI ALIPOKUWA AMELEZWA”
Nikaanchana nayo kwani ni habari iliyo tolewa mwezi na nusu ulio pita na nikakutana na taarifa nyingine inayo husiana na mama.
{“BI MAGRET INASADIKIKA AMETEKWA NA KUNDI LA KIGAIDI LA AL-SHABABI”}
Mapigo
ya moyo yakaanza kuniende mbio na nikaifungua taaribu hiyo na kuanza
kuisoma huku mwili mzima ukinitetemeka hadi nijajikuta ninacho kisoma
sikilewi.
{“Mume
wa Bi Magreti bwana Godwin amabeye ni mkuu wa jeshi kikosi maalumu
amedai kuwa mke wake ametekwa na magaidi hao ambao wanahitaji kiasi cha
dola za kimarekani milioni 50 kutoka kwenye serikali ya Tanzania ili
kumuachia huru waziri huyo”}
{”Raisi
aishutumu serilakali ya Afrika kuwa hawapo makini katika swala la
ulinzi viongozi wanao toka nchi mbalimbali wanao lazwa kwa ajili ya
matibabu katika hospitali zao”}
Nikajikuta
nikijikuna kichwa kiasi kwamba nikahisi nywele nitazitoa kwa
kuzivuta.Moyo kwa moja nilajua kuwa mama hajatekwa na kundi hilo la
magaidi kama inavyo semekana na moja kwa moja atakuwa ni baba ambaye kwa
sasa anajifanya kuwa watekaji ni kundi la Al-shababi.Nikaendelea
kutafuta habai nyingine na kukutana na habari nyingine ikesema
{“HIZI
NDIZO PICHA ZINAZO MUONYESHA WAZIRI BI MAGRET AKIWA MIKONONI MWA
MAGAIDI WALIO TOA SIKU KUMI NA TANO KWA SETIKALI YA TANZANIA”}
Nikaanza
kutazama picha moja baada ya nyengine na kumuona jinsi mama alivyo
fungwa kitambaa cheusi machoni mwake huku kichwani mwake akiwa amewekewa
mitutu kama sita ya bunduki aina ya SMG.Machozi yakaanza kunimwagika
baada ya kuiona picha nyingine ya mama akiwa amechorwa maandishi ya
kiarabu yenye rangi nyekundu kwenye kifufua chake huku mkono mmoja wa
mtu ulio valia gloves nyeusi ukimshika kwenye sehemu ya chini ya kidevu
chake huku akimminya mashavu yake kwa nguvu.
Nikajikuta
mkono wangu ukielekea kwenye kitufe cha kuzimia computer na kurudi
kitandani huku machozi yakinimwagika na hasira ikawa imenikaba kifuani
mwangu hadi nikahisi kifua changu kinaweza kunipasuka.Sikupata usingizi
hadi asubuhi na kitu cha kwanza nikamsubiria baba ili nimpe taaria hiyo.
Baba
akanikuta nimekaa sebleni nikiwa nimeshika tama na baada ya salamu
nikamuomba nizungumze naye na akakubali na akakaa pembeni yangu na
nikanza kumsimulia kuanzai A hadi Z kwa hali aliyo kuwa nayo mama
“Sasa hapo tutafanyaje mwanangu?”
“Una hizo milioni 50?”
“Mmmm hicho ni kiasi kikuwa cha pesa japo ninacho ila ngoja kwanza tujua hiyo hali itakwenda vipi?”
“Basi inanibidi nirudi Tanzania leo?”
“Kwa leo mwangu siwezi kukuruhusu kurudi Tanzania ila ngoja nitwapa hiyo kazi wafanya kazi wangu hiyo kazi”
“Wataiweza kweli?”
“Ndio ila sio hawa una waona hapa kuna wengine nitawapa”
“Lini utawapa?”
“Leo
ngoja tupate kifungua kinywa kisha tutakwenda kwa hao watu wangu na
sipendi waje hapa kwani wanatafutwa sana kwa matukio wanayo yafanya
inanibidi tuwafwate”
“Sawa”
Tukapata
kifungua kinywa kisha nika tukajiandaa kwa ajili ya kwenda alipo
ndiambia baba na tukatumia gari jengine ambao linaendesha na yule mlinzi
wake wa jana sukiku,Ndani ya gari sote tukawa kimya huku akili yangu
ikiwa inamuwazia mama yangu.Tukafika kwenye gorofa moja na baba akashuka
“Eddy nisubirini nikaongee na kiongozi mmoja hapa wa jeshi kisha tutawafwata hao watu”
“Sawa baba ila nina ombi”
“Ombi gani mwanangu?”
“Baba ninaomba pesa ya kununua simu kwa ajili ya mawasiliano”
“Sawa”
Baba
akatoa kikadi cha banki na akaniandika namba zake za siri kwenye
kikaratasi na kumuomba dereva wake anipeleke kwanye ATM za banki na kish
yeye akaingia kweye ndani ya gorofa na sisi tukaondoka.
“Kaka hivi simu za gharama huku nitazipata wapi?”
“Maduka yapo mengi tuu utakapo hitaji wewe nitakupeleka”
“Maduka yanatumia pesa aina ya dola au Rand”
“Inategemea na duka lenyewe linatumia pesa ya aiana gani ila ninakushauri ukatoa dola ya marekani”
“Sawa utanirushia zile picha za jana”
“Sawa”
Tukafika
kwenye gorofa ambalo lina mashine za kutolea pesa(ATM) na tukashuka
ndani ya gari na jamaa akabaki njea na mimi nikaingia ndani.Nikachukua
kiasi cha pesa ya kunitosha hata kwa matumizi mengine kisha nikatoka nje
na kumkuta jamaa akiminyana na dada aliye na nywele zilizo changuka
huku dada huyo akiwa amenipa mgongo na mavazi yake yakiwa yamechafuka na
kuchanika chanika sana.Mwili wake umejaa ukurutu na amepauka sana huku
ukiwa umedhohofika sana japo anaonekana kuwa na nguvu nyingi na
kwaharaka haraka nikatambua kuwa dada huyu ni kichaa.
“Eddy nenda kwenye gari ninakuja sasa hiv....khaaa”
Jamaa
alipiga kelele baada ya dada huyo kumng’ata kwanye mkono kisha
akanigeukia na mimi na kujikuta nikibaki nikiwa nimesimama huku nikiwa
nimemshangaa kichaa huyu kwani ni Sheila mpenzi wangu ambaye mara ya
mwisho kumuona ni siku niliyo gongwa na gari.Nikiwa nimesimama Sheila
akamuachia jamaa na kunirukia mimi na sote tukaanaguka chini huku
nikijitahidi kumshika kichwa chake anacho taka kuning’ata kwa meno yake
yaliyo machafu huku akidondosha udenda mwingi na akinguruma kama mbwa
mkali mwenye njaa kali....
******SORY MADAM******(34)
Mlinzi
akamuwahi Sheila na kumnyanyua juaa na lipindi tukio linatokea askari
waliweza kuliona na wakamkamata Sheila na kabla hawajaondoka naye
nikawazuia
“Jamani samahani kaka zangu ninamuhitaji huyo binti”
“Huyu ni mwenda wazimu na ametoroka katika hospitali ya vichaa na karibia wiki sasa tunamtafuta”
“Sawa nimewaelewa sijui tunaweza tukaongozana hadi sehemu ilipo hiyo hospitali?”
“Kwani wewe unamfahamu huyu binti?”
“Hapana ila ninahitaji kuweza kuyafahamu maendeleo yake”
Askari
wakanitazama kisha wakaniruhusu kama kuongozana nao,tukaingia kwenye
gari letu na kuongozana na askari hadi kwenye hospitali ambayo ni yawatu
walio pungukiwa na akili.Sheila akakabidhiwa kwa madaktari na polisi
wakanionyesha sehemu ambayo ninaweza kupata kawimu za maendeleo ya
Sheila,
“Samahani dada yangu”
Nilimuuliza nesi mmoja niliye mkuta kwenye dirisha la kuudumia wateka wanao hitaji huduma kwenye hospitali hii
“Bila samahani”
“Kuna mgonjwa ameletwa dakika tano zilizo pita na ninaomba kuweza kujua takwimu zake za nyuma”
“Ahaaa
juyo dada aliyeletwa hapa akiwa hajitambui na kadris siku zilivyo zidi
kwenda alikuwa msumbufu anapiga wezake hadi kunasiku alimuua mwenzake
mmoja kwa kumpiga kwa chupa kichwani”
Nikajikuta nikiwa nimeuacha mdomo wangu wazi kwa mshangao kwa maana sikutegemea kusikia taarifa kama hiyo
“Labda tatizo leke kubwa haswa ni nin?”
