RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 23 & 24 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


Mtunzi:EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA
 Mkuu wa shule na akasimama eneo tulilo jificha na Madam Rukia huku kila mmoja akiwa nguo zake amezivaa vizuri baada ya kuwasikia walimu hawa mambao walinitoroka mchana wakizungumza.Mkuu wa shule akaanza kukojoa huku akipiga mluzi akiisikilizia raha ya kukojoa na mkono wake mmoja ameshika bastola yake na gafla Madam Rukia akakohoa na kumfanya mkuu wa shule kugeuka na macho yake na yangu yakakutana huku akionekana kuto amini kuniona katika eneo hili

ENDELEA
Akili yangu ilafanya kazi ya haraka ya kufikiri na wazo lililo nijia ni kumshika Madam Rukia na kumsukuma na akaangukia kwenye miguu ya mkuu wa shule na mimi nikanyanyuka kwa haraka na kuanza kutokomea porini.Milio ya bunduki nikaanza kuisikia kwa nyuma nikajua atakuwa ni mkuu wa shule pamoja na waalimu wengine ambao wanamuunga mkono mkuu wa shule.
Nikafanikiwa kuwaacha kwa umbali mkubwa na kutokana na kuchoka sana ikanilazimu nipande juu ya mti ili niweze kujipunzisha kwani tofauti na hapo ninaweza kupata maumivu makali ya kifua yatokayono na jeraha la risasi nililo kuwa nimepigwa na Manka
 
Nikajilaz akwenye tawi huku nikiangalia chini na kuumshuhudia mwalimu wa nizamu akipita kwa kasi akielekea nilipokuwa nikielekea.Ndani ya dakika moja wakapita waalimu wengine wawili wakiwa katika mwendo wa kukimbia.Nikaanza kusikia sauti ya Madam Rukia akilia na nikamshugudia mkuu wa shule akiwa amezishika nywele za Madam Rukia huku akimvuta kwa nguvu akimlazimisha atembee kwa haraka
 
Mkuu wa shule na Madam Rukia wakasimama chini ya mti niliopo huku Madam Rukia akilalamika amechoka
“Nitakuua tambua mimi sasa hivi sio mwalimu wako mkuu.Ohooo wewe niletee ufala”
Mkuu wa shule alizungumza huku bastola yeke akiwa amaiweka kwenye sikio la Madam Rukia la upande wa kushoto.
 
“Sema huyu fala mwenzako amekwenda wapi?”
“Mimi sijui kwani si alikimbia mbele ya macho yetu”
“Ahaaa hujui eheee?”
“SIJUI MKUU WEWE UNANIONEA TUU”
Mkuu wa shule akavuta kashati ka Madam Rukia na kakachanika na akabaki na sidiria kisha akaanza kumshika shika maziwa kinguvu kiasi kwamba Madam Rukia akaanza kufanya fujo ya kujitoa mikononi mwa mkuu wa shule
“Nitakupasua hichi kichwa”
“Nipasue ila sio kuniambukiza ukimwi wako”
“Ahaaa sasa nakuambukiaza”
 
Mkuu wa shule akaendelea kuzichana nguo za Madam Rukia kwa kutumia nguvu galfa nikastuka kuiona simu yangu ikienda chini huku ikitoa mwanga na inavyoonyesha inaita na sikujua ni kivipi imetoka mfukoni mwangu na kwabahati mbaya ikaanguka katikati ya Mkuu wa Shule na Madam Rukia.Mkuu wa shule akaiokota simu yangu na kuangalia juu haraka na kuniona.Madam Rukia akampiga mkuu wa shule kigoti cha sehemu za siri na kumfanya atoe ukulele huku akiiangusha simu aliyo ishika.Nikashuka kwenye mti kwa haraka na kumkuta bado mkuu wa shule amejikunja.
 
Madam Rukia akaiokota simu yangu na mimi nikampiga teke mkuu wa shule lililo tua kwenye kifua chake na kumfanya angukie mgongo kabla sijamsogelea nikwaona waalimu wakirudi katika eneo alilopo mkuu wa shule.Nikamshika mkono Madam Rukia na kuanza kukimbia naye kurudi tulipo liacha gari
“Eddy nimechoka?”
“Jikaze bwana”
“Niache wewe ndenda”
“NINI?”
“Eddy wewe nenda zako mimi niache hapa hapa nitajua cha kufanya”
Nikawaona waalimu wakiwa na mwalimu mkuu wakishuka kwa kasi kwenye kilima wakija katika eneo tulipo
 
“Eddy wewe nenda na chukua na simu yako”
Mada Rukia alizungumza huku akiwa analia kwa uchungu,Nikaichukua simu nikamuachia mkono taratibu na kuanza kukumbia kwa kasi huku nikianza kuvuta kumbukumbu ni wapi nilipo liacha gari kwani miti mingi iliweza kunichanganya kiasi kwamba nikawa ninazunguka zunguka pasipo kujua ni wapi lilipo gari.Gafla nikasikia mlio wa bunduki na kunifanya nisimame gafla na akili yangu moja kwa moja ikamkumbuka Mada Rukia
“Fuc*k wamemuua”
 
Nilizungumza huku nikitazama sehemu ulipo tokea mlio wa bunduki,nikataka kurud ila nikasita na kujikuta nikishikwa na bumbuazi.Mwanga wa simu yangu ukanistua na kuigeuza na kukuta namba ngeni ikiingia kwenye simu yangu.Nikaipokea na kujibanza kwenye mti huku nikiwa ninahema kiasi kwamba hata mtu aliye nipigia simu atahisi kitu
 
“Vipi kijana?’
“Salama nani mwenzangu”
“Mimi ni daktari wa hospiytali uliyo mleta binti wa kike na ukaniachia namba nikujulishe kitakacho endelea”
“Ndiio nimekukumbuka dokta”
“Hali ya Salome sio nzuri nainatubidi yumsafirishe tumpeleke Dar es Salaam kwa matibabu zaidi”
“Kwani tatizo lake lilikuwa ni kubwa sana”
“Ndio mishipa ya damu inayoingiza damu kwenye moyo wake imepasuka”
“MUNGU WANGUUUU”
“Na hapa inabidi sisi kama Hospitali kushuhulika katika garama zote kwa wakati huu ila wewe utakuja kuzilipa”
“Saaaw........Haaaa!!!”
 
Nikastukia gongo likipiga sehemu ya juu kwenye mti na nikageuka haraka na kumshuhudia mwalimu wa nidhamu ambaye siku zote huwa sipatani naye akija kwa kasi huku akiwa peke yake,Nikaiweka simu yangu mfukoni na kuipandisha juu kidogo suruali yangu ya jeanzi na kumsubiria kwa hamu mwalimu.
Nikastukia mwalimu wa zamu akinipita kwa kasi kama hajaniona na sekunde kadhaa nikaona kundi la vijana wapatao kumi wakija kwa kasi huku wengine wakiwa na mapanga na magongo,
Na mimi nikaungana na mwalimu wa zamu katika kukimbia katika njia anayo elekea huku vijana hao wakionyesha ni wachaga wakitufwata kwa kasi,Tukagawana njia mimi na mwalimu wa zamu kila mmoja akaenda upande anapo pajua yeye huku nyuma yangu wakiwepo vijana wawili wakinifwata mimi
 
“Mungu wangu nisaidie”
Nilijiesemea kimoyo moyo huku nikijikaza katika kukimbia kiasi kwamba niliaza kuhisi kuchoka huku kifua kikiniuma kwa mbali.Nikakaza mwendao huku nikiwatazama vijana wanao nifwata nikaona wakikata tama ya kunikimbiza na mwisho wa siku wakasimama na kuanza kutukana kilugha na wakarudi walipo tokea.
Nikasimama na huku nikiinama na pumzi nikizihisi zikiniishia pamoja na koo langu kukauka mate.Mazingira ya eneo nililopo yakanipa matumaini kwani ndio sehemu ambayo tulifanyia mapenzi na Madam Rukia,Nikajikaza na kunyanyuka na kwenda lilipo gari na kukuta tairi moja ya mbele ikiwa haina upepo.Nikafungua buti la gari na nakuta batani ikinielekeza niminye nikaminya na ndani ya buti kukafunguka na kukuta tairii  pamoja na vidungu viwili vya lita mbili mbili vya mafuta ya petrol na vinaonekana ni maalumu kwa gari hili kwani bado vina upya
Nikalitoa taira na kuliweka chini huku nikiwa na mashaka na kila muda nikawa na kazi ya kuangalia pande zote za sehemu niliyopo.
Simu yangu ikatoa mwanga ulionekana kwenye mwanga wa jeanzi yangu ikiashiria simu inaita nikaitoa mfukoni na kukuta ni Sheila ndio anapiga nikaipokea na kuibana sikioni kwa kutumia bega
“Baby mbona nilikuwa ninakupigia hupokei?”
“Baby weee acha tu hapa nilipo nipo kwenye matatizo”
“Matatizo gani mume wangu?”
“Wee acha tu nitakusimulia”
 
“Saa zile nilitaka nikuambie kuwa utazame kuna mafuta ya emergence kwenye buti na sikujua kama ulielewa?”
“Sikuelewa ila sasa hivi ndio ninayaona”
“Fanya basi urudi dady”
“Sawa”
“I love you”
“Love you too”
Nikakata simu na kuirudisha simu ndani ya gari kisha nikaanza kazi ya kufungua tairi lililo na pancha na kulifunga tairi lililo jipya na ikanichukua kama dakika ishirini katika kuikamilisha kazi yangu.
Nikayamimina mafuta kweye tanki la gari kisha nikaingia na kuliwasha na nikazifwata taratibu za uwashaji wa gari hili kisha nikaanza kuomdoka huku nikirudi katika barabara ya niliyo jia.Kutokana ni msituni mingi sikuweza kukimbiza gari kwani ninahofia kuchanganya njia,Gafla nikaona taa za gari zikija mbeke yangu kwa kasi huku zikiwasha king’ora nikatambua watakuwa ni gari la polisi.
 
Dereva wa gari la polisi akaanza kuliendesa gari lake kwa fujo ya kutanda barabara nzima huku taa zake akiziwasha kwa mtindo wa zima washa kitu kilicho niumiza macho.Nikapungunza mwendo na kadri nilivyojaribu kuwakwepa kwa kubana upande mmoja wa barabara ila dereva wa gari ya polisi akanifwata upande niliopo
“Huyu jamaa ni chizi nini?”
 
Nilijiuliza kwa sauti ya juu huku gari langu nikilirudisha barabarani ili niweze kuona atanifanya nini.Na yeye akalirudisha barabarani gari lake huku akiziwasha taa zake kwa mtindo ulionikera huku akipunguza mwendo na gari zetu zikabaki zimetazamana huku dereva huyo akivuta akikanyaga mafuta kama wafanyavo madereva wa mashindano ya magari kabla hawajaruhusiwa kuanza kasi.
Nikastuka baada ya kuwaona watu wawili wenye miili mikubwa wakiwa wamevalia makoti meusi na makofia yaliyo yaficha sura zao na kubaki macho wa kishuka kwenye gari ya polisi huku wakiwa na bubduki mikononi wakizielekezea kwangu.Nikairudisha gari nyuma kwa kasi ya ajabu na kuwafanya jamaa kuanza kunishambuli kwa risasi.
‘HALO BWANA EDDY GODWIN GARI YAKO IMEPATA ULINZI BINAFSI’
Sauti ya kike ilisikika kupitia spika zilizopo kwenye gari ambalo kwangu kila kinacho fanyika ninaona ni kipya na sauti hii si ngeni kwangu
 
‘CHAGUA SILAHA’
Kioo kidogo kilianza kunionyesha aina za bunduki zilizopo ndani ya gari kwa kigugumizi nikajikuta nikijiminyia kwenye silaha ambayo wala sikujua itajitokeza wapi,Gafla gari yangu ikasimama na haikurudi nyuma na nikaanza kusikia mtetemeko ndani ya gari na kuona vitu vyenye moto na vinavyokwenda kwa kasi kali vikitoka sehemu ya mbele ya gari na vikielekea lilipo gari la polisi na kulifanya lirushwe juu na kulipuka huku jamaa wanao nirushia risasi wakianguka chini
“UPO SALAMA BWANA EDDY GODWIN UNAWEZA KUENDELEA NA SAFARI YAKO.ASANTE”
 
Gari ikarudi katika hali yake ya kawaida na taratibu nikaanza kukanyaga mafuta na kufika katika sehemu ambayo wameangukia watu ambao sikujua lengo lao ni nini hadi wanisambule kwa risasi.
Nikawachungulia kupitia kwenye kioo nikagundua wamefariki kwani miili yao ilijaa matobo mengi yaliyo tokana vichuma vya bomu zilizo toka kwenye gari huku damu nyingi zikivuja kwenye miili yao,Nikashuka huku nikitetemeka na kuanza kumfunua mmoja baada ya mwengine na kujikuta kumbukumbu zangu zikirudi hadi siku niliyo kamatwa pamoja na derava wetu na kuingizwa katika maabusu ya kituo cha polisi Lushoto na kulikuwa na majaamaa yenye misuli mikubwa na katika mazungumzo yetu walisema wao ni majambazi sugu wanashuhulika na utekaji wa magari.
Sura mbili za majamaa wale ndizo zilizo lala chini,Sikutaka ushahidi nikaingia haraka ndani ya gari na kuondoka katika eneo hili.Baada ya lisaa nikawa nimefika mjini na muda ulio timu sasa ni saa kumi na nusu usiku.
Nikafika hospitalini na kulisimamisha gari katika maengesho ya magari nikatoa simu yangu mfukoni na kuakuta missed call nyingi za Sheila.Nikafumba macho yangu na kusali kwa kumshukuru Mungu kunisaidia kutoka katika majanga yaliyo nikuta ila nafsi na moyo wangu vikajikuta vikiniuma kutokana na kifo cha madam Rukia
Nikashuka ndani ya gari na kwenda moja kwa moja katika chuma alicholazwa Sheila ila sikumkuta na nikatoa simu na kumpigia akapokea nesi
 
“Mgonjwa wangu yupo wapi?”
“Tumemuhamisha chumba panda huku gorofani ukunje kushoto chumba namba 16 ndipo alipo mgonjwa wako”
“Sawa”
Nikafanya kama alivyonielekeza nesi na kuingia katika chumba namba 16 na kumkuta Sheila akiwa hana raha na baada ya kuniona akataka kushuka kitandani kuja kunikumbatia ila sindano ya dripu ilimzuia,Nikamfwata na kumkumbatia na sote tukajikuta tukitokwa na machozi ya furaha
 
“Mume wangu pole”
“Asante mke wangu”
“Mimi kidogo hali yangu inaendele vizuri zile sindano walizo nichoma kidogo kidonda kimeanza kukauka kwa haraka”
“Nijambo la kumshukuru Mungu”
Nikaanza kumuadisia Sheila yaliyo nikuta ila sikumuadisia juu ya Madam Rukia kwani ninajua nilicho kitenda hakikustahili kwa mimi kumfanyia
“Sasa huyo uliye mgonga anaendeleaje?”
“Sijajua ila asubuhi itanibidi nikamfwatilie niweze kujua ni nani?”
 
“Utampatia wapi?”
“Nitauliza uliza na itanibidi niweze kuwa na pesa ya kumsaidia kama nitamuona na hapa sina hata pesa?”
“Kwani ni kiasi gani cha pesa kitatosha?”
“Sijajua ila niwe na pesa ya kutosha”
“Basi nitakupa kadi ya benki ukachukue pesa ya kutosha”
“Sawa mke wangu”
Tukaendelea kuzungumza mazungumzo ya kawaida hadi asubuhi nichukua kadi moja ya Sheila na akaniambia namba zake za siri kisha nikaondoka.Sikutaka nitumie gari kuhofia watu wa eneo nililo gonga mtu jana kuweza kulijua.Nikatembea kwa miguu hadi benki na nikabaki ninashangaa baada ya kukuta salio la akaunti ya Sheila milioni miambili na themanini 280.00.
 
“Huyu mwanamke kumbe anapesa kiasi hichi?”
Nikachagua huduma ya kutoa pesa nikaanza kutoa kiasi kidogo dogo hadi ikatimu milioni moja na nusu.Nikaingia kwenye duka kubwa la nguo na kununua nguo nyingine mpya pamoja na viatu.Nikanunua begi la mgongoni na kuziweka nguo nilizo zivua pamoja na viatu kisha nikatoka nje na kuingia kwenye kihoteli kidogo nikaagizia chakula kifungua kinya na kuanza kuka taratibu huku kichwa changu kikisongwa na mawazo.Nikamaliza na kutoka kwenye mgahawa huo na moja kwa moja nikaeleka kwenye vituo vya kukodisha taksi nikaingia kwenye taksi moja na kumuomba dereva anifikishe kweye hosptali ya mkoa.Tukafika na nikamuomba derava taksi anisubiri
 
“Lakini kaka itabidi pesa iongezeke”
“Haina shinda”
“Niachie japo advance ili nipate moyo wa kukusubiria”
Nikatoa elfu ishirini na kumpa kisha nikaelekea kweye ofisi ya daktari wajana na kukuta foleni kubwa ya watu wakiwa wanasubiri kuingia ndani ya ofisi hiyo.Nikawasalimia wakaitikia baadhi huku wengine wakionekana wapo kwenye maumivu makali ya magonjwa yao
“Samahani dada akitoka huyo mtu humo ndani unaweza ukanifanyia msaada niingie nikaonane na daktari mara moja?”
 
“Mmm kaka yangu ni bora uakapanga foleni tuu kwani mimi nimekuja tangu saa kumi na mbili asubuhi na foleni ilikuwa kubwa kama nini?”
“Dada mimi sio kama ninaumwa ila ninaingia mara moja kumuona huyo daktari tuu”
“Nimesema panga foleni mbona wewe kaka sio muelewa”
Watu waliopo nyuma ya dada wakaanza kulalamila wengine wakitaka niingie wengine wakikataa nisipishwe na dada huyo.
“Jamani samaani kama nitakuwa nimewaudhi kwa ombi langu”
“Ndio umetuudhi wewe utoke zako huko nyuma ulete kwato zako huku mbele,Unadhani na nina atakubaliana na ujinga kama huo kama vipi wewe ondoka”
 
Jamaa mmoja alizungumza kwa hasira kiasi kwamba watu wa karibu yake wakaanza kumtuliza hasira.Nikamuangalia kwa macho ya hasira kisha nikapiga hatua na kuufungua mlango wa daktari na kuingia bila dokta na kuwaacha watu wakilalamika.Daktari alipo niona akastuka na akanitazama kwa mshangao
“Mgonjwa wangu yupo wapi?”
“Kijana huo sio utaratibu wa kazi kama uliwakuta wezako kwenye foleni inabidi ukae kwenye foleni”
“Dokta hilo sio jibu nataka nijui mgojwa wangu yupo wapi?”
“Nakuomba uwe mpole kijana.Mgonjwa wako yu....yuu”
“Yuuu yuuu nini sema yupo wapi.....?”
Kwa haraka haraka nikaanza kuhisi kuna kitu ambacho daktari ananificha kwani kwa jinsi anavyo zungumza ananipa wasiwasi
 
“Yupo kwenye wodi ya wazazi”
“Twende ukanionyeshe”
Daktari akajishauri kisha akamuomba mgojwa wake niliye mkuta amsubiri anarudi ndani ya muda mchache.Tukatoka nje na kuwafanya wagonjwa wanao lalamika kukaa kimya huku wakitutumbulia mimacho ya mshangao.Tukaelekea kwenye moja ya wodi na kumkuta Madam Mery akiwa amelala kwenye moja ya kitanda huku pembeni yake akiwepo jamaa ambaye nilimuona kwenye picha za harusi yao kwa na moja kwa moja nikajua ndio mume wake.Madam Mery baada ya kuniona akastuka huku kwa ishara akiniomba nisisogee kwenye kitanda chake.
 
“Mgojwa wako yule pale”
Dokta aliniambia baada ya kuniona nimesimama
“Pesa iliyo baki ni kiasi gani?”
“Imeshalipwa na yule jamaa pale kwenye kitanda”
“Powa nakushukuru dokta”
“Na wewe pia nakushukuru”
Dokta akaondoka na kuniacha nikiwa nimesimama huku macho yangu yakimtazama Madam Mery hadi jamaa yake anakaanza kuhisi kitu.Jamaa akapiga hatua za kunifwa na kabla hajanifikia nikageuka na kuondoka kwa hataua za haraka na kutoka katika wodi na kumfanya jamaa kuongeza mwendo na kuja kunishika bega
 
“Kaka vipi?”
Jamaa alinisalimia huku akinitazama machoni
“Salama tuu vipi?”
“Mbona umemtazama mke wnagu na ukaondoka baada ya mimi kukutazama?”
“Kwani tatizo lako ni nini?”
“Nahitaji kujua kama wewe unamjua mke wangu au humjui?”
“Simjui”
“Sasa kwanini umtazame?”
“Wee jamaa vipi kumtizima mke wanko ni kosa?”
“Ndio ni kosa sipendi mke wangu atazamwe...Na ukirudia kumtazama nitakutoa duniani”
 
Jamaa alizungumza huku akilifunua koti la suti yake na kunionyesha bastola aliyo ichomeka kiunoni mwake.Sikutaka ugomvi naye nikageuka na kuanza kupiga hatua za kuondoka kabla sijafika mbali na sehemu niliyo kuwa nimesimama nikastukia nikivutwa tisheti na nikageuka na kumkuta mume wa Madam Mery akinitazama kwa hasira
“Mimi ninakusemesha alafu wewe unaondoaka ina maana umenidharau si ndio?”
 
Jamaa alizungumza kwa hasira na sauti ya juu na macho yangu nikayapeleka hadi kwenye kioo cha TV(Luninga) iliyopo eneo la mapumzikio ya wagonjwa na kuitazama taarifa ya habari inayorusha na shirika la utangazaji nchini Uingereza shirila la BBC inayozungumzia kupotea kwa ndege ya shirika la KLM iliyokuwa ikitokea nchini Tanzania na inavyosemekana ina viongozi wa juu wa serikali wa nchi ya Tanzania na moja kwa moja nikatambau mama yangu ni miongoni mwa viongozi hao na mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio
 
Gafla nikastukia kibao kikali kikitua shavuni mwangu kikitokea kwa jaamaa na kunifanya niyumbe na kumgonga nesi mmoja anaye saidiana na mwenzake katika kusukukuma kitanda cha matairi na juu yake kuna mgonjwa ambaye sikuamini macho yangu kwani ni Manka ndiye aliyelazwa juu ya kitanda hicho kuku sura yake ikajaa michubuko na amewekewa kifaa maalumu cha kuhemea huku macho yake akiwa ameyafumba na hali yake inaonekana sio nzuri

               *****SORY MADAM*****(24)

“Kaka kuwa makini?”
Nesi alizungumza huku akijiweka vizuri na nikabaki nimeduwaa huku nikiwaangalia wanavyokisukuma kitanda wakielekea kwenye moja ya chumba ambacho kina maandishi mekundu makubwa juu ya malango ambayo yameandikwa ICU huku chini kukiwa  na maandishi yaliyo andikwa CHUMBA CHA WAGONJWA MAHUTUTI.
Jamaa akanishika tisheti na kunigeuza huku akirusha ngumi ambayo kabla haijanifikia nikaidaka na kumuangalia kwa macho ya kumshangaa na kuzifanya kumbukumba za tukio lake na langu linalo endelea katika sehemu hii kurudi
“Oyaa brother vipi wewe?”
 
“Sio vipi stozi zako nimezipata na utajuta kunijua”
Jamaa alizungumza huku akilivua koki lake la suti kwa dhumuni la kupigana na mimi,Akiwa anakamilisha kazi yake ya kulivua koti lake la suti nikampiga ngumi ya pua na kumfanya atoa ukulele mkali huku akiwa ameinama na kuishika pua yake,Watu na waauguzi walipo kwenye eneo hili wakanza kujisogeza kwa haraka huku wengine wakiomba ugomvi usiendelee,
“Wewe dogo lazima nikutafute tuu sehemu yoyote na nilazima nikuue”
 
Jamaa alizungumza huku akishikwa na baadhi ya watu,sikutaka kumjibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kuelekea kwenye chumba ambacho nilimuona Manka akiingizwa kabla sijakifikia madaktari wawili wakanizuia
“Huwezi kuingia humu ndani?”
“Kwa nini?”
“Hichi ni chumba cha wagonjwa mahututi haturuhusu mtu wa aina yoyote kuingia humu hususani wewe ambaye umetuchafulia hewa ya hospitli”
 
Daktari mmoja alizungumza huku akinitazama kwa macho makali kiasi kwamba nikajikuta nikibaki nimemtazama.Nikatoka nje na kuifungua simu yangu sehemu ya Internet na kuingia kwenye mtandao wa google na kuanza kuitafuta habari ambayo nimeiona kwenye Tv,Nikaingia kwenye tovuti ya BBC Swahili na taarifa ya kwanza kuikuta ni ambayo inahusiana na kupotea kwa ndege ambayo hadi wanakwenda mitamboni hawakujua ni wapi ilipo.Nikajikuta nikizidi kuchanganyikiwa na kuanza kuzungumza mwenyewe
 
“Ila mama mimi nilikuwambia usiende ila wewe umejifanya mbishi unaona sasa yaliyo kukuta”
Nilizungumza huku machozi yakinimwagika,Nikaingia kwenye taksi nilio kuja nayo na kumuomba dereva anipeleke kwenye hospitali aliyolazwa Sheila
“Kaka mbona unalia?”
“Ahaaa hakuna kitu kaka”
“Hapana una ndugu aliye fariki nini hapo hospitalini?”
“Hapana ila kuna mambo yangu binafsi tuu”
“Sawa kaka ngoja nikuwashie redio usikilize muziki upunguze mawazo”
Dereva wa taksi akawasha redio ya gari yake na tukaanza kusikiliza nyimbo kwenye stesheni moja ambayo sikujua ni stesheni ya wapi.Mara gafla miziki ikakatishwa na kukaja taarifa ya habari na sauti nzito ya muandishi wa habari ikaanza kusikika vizuri masikioni mwangu
 
“TAARIFA KUTOKA IKULU ZINASEMA NDEGE ILIYOBEBA VIONGOZI WA NCHI YA TANZANIA YA SHIRIKA LA KLM IMEPOTEA KATIKA MAZINGIRA YA KUTATANISHA NA INASADIKIKA KUWA IMETEKWA NA MARUBANI HAO AMBAO WAMEZIMA MITAMBO YA RADA INAYO ONYESHA SEHEMU AMBAZO NDEGE HIYO HUPITA.
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI ANAWAOMBA WANANCHI WAWE WASIKIVU KWANI UMOJA WA MATAIFA WAMETUMA NDEGE ZA KIJESHI KWENDA KUIFWATILIA NDEGE HIYO”
 
Nikajikuta nikijifunga mdomo huku machozi yakizidi kunimwagika na sura yangu nikaiinamisa chini na sikutaka dereva aelewe ni kitu gani kinacho endelea
“Ahhh acha watekwe bwana kwa maana wamezidi kula pesa za serikali.Watu wanakaa na kujaziana matumbo yao na sisi wananchi wa hali ya chini tanazidi kufa kwa tabu kila siku vitu vinapanda bei”
 
Maneno ya dereva Taksi yakazidi kuumiza moyo wangu huku hasira ikinipanda na kujikuta nikiyang’ata meno kwa nguvu ili kuizuia hasira yangu na mbaya zaidi katika maisha yangu mimi ni miongoni mwa watu wagonjwa wa hasira na siku zote huwa nikikasirika ninaweza kufanya maamuzi ambayo yatapelekae baadaye kujutia
“Unajua hawa vionngozi wetu wamezidi kutunyanyasa hapa utakuta walikuwa wanakwenda kula bata na hao Marubani wamewapatia kweli kwa maana ni washenzi sana”
Dereva alizidi kuzungumza huku akiongeza sauti ya redio ili asikilize majina ya viongozi sita waliomo ndani ya dege hiyo huku wengine wakitokea Kenya.Jina la mama yangu likwa ni lasita katika kutajwa na kumfanya  dereva taksi kuanza kucheka
 
“Haaa huyu mama naye yuopo.....Kweli Mungu hapendi dhambi kuna siku bwana alikuwa na dereva wake sasa kwa bahati mbaya nikamchomekea kwa mbele ile barabara ya kuingilia K.C.M.C nilikuwa namuwahisha mgonjwa hospitalini.Ahaaaa alikwenda kunilaza polisi hadi siku anaondoka Arusha ndio wakaniachia......Tena hao watekaji kama wanajua wamfanye wa kwanza kufa kwa maana yule mama roho mbaya sana”
 
Maneno ya dereva yakazidi kunipandisha hasira hadi mwili mzima ukaanza kunitetemeka huku misuli ya mwili wangu ikikaza na kujikuta nikikunja ngumi na kuipiga kwenye sehemu niliyokuwa nimeinamisha kichwa na kusababisha kifuniko chake kuchangukuka
“Aiiseee inakuwaje chalii wangu mbona unanaribia gari yangu,”
“Funga bakuli lako”
Nilizungumza huku meno yangu nikijitahidi kuyang’ata kwa nguvu kwani kiwango cha hasira kinazidi kuongezeka huku mapigo yangu ya moyo yakienda kwa kasi huku jasho likinimwagika
“Haa wewe vipi umearibu gari yangu unaniambia ninyamaze....Kama umechanganywa na mambo yangu ndio unizingu mimi na utalipa tuu”
“Funga bakuli lako nitakuua”
“Wewe fala kweli nani umuue?”
 
Dereva alizngumza huku akipunguza mwendo wa gari,Nikakishika kwichwa chake kwa nyuma na kukigongesha kwenye mskani mara tatu mfululizo na nikasababisha gari kuanza kuyumba na likatoka barabarani na tukajikuta likiingia kwenye mtaro na kulalia upande wa dereva huku kichwa changu kukichanwa na kioo kwenye sehemu ya paji la uso na damu zikaanza kunijaa usoni,Sikutaka kumuangalia dereva taksi anaendeleaje na nikaanza kujitahidi kuufungua mlango wa gari na watu wakaanza kukusanyika na kunisaidia katika kuufungua kwa kwa nje na kunitoa ndani ya gari.Kutokana na wenge nikataka kuondoka eneo la ajali ila wakanizuia huku wakinikalisha chini kiulazima
 
“Jamani musimzunguke mpeni hewa ajisikie vizuri”
Jamaa mmoja alizungumza huku akiwasogeza watu wanao nishangaa,dada mmoja akaanza kunifuta damu zilizo samba usoni kwangu na sikujisikia maumivu ya aina yoyote
“Begi langu lipo wapi?”
Niliwaauliza watu na mtu mmoja akaniletea begi langu na kuliweka sehemu niliyokaa,Nikawaona wakijitahidi kumtoa dereva taksi ambaye sikujua kama amekufa au laa,
“Jamani tumuwahisheni hospitali”
“Nipo salama”
“Kaka umeumia damu zinakutoka bado”
“Zitakata zenyewe”
“Dada huyo mnamsemesha hapo akili sio zake cha msingi ngoja kuna teksi imekwenda kuchukuliwa tumpeleke hospitali”
Simu yangu ikaanza kuita na dada aliyekuwa akinifuta damu akaanza kunisaidia kuitoa mfukoni na akanionyesha namba ambayo kwa ukungu ulio nitawala machoni mwangu sikuweza kuigundua kwa haraka
“Ipokee”
Dada akaipokea na kuisikilizia huku akiwa ameiweka laud speaker
 
“Eddy upo wapi mume wangu mbona makelele?”
“Samahani dada yangu”
“Wee ni nani unaye ipokea simu ya mume wangu?”
“Mimi ni masamaria mwema mume wako amepata ajali ya gari na hapa alipo hawezi kuzungumza vizuri”
“Mungu wangu ni mzima?”
Nikagundua ni sauti ya Sheila na kukumbuaka hali yeka aliyo nayo ikanibidi nimpokonye dada simu na kuiweka sikioni
“Baby sijaumia sana?”
“Eddy ni wewe?”
“Ndio mke wagu sijaumia sana na usiwe na presha”
“Baby usife....nitabaki na nini jamani mume wangu”
Sheila alizungumza huku nikimsikia akiwa analia
“Baby siwezi kufa nakuomba uache kulia si unajua hujapona vizuri utazifanya hizo nyuzi za kidonda kuachia”
“Baby kama haujaumia basi waambiea wakulete huku hospili”
 
“Sawa baby ila nyamaza kulia”
Nikakata simu na kuiweka mfukoni na kunyanyuka nikisaidiwa na baadhi ya watua na tukaingia kwenye moja ya taksi na nikawaomba wanipeleke kwenye hospitali aliyo lazwa Sheila na madaktari wakanipokea na kuniingiza kwenye chumba ambacho wakananishona kwenye jerala langu la usoni na kunifunga bandeji.Nikaelekea kwenye chumba alicholazwa Sheila na kumkuta akiwa yupo na nesi wakiomba huku mikono yao wakiwa wameiweka juu ya Biblia na macho yao wakiwa wameyafumba.Nikawaacha wamalize kuomba na wakafumbua macho na kuniona nikiwa nimekaa pembeni ya kitanda alicho lala Sheila na akaonekana kunishangaa huku machozi yakimwagika
“Eddy upo salama?”
“Nipo nipo mke wangu sawa”
“Pole mwanangu”
Nesi ambaye ni miongoni mwa masister wa kanisa la katoliki wanaofanya kazi katika hospitali hii alinipa pole na nikamuitikia kwa sauti ya upole na yenye unyonge ndani yeke
 
“Mwanangu hujaumia sana?”
“Sijaumia sana ni hapa usoni ndio nimechanwa na kiio cha gari”
“Eddy afandhali hujumia sana ila gari halina dhamani kwangu kuliko wewe”
“Sikwenda na gari yetu nilikuwa nimepnda taksi”
“Pole sana mwanangu.....ngoja niwaache ninakwenda kuendelea na shuhuli nyingine”
Nesi akatoka ndani ya chumba na kutuacha tukiwa kimya,Nikamsogelea Sheila na kumfuta machozi taratibu na ukimya ukatawala ndani ya chumba
 
“Eddy”
“Naaamm”
“Mbona unaonekana una mawazo?”
“Ni mama?”
“Amefanyaje?”
“Ametekwa kwenye ndege?”
“Weee”
“Ndio”
“Wewe umejuaje?”
“Nmesikia kwenye taarifa ya habari”
“Mmmm Eddy turudi Dar tukajue ni nini kinacho endelea”
“Tutarudi hadi wewe upone”
“Nmeshapona mume wangu?”
“Haujapona vizuri mpaka madaktari wakikupa ruhusa ndio tutarudi Dar”
Simu yangu ikaita na kukuta ni namba ngeni ndio inayopiaga tena ni namba ya mezani.Nikaitazama kwa muda kisha nikaipoke
“Habari yako Eddy”
 
Sauti nzito ya kiume ilisikika kutoka upande wa pili wa simu na kunifanya nistuke kidogo
“Salama nani mwanzangu?”
“Mimi ni mkuu wa upelelezi wa Taifa nimepewa jukumu la kukujuisha kitu kinachoendelea juu ya mama yako”
“Sawa”
“Nina taarifa ambayo sio nzur sana kwa mama,kwanza tunakuomba usiwe na wasiwasi kwa maana hali ya abiria wote waliomo kwenye ndege ya shirika la KLM tumegundua wanaendelea vizuri akiwemo mama yako na hapa tunafanaya juhudi za kuwaokoa na nitazidi kukujulisha kila kitakacho endelea”
“Sawa nashukuru kwa taarifa yako”
Nilizungumza kwa sauti ya unyonge na simu ikakatwa na nikairudisha mfukoni huku nikimtazama Sheila
“Wamewapata?”
“Bado”
 
“Ohoo Mungu wangu msaidie mama yangu mkwe anusurike na matatizo hayo”
Maneno ya Sheila yaliyojaa huzuni yakaamsha hisia zangu za kulia na kujikuta nikimkumbatia Sheila na akaanza kuniliwaza na maneno matamu
“Ni wapi nimekosea kwenye maisha yangu Mungu wangu kwa nini kila siku ni mimi..Likiiasha hili linakuja hili kama ni vipi ni bora nife kuliko kupitia kipindi hichi kigumu kwenye maisha yangu”
 
Nilizungumza huku machozi yakizidi kuni kunitiririka huku moyoni mwangu nikiwa nimekosa amanani na kukata tama ya kushi kabisa duniani
“Eddy kwanini unazungumza hivyo.....Unataka mimi niishi peke yangu? Unadhani wewe ukifa mimi nitaishije ninaamini kwamba wewe unaijua historia ya maisha yangu.Sina baba,Mama,kaka,dada wala jamaa wa karibu.Eddy wewe ndio mwanga wangu...wewe ndio baba yangu..wewe ndio mama yangu.Ukifa wewe na mimi nilazima nife”
 
Sheila akazidi kuniongeza uchumgu wa kulia kwani kusema kweli kila hatua ya maisha yangu ninayopitia kwangu inamikosi
 
“Sheila hata mimi nikifa nakuomba usijiue...Mimi ni mwaname natambua wewe utapata mwanaume mwengine wa kukuoa ila usije ukafanya hivyo kwa ajili yangu”
“Eddy hapana wewe ndio kila kitu kwangu kwa sasa..Japo tunamuda mfupi ila kwako nimepata tulizo la moyo wangu”
Nikanyanyuka kitandani na kufungua dirisha na kuchungulia kwa chini nikiangalia watu wanao ingia na kutoka ndani ya hospitalini hii.
Mawazo ya ajabu yakaanza kunitawala akilini mwangu na gafla nikamuona mama kwa chini akiwa amekaa pembeni ya jeneza huku akiwa amevalia nguo yeupe huku puani akiwa na pamba na akaanza kuniita huku akilia kwa uchungu kiasi kwamba nikaanza kuchanganyikiwa,Kwa nyuma yake akatokea mtu mwenye nyundo kubwa na kuinyanyua juu na kuanza kumshindilia nyondo za kichwani na kusababisha damu kuruka na mtu huyo akaanza kucheka huku akuninyooshea kidole.Kwa hasira nikapanda kwenye dirishana kabala sijajirusha nikastukia nikishikwa kwa nyuma na kuaza kuvuta na madaktari wawili wa kiume
“Eddy mume wangu nini unataka kufanya....Kwa nini unataka kujiua,Eddy nakupenda tena nakupenda sana mume wangu kwa nini jamami?”
Sheila alizungumza huku akilia kiasi kwamba akataka kushuka kitandani ila madaktari wakamzuia
“Mama yangu amekufa”
“Eddy mama hajafa”
 
“Mama yangu amekua mimi nitaishi na nini.....Hadi sasa hivi simjui nani na baba yangu halisi”
“Eddy mama hajafa nakuomba usimpe shetani mawazo kama hayo yakatawala kichwani kwako”
“Sheila nimemuona mama pele chini yupo kwenye jenezaa na kuna mtu amempiga hadi amekufa”
“Baby sio mama.....Dokta namuomba mumlete hapa”
Madaktari wakanikalisha kwenye kitanda na Sheile hakujali kama anajeraha kifuni kwake,akanivuta na kunikumbatia kwa nguvu huku sote tukiendelea kulia
“Mama amekufa”
“Eddy acha kuzungumza hivyo nakuomba tafandali”
“Sheila”
“Mmmm”
“Unanipenda?”
“Eddy nakupenda tena sana”
“Nakuomba nife”
“Eddy ni nini unacho kizungumza?”
 
“Sheila mama yangu ameshakufa sina dhamani tena duniani...Mama yangu ndio rafiki yangu wa karibu.....Sheila mimi sina upendo wa baba si...”
Sheila akanivuta na kuanza kuninyonya mdomo kwa nguvu kunizuia nisiendelee kuzungumza,Madaktari wakatoka ndani ya chumba na kutuacha tukiendelea na kitendo ambacho kilianza kuusisimua mwili wangu.Sheila akauchukua mkono wangu na kuushikisha kwenye chuchu yake ya kushoto na nikaanza kuiminya taratibu ila nikajikuta nikimuachia Sheila
“Sheila unaumwa sitaki tufanye sasa hivi”
“Eddy....”
 
“Hapana unaumwa”
“Ok mume wangu asante kwa kunijali.....Alafu baby ukilia unakuwa kama yale makatuni ya Tom na Jerryjea yakilia”
Nikajikuta nikitabasamu na kumfanya Sheila na yeye kutabasamu huku akiishika shika pua yangu na kuanza kuiminya minya kiasi kwamba furaja yangu ikaanza kunirejea taratibu
“Na wewe ukilia unakuwa kama wale katuni wa powefull girl machozi yao yanaruka kama maji haswa yule Babon akilia machozi yanaruka hayo kama bomba lililo pasuka”
“Jamani baby kwa hiyo machozi yangu yanaruka kama maji ya bomba lililo pasuka?”
“Ndio unatisha kama nini?”
“Hata wewe ukilia unatisha unakuwa kama yale mazombi ya wrong turn...Kuna ile sijui ni part one kuna kazombi kamoja kaliuliwa wacha baba mtu aanze kulia sasa yule ndio unafanana nye”
 
Nikazidi kucheka huku na kujikuta nikisahau tukio lililo tokea katika dakika chache zilizo pita
“Basi na wewe unakuwa kama yule kale kasichana kwenye wrong turn kalicho mfumania jamaa yake akiwachungulia jamaa wakifanya mapenzi....Uliona jinsi kalivyokuwa kanalia kwa hasira”
“Mmmmmm haya baby wewe ndio umeshindi....Mume wangu unapenda nikuzalie mtoto wa kike au wa kiume”
“Nataka wa kike ili mtu akija kumchumbia kitangulizi cha mahari nataka mabasi saba”
“Hahaa mume wanagu hayo mabasi saba jamani mtu wa watu atayatolea wapi au ndio hivyo unataka ujipatie mtaji kupitia mtoto wako?”
 
“Ndio na atakuwa mzuri kama wewe mama yao”
“Mmmmm mimi nataka wachukue lipsi zako na macho yako?”
“Sawa itakuwa ni vizