Gonzalo anunuliwa kwa pauni milioni 75
Juventus wamemnunua mshambuliaji wa Agentina Gonzalo Higuain kutoka Timu ya Napoli kwa pauni milioni 75.5
Mchezaji
huyo mwenye miaka 28 amesaini mkataba wa miaka mitano baada ya Juventus
kukubali kutoa kitita hicho kinachokaribia Euro milioni 90 ambazo
watazilipa kwa awamu.
Malipo hayo ya Mzaliwa wa Ufaransa Higuain
aliyeanzia uchezaji wake wa kulipwa katika timu ya River Plate ya
Argentina yanachukua nafasi ya tatu kwa ukubwa baada ya yale yaliyolipwa
na Real Madrid walipomnunua Cristiano Ronaldo kwa Pauni milioni 80 na
Gareth Bale kwa Pauni milioni 85.
Gonzalo anunuliwa kwa pauni milioni 75
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:20:00
Rating:
No comments: