Kikwete: Nashukuru Mungu Kwa Kuutua Mzigo Salama Huku Nikiiacha Nchi Ikiwa Salama Tulii Kabisa

Na David John Pwani
MWENYEKITI Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt.Jakaya Kikwete amesema anashukuru Mungu Kwa kuutua mzigo salama huku akiicha nchi ikiwa salama tulii kabisa.

Amesema kuwa safari yake ya urais ilianzia Bagamoyo akitokea wilayani hapo ambapo baada ya hapo alikwenda Kibaha kutangaza nia ya kugombea urasi nakudai kuwa amejisikia furaha kurudi tena Bagamoyo akiwa salama.

Amesema wakati akielekea kutangaza nia ya kugombea urais alikuwa na mtoto wake Ridhiwani Kikwete ambapo yeye alikuwa anaandika na Ridhiwani anachapa kwenye Komputa.

Dkt.Kikwete aliyasema hayo jana wilayani Bagamoyo katika hafla ya kumkaribisha Nyumbani baada ya kuitumikia nchi Kwa miaka mingi, ambapo iliandaliwa na Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani.

Alisema anashukuru Kwa Mara nyingine kurudi mahala alipoanzia na kwamba amemaliza salama na ameacha nchi ikiwa salama na imetulia tulii kama Maji kwenye mtungi.

Akikumbuka mchakato wa mwaka jana wa kumpata Mgombea ulikuwa na mambo mengi lakini mambo yalikwenda salama na hakuna lililokuwa limeharibika .

"Ilikuwa Kazi kubwa si ndogo lakini hatimaye wa kavuka na wakaingia kwenye uchaguzi ambao ulikuwa na vurumai" alisema Dkt.Kikwete .

Aidha alisema kuwa hata hivyo katika uchaguzi huo kulikuwa hakuna mtu ambaye alipatwa na tukio la kumpiga mwezake hali ambayo iliwashangaza hata nchi jirani.

Alisema kuwa katika kipindi chake cha uongozi amefanya kazi kubwa ya kusukuma maendeleo ya wananchi Kwa mikoa yote,wilaya zote bila ubaguzi wowote ule huku akikiri kukabiliana na Changamoto ya kunyoshewa vidole hususani pale alipojaribu kupeleka maendeleo Wilayani Bagamoyo kanakamba wananchi wa Bagamoyo walikuwa hawana haki.

Aidha Dkt.Kikwete alisema kuna wakati alisimamisha fedha za ujenzi wa barabara hiyo na kupeleka fedha hizo kujenga barabara ya Geita, Sengerema,usagala ,na kulizuka na Maneno mengi dhidi yake na hadi kufikia wabunge kulumbana.

Alisema hata hivyo anashukuru kwamba amemaliza salama na Kwa bahati nzuri amepatikana rais ambaye ana ari kubwa ya kuwaletea maendelea watu huku akitaka watanzania kumuunga mkono.


Kikwete: Nashukuru Mungu Kwa Kuutua Mzigo Salama Huku Nikiiacha Nchi Ikiwa Salama Tulii Kabisa Kikwete: Nashukuru Mungu Kwa Kuutua Mzigo Salama Huku Nikiiacha Nchi Ikiwa Salama Tulii Kabisa Reviewed by WANGOFIRA on 08:33:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.