“Mmmm kwa mimi siwezi kujibu labda ngoja nikukutanishe na daktari ambaye alikuwa akimuhudumia tangu siku ya kwanza alipo kuja”
Akanyanyua
mkonga wake wa simu na kuzungumza na mtu aliyo upande wa pili wa simu
kisha akaniomba niweze kuingia ndani kwenye ofisi ambayo ipo upande
wangu wa kushoto na ikanilazimu kumuacha nje dereva,Nikamkuta daktari wa
kiume mwenye umri mkubwa kiasi na akaniruhusu nikae pembeni kwenye
kiti.
“Nikusaidie nini kijana?”
“Kuna mgonjwa ambaye ameletwa muda mchache ulio pita na sijui ninaweza kupata taarifa yake ya nyuma?”
“Wagonjwa walio letwa muda mcha ulio pita ni wengi labda wewe unamzungumzia yupi kati ya hawa?”
Daktari akawasha Tv yake kwa kutumi rimoti na nikaziona picha za Sheila akiwa ameshikwa na askari
“Huyo picha namba tano”
Nilimuonyesha
daktari kwa kutumi kidole na akaizima Tv yake na kunigeukia huku
akisaidiwa na kiti chake chenye uwezo wa kuzunguka
“Huyo hapa sisi tunamuita Vaiper Lady”
“Kwa nini?”
“Kwanza nimkali na ninamfananisha na hao nyoka ambao wanasifa ya kung’ata sana,Pili hatulitambui jina lake halisi ni nani”
“Sawa ila tatizo lake ni nini?”
“Huyu
binti amedhirika sana kiakili hii ni kutokana na mambo magumu ambayo
ameweza kupitia huku nyuma.Pia ubongo wake umetingishika kiasi kwamba
imemfanya akili zake kufyatuka”
“Akili yake imetingishika?”
“Ndio
ina maana aliweza kupigwa kwa kitu kizito kichwani ambacho kiliipelekea
akili yake kucheza kidogo na jambo kubwa la kumshukuru Mungu ni kwamba
mishipa ya damu haikuweza kupasuka kichwani mwake”
“Anaweza akapona?”
“Mmmm
sidhani kwa maana sisi tumejaribu kutumia ujuzi wetu mwingi ila
tumeshindwa ila kitu kibaya zaidi huwa hapendi kuona jinsia ya kiume na
alashawahi kufanya tukio la mauaji kwa….”
“Hili nilisha ambiwa……Sasa dokta imi ninahitaji kukaa naye kwa ukaribu sana ili niweze kumtuliza”
“Wewe kijana unahitaji kufa au…..kwa maana hataki kuona jinsia yoyote ya kiume”
“Mimi nitaweza dokta na Mungu akibariki kesho nitakuja kwa kazi hiyo”
“Mmmm kwa kweli si……”
Nikachomo noti mbili za dola mimi kwenye mfuko wa suruali na kumuwekea daktari mezani na akanyamaza
“Kaka utahitaji kiwango kingine zaidi ya hicho nitakupatia”
Daktaria
akanyamaza kimya na kushindwa kuzungumza kwa aibu na nikanyanyuka na
kumuacha akiwa ananishangaa.Hali ya furaha ikanitoweka kabisa na hata
ndani ya gari nikawa kimya huku nikimuwazia Sheila na sikusema kuwa
ninamfahamu Sheila hii ni kuepuka maswali mengi yasiyo na msingi
kwangu.Tukaingia kwenye moja ya duka la simu na kununua simu aina ya
Blackbery.Tukarudi kwenye jengo ambalo baba aliingia na kumkuta akiwa
anatusubiri.
“Mbona mumechelewa?”
“Ahaa kuna sehemu sehemu nilipitia”
“Hiyo simu umesha nunua?”
“Ndio baba”
“Sasa turudi nyumbai kwa maana lile swala nimesha likabidhi kwa wahusikana wameniahidi ndani ya siku mbili watanipa jibu”
“Kweli baba?”
“Ndio wewe kuwa na amani na kama utataka kuendelea kutazama tazama mji nipige simu nyumbani nije kuchukuliwa na gari nyingine?”
“Hapana kwanza nimechoka ninahitaji kupumzika kidogo alafu ninaomba namba yako baba”
“Sawa”
Baba
akanipatia namba yake ya simu na kutokana sikuwa na line ikamlazimu
kunipa laini yake moja ya simu ambayo haitumii sana.Tukarudi nyumbai
huku msongamano wa mawazo ukiwa umenitawala na moja kwa moja nikagundua
baba wa zamani mzee Godwin ndio chanzo cha Sheila kuwa katika hali kama
hii.Sikuweza kupata suingiza kabina na kila nilipo jaribu kuivuta amani
kutawala usoni mwangu nikajikutani kishindwa kabisa na sura yangu ikawa
imetawaliwa na mikunjo ya hasira.
Nikiwa
nemekaa kwenye moja ya masofa ya kupumzikia yaliyopo kwenye bustani
yenye maua mengo mazuri na kuna kijibwawa kidogo chenye maji masafi na
upepo mwingi nikamuoana mke wa baba akiwa na yule jamaa wa jana usiku
wakiwa kwenye moja ya kijijumba kilicho kwa vioo na ndani yake kukiwa na
maua mengi yanayo uteshwa kwa masaada wa mwanga wa jua.
Wakanza
kushikana shikana na mwisho wa siku wakanza kupeana mambo ya chumbani
bila kujali kama wanaweza wakaonekana na mtu.Nilicho kifanya ni kurekodi
tukio zima mwanzo hadi mwisho hadi wanamaliza na jamaa akawa wa kwanza
kutoka na baada ya dakika kama kumi mke wa baba naye akatoka huku
akijifanya kunusa nusa kipande cha ua alicho toka nacho na kwabahati
mbaya macho yetu yakakutana na akanipandisha na kunishu kiasi kwamba
akaanza kunikera
“Mama ninakuomba”
Akatembea kwa mwendo wa madaha huku mdomo wake akiwa ameubenua kiasi kwamba nikaanza kujiuliza sijui kipigo cha jana amekisaha
“Unasemaje?”
“Hivi baba yangu ni nani kwako?”
“Khaa wewe unamuona ni nani?”
“Jibu nililo kuuliza”
“Ni mume wangu”
“Una uhakika na unacho kizungumza?”
“Ndio kwa maana hata pete hii hapa ninayo”
“Unajua siku zote kwenye maisha usipende kumfanyia mwenzako kile usicho penda kufanyiwa”
“Una maana gani?”
“Utaijua wewe nenda zako”
Akaniandisha
kuanzi chini hadi kitendo ambacho maishani mwangu sipendi mwanamke
anifanyie akaachia msunyo mkali uliao nifanya ninyanyuke kwa haraka na
kumfwata kwa hasira na akaanza kukimbia ila kutonaka na uwezo wangu wa
kukimbia nikamdaka katika mlango wa kuingilia sebleni na kukutana na
baba akiwa anatoka ndani.
“Huyu mwanao ni mwenda wazimu nini?’
Sikumjibu
kitu cha aina yoyote zaidi ya kumfwata na nilipo sikia swala la uwenda
wazimu na mimi nikajichetua sana na ili nionekane ni mwenda wazimu
kweli.Tukaanza kazi ya kukimbizana huku tukimzunguka baba aliye kosa
kitu cha kuzungumza,
“Mume wangu mkamate mwanao atanijeruhi”
Na
mimi nikaanza kuuigilizia mlio wa Sheila alio kuwa akiningurumia na
kumfanua baba kuhamako na kadri muda unavyo kwenda ndivyo nikazidi
kujichetua kaisi kwamba baba akaagiza walinzi wake kunikamata na
wakashauriana wanipeleke hospitali ya vichaa kwa ajili ya vipimo
zaidia.Kwa bahati nzuri tukafika kwenye hospitali tuliyo toka masaa
machache yaliyo pita na kwabahati nzuri daktari aliye pewa jukumu la
kunipima na yule niliye mpa dola mia mbili na akawa ananishangaa kuniona
nikiwa nimeletwa kama mgonjwa.
“Dokta wakikuuliza waambie kuwa itanibidi hapa nikae kwa wiki mbili”
Nilimuambia daktari baada ya baba na watu wake kutoka nje ya chumba nilicho ingizwa
“Saaa….saaa”
“Dokta
acha kupata kigugumizi wewe waambie hivyo kuwa mimi ni mgojwa na
mutaniweka hapa kwa wiki mbili ili kunichunguza zaidi na kama ni pesa
mimi nitakulipa ila hili ni dili kati yangu mimi na wewe”
“Sawa nimekuelewa”
Daktari
akanipima pima kiuongo ili kupoteza muda kisha akatoka na baada ya muda
baba akaingia huku akiwa na sura ya unyongee na kwambali machozi
yanamlenga lenga
“Ohhooo Eeeehee baba ukuwaa mkubwaa kamaaaaa John Cennaaaaaa hahaaa…babaaa huuuyoooo katokaaaa kaziiiniiiiiiiii ohooaaooa”
Niliimba nyimbo za kuwehuka na kuzidi kumfanya baba aamini kuwa mimi nimepata kichaa
“Dokta kweli mwangu atapona?”
“Kama nilivyo kuambia hapo awali tunamuweka hapa ndani ya wiki mbili kisha tutaangalia jinsi maendeleo yake yanatavyo endelea”
“Ahahaa doktaaa wiki mbiliiiii hahajhhhaa mimi takaaa kaaaa mwakaa mzimaaaa baaaabaaa lia liaaa kama totojingaaaaaa hahaahaa”
Nikazidi
kuzungumza huku nikirusha rusha miguu na mikono na ikawalazimu watu wa
baba kunilaza kitandani na kunifunga mikono na miguu kwa kitumia mkanda
maalumu uliopo juu ya hichi kitanda nilicho lalia.
“Ohoo Mungu wangu sijui ni kitu gani kimempata mwanangu?”
“Usiwe na wasi wasi atapona tuu cha msingi ni kumuomba Mungu aweze kumjalia afya njema”
Baba
akanitazama kwa sura ya simanzi na akashindwa kuyazuia machozi yake na
akaanza kulia na ikamlazimu mlizi wake mmoja kutoa kitambaa na
kumkabidhi baba kisha akatoka naye nje na walinzi wake wengine wawili
wakafwatia nyuma.
“Dokra wachungulie wamesha ondoka?”
“Ngoja niangalie”
Dokta akafungua mlango na kuchungulia kisha akaufunga na kunifwata kitandani huku akiwa anacheka
“Ndio wamesha ondoka….hivi wewe kijana mbona msanii kiasi hichi?”
“Ahaaa
uanajua unapo amua kufanya kitu mtu inabidi uweze kufanya juu chini
unakifanikisha hata kwa staily kama hii pia ni vyema si umeona sasa
mpaka mzee ame….hahaaaa chipissssisisisisiiii oohoooo”
Nilirudi
katika hali yangu ya kuchanganyikiwa baada ya mlango kufungulia na
wakaingia majamaa wawili wenye misuli na wamevalia makoti meupe na
suruali nyeupe
“Huyo naye dokta ana tatizo gani?”
“Ahaa mchukueni mumpeleke kwenye chumba chake”
Jamaa
wakanifungua mikanda na kuninyanyua kwa nguvu na mmoja akanishika mkono
wa kulia na mwengine mkono wa kustoto,tukatoka nje ya chumba na kuwaona
baba na watu wake wakija kwenye ofisi ya daktari na ikanilazimu nianze
kuchetuka kama kawaida huku nikijirusha rusha juu na kuwafanya majama
hawa kutumia nguvu zaidi katika kunibana,Baba akawaomba wasimama kisha
akasimama mbele yangu na kunitazama kwa muda huku akijikaza kuto
kulia.Akanikumbatia na kuwaruhusu jamaa wanipekeleke wanapo nipeleka.
Nikaanza kupata woga kwa maana kila nilipo pita vichaa wakiume walianza kushangilia huku wengine wakiwa na sura za ajabu ajabu
“Sasa dokta naye tulimuuliza anatatizo gani huyu hajatujibu sasa tutampeleka kwenye wodi gani?”
“Kwa jinsi ninavyomuona tumuingize wodi namba nano itamfaa”
Jamaa
wakashauriana na kweli wakaniingiaza kwenye wodi yenye vitanda vingi na
vingi vinawatu ambao kwa muonekano wao ni vichaa walio pitiliza na
mbaya zaidi wengi wana miili mikubwa kupita maelezo kiasi kwamba kila
nilipo pita walinitazama kwa macho makali.Jamaa wakanionyesha kitanda
changu kisha wakatoka kwa haraka huku wakionekana kujishuku.Majamaa
matatu yakasimama kwenye vitanda vyoa na kuanza kupiga hatua za
kunifwata kitandani huku ikinguruma kama mimbwa inayo gombania mke
mmoja,mapigo ya moyo yakazidi kunidunda huku kijsho kikinimwagika kiasi
kwamba ubabe wangu wote ukaniishia.
Majaa
yakanitazama kwa muda huku yakinguruma na yakaanza kunishika shika
kichwa changu huku kila mmoja akitaka nimtazama yeye,Nikastukia kofi
moja takatifu likitua kwenye sikio langu na kusababisha uwezo wa kuona
vizuri ukakata na kuona vitu vyenye alama kama nyota nyota vikielea
angani kiasi kwamba nikajikuta nikiona giza lililo endana na ukungu.
Nikastukia
nikiwa nimelala chini sakafuni wala sikujua nimeshuswaje kwenye
kitanda.Makelele ya vichaa wengine yakazidi kunichanganya kiasi kwamba
nikawa sielewi nini cha kufanya.Kipigo kutoka kwa haya majamaa ambayo
yanaonekana ni mababe kwenye hii wodi kikanifanya nijikunyate huku
nikilia kwa uchungu.Nikaingia chini ya uvungu wa kitanda ili kujinusuru
kwani inadi ya vichaa wanao nishambulia ikaongezeka,Nikastukia nikivutwa
miguu yangu na wakaanza kuniburuza huku wakishangilia kwa nguvu.
Maumivu
makali yakazidi kuniumiza kiasi kwamba nikajuta kwa uamuzi nilio
uchukua.Wakanigongesha gongesha kwenye kwenye vitanda kisha wakanilaza
kwenye kordo iliyo tenganishwa na vitanda na wakanizunguka huku
wakinitaza na vijamaa viwili vyembaba vikapanda juu ya vitanda nawezao
wakaacha nafasi na sikujua wanataka kufanya nini,Nikastukia wa kwanza
akijirusha na kunifanya nimkwepe na akapiga kichwa kwenye sakafu na
kutulia tuli.Wa pili akafanya kama alivyo fanya mwenzake na akanitulia
kwenye tumbo na kunifanya nitoe ukulele mkali wa maumivu huku kicha
kizima kikiwa kimejaa manundu ya kipigo nilicho kipata.
Nikastukia
wakianza kunikojolea huku wakicheka kwa furaha na kupeana mikono na
kunifanya nizidi kulia kwa uchungu japo hasira imenipanda sikuwa na
uwezo wa kufanya chochote dhidi yao.Wakatawanyika na kuondoka kila mmoja
akarudi kawnye kitanda chake na wakaniacha nikiwa nimejilaza chini
pamoja na kale kajamaa lalicho nirukia.Nikaanza kujivuta taratibu hadi
kwenye kitanda changu huku mwili mzima ukiwa ninanuka mikojo pamoja na
kuvimba juu na nikakaa na baada ya muda mlango ukafunguliwa na wakaanza
kutoka mmoja baada ya mwengine.Akachugulia daktari mmoja na kutuona
ndani ya chumba tumebaki wawili na baada ya muda wakaingia madaktari
wanne ambao wawili wakanifwata mimi na wawili wakaenda kwa kale kalicho
zimia.
“Huyu ni mgeni eheee?”
“Naona”
“Ahaaa wageni huwa wanapata shida sana”
“Kweli kwa maana walivyo mfanya mmmm ni zaidi ya maumivu”
Madtari
wakaendelea kuzungumza huku wakinihudumia na kuniweka kwenye machela na
kunihamisha kwenye na kuniingia kwenye chumba cha matibabu.
Ndani
ya siku nne nikawa nimepona vuzuri japo sio sana kwani kuna baadhi ya
sehemu zinamaumivu kidogo.Nikarudishwa kwenye wodi ambayo nilitembezewa
kichapo na nikaanza kazi yangu rasmi ya kumtafuta Sheila kwenye kila
sehemu ya hospitali hii,Ndani ya siku mbili sikuweza kumuona Sheila na
sikujua ni wapi alipo,Nikaanza kuzoeana na vichaa kadhaa ambao ni
wanyonge kama mimi kwa maana jinsi watu wanavyo ishi kibabe kwenye hii
hopitali inasababisha kuwemo na mgawanyiko wa vichaa wababe na vichaa
wanyonge.Wakati wa kuoga ukawadia na kama kawaidi kila wodi ina mabafu
yake ambayo muda wa kuoga unapo wadia ni wote tunatakiwa kufanya hivyo.
Nikatafuta
sehemu isiyo na mminyano na kusimama na kuwatazama jinsi vichaa wengine
wanavyo minyana kwenye kuoga.Wakaoga wote kisha wakatoka na mimi
nikanza kuvua nguo zangu na kabla sijamaliza kuzivua akaingia lile
jijamaa ambalo lilinizaba makofi pamoja na wezake na baada ya kuniona
likaanza kunguruma na kuanza kunifwata na nikajiandaa kwa chochote
atakacho hitaji kukifanya kwangu mimi.Likanisimamia mbele yangu huku
likinitazama kisha likanitisha kama ninataka kunipiga kofi na kujikuta
nikiinama huku mikono yangu nikiwa nimeiweka kichwani kuziba uso wangu
na nikastukia likaanza kucheka sana hadi likakaa chini kwa kucheka na
ikanibidi na mimi kuanza kucheka
Hata
hamu ya kuoga ikaondoka na kujikuta nikivaa nguo zangu na kutoka
bafuni.Kama kawaida muda wa michezo ukawadia na kila kichaa anaye penda
mchezo wake anakwenda kwenye eneo lenye kiwanja cha mchezo wake.Nikaanza
kuzunguka zunguka nikaangalia jinsi vichaa wanavyo fanya mambo ya ajabu
kusema kweli inahitaji moyo wa uvumilivu kuishi nao kwa maana kama
akili yako ni nzima basi ukishindwa kuvumilia unaweza ukawaambia
madaktari kuwa umepona.Nikakuta wasichana watatu vichaa wakiwa wamekaa
chini wakichora chora na katika kuwachunguza vizuri nikamuona Sheila
akiwa katikati yao
Na
mimi nikajisogeza karibu yao na kukaa huku nikimtazama Sgeila jinsi
anavyo chora chora cini kwa kkutumia kijiti huku akifuta futa.Wezake
wakasimama na kuondoka zao na akabaki peke yake.Sheila hakuinyanyua sura
yake kunitazama na akazidi kuchora chini huku akikigandamiza sana
kijiti chini na akiwa anaonekana kama anahasira kali.Machozi yakaanza
kumwagika kiasi kwamba akafuta alicho kichora kicha akaanza kuandika
herufi moja moja kwa uchungu{I…….L…..O…….V…….E}
Nikabaki
nikimuangalia huku kwa mbali na mimi machozi yakinilenga lenga kwani
afya yake imedhohifika sana isitoshe mwili wake umetawaliwa na makovu
mengi sana ambayo yamemfanya azidi kuonekana mbaya.Akayafuta maandishi
yake kisha akachora vikatuni viwili kimoja kikiwa cha kike huku kingine
kikiwa cha kiume na akavipatia majina kwa herufi za mwazo ambacho
kikatuni cha kike akakiandikia herufi kubwa ya ‘E’ huku cha kike
akikiandikia kiherufi cha ‘S’.Hapo ndio nikashindwa kuzizuia hisia zangu
na kujikuta nikimwagikwa na machozi na kumuona Sheila akiinyanyua sura
yake tartibu na kuniangalia kwa muda kisha akairudisha sura yake chini
na akanitazama tena kwa umakini huku akiwa kama mtu anaye jitahidi
kuvuta kumbukumbu ya kitu fulani ila anashindwa kujua ni nini anacho
kiwazia
“Sheila…..Sheila?”
Akaonekana
kustustuka na akanikazima macho hadi akaanza kuniogopesha akajaribu
kuzungumza ila akawa kama anashindwa.Aafuta vidoli vyake chini na
kuandika maandishi yaliyo nistua zaidi.
{MIMI SIWEZI KUZUNGUMZA NIPO SAWA SAWA NA BUBU}
Maumivu
makali yakapenya kwenye moyo wangu na kujikuta sura nzima ikitawaliwa
machozi.Nikachukua kijiti chake na kumuandikia chini
{KWANINI HUWEZI KUONGEA?}
Sheila akanitazama kwa macho ya mshangao kwa jinsi ninavyo lia kisha akaniandikia chini
{SIWEZI TUU KWANI NILILISHWA MAKAA YA MAWE KWENYE MDOMO WANGU}
Sheila
akaufungua mdomo wake na kuutoa ulimi wake nje na nikajikuta
nikitetemekwa kwa woga kwani ulimi wake una majeraha makubwa yanayo
onyesha vika ni kweli alilishwa makaa ya moto.Sheila akasimama gafla na
ni mimi nikasimama na akaanza kutembea na kujikuta nikizidi kuumia kwani
hata shepu lake la nyuma lilidhohofika sana.Tukaongozana hadi kwenye
moja ukumbi ambao kuna kiwanja cha mpira wa kikapu(basketball) na
akazidi kunipeleka hadi kwenye moja ya mabafu na akanitazama na kulivua
gauni lake
Nikajikuta
hata uwezo wa kuhema ukianza kuwa mdogo kutokana na mstuko nilio upata
baada ya kuuna mwili wa Sheila ulivyo jaa majeraha makubwa ya kachanwa
chwana na kutu chenye ncha kali.Akanigeukia mgongoni na kunionyesha kuvu
kubwa la kutobolewa huku ngozi ya sehemu hiyo ikiwa imekunjamana na
kujikuta nikizidi kuteswa na uchungu,Macho ya Sheila yakaanza kuvunjwa
na machozi na akatazama tazama ndani ya bafu hili na sikujua anatafuta
nini.Akafungua koki ya bomba la maji kisha akachovya kidole chake kimoja
ndani ya maji na kuandika kwenye kiio kikubwa kilichopo ukutani.
{MIMI
SIO KICHAA ILA WATU WANANIISI KUWA MIMI NI KICHAA ILA UKWELI NI KWAMBA
NINAAKILI ZANGU VIZURI NA HAYA YOTE YAMETOKANA NA MAUMIVU MAKALI NILIYO
PEWA NA MZEE MMOJA AMBAYE NI MKUU WA JESHI NA NIBABA WA MPENZI WANGU
EDDY}
Sheila
akanigeukia na kuniuliza kwa ishara kama nimeelewa alicho kiandika na
mimi nikatingisha kichwa nikimuashiria kuwa nimeelewa
“Unanikumbuka?”
Nilimuuliza Sheila na akabaki akinitazama kwa muda kisha akachovya kidole chake kwenye maji na kuandika kwenye kioo
{HAPANA ILA NINAKUFANANISHA NA EDDY WANGU ILA SIO WEWE KWANI YEYE ANAAKILI ZAKE TIMAMU NA SIO CHIZI KAMA ULIVYO WEWE}
Nikatulia
kwa muda huku nikiyatafakari maneno ya Sheila aliyo toka kuniandikia
muda mchache ulio pita.Nikamsogelea Sheila na kumkumbatia huku nikiwa
ninamwagikwa na machozi.Mlango ukafunguliwa na wakaingia madaktari
wawili wa kiume na walivyo tuona tumekumatiana wakanitoa mimi kwa nguvu
na kuchomoa virungu vyao na kuanza kunipiga huku wakiniburuza na kunitoa
nje
“Sheila….nisaidie ninakufa mimi”
Nilizungumza
kwa sauti ya juu huku nikiwa ninalia kwa uchungu na kuzidi kuwaongezea
hasira madaktari hawa na kuzidi kunipiga,Sheila kwa haraka akatoka huku
akiwa na nguo ya ndani na akamsukuma dokta mmoja ana akajibamiza kichwa
ukutani na akaanguka chini kisha akamshika kichwa cha gaktari na kunaza
kukibamiza kwenye sakafu kwa nguvu hadi kipasukwa kwenye kisogo
chake,Daktari aliye kuwa anaendelea kunipiga baada ya kumuona mwenzake
akiwa anaaga dunia akaniacha na kwa nguvu zake zote akarusha kirungu
chake na kikatua kichwani mwa Sheila na akadondoka chini na damu za
puani zikaanza kumwagika
ITAENDELEA...
RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 33 & 34 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )
Reviewed by WANGOFIRA
on
21:27:00
Rating:
No comments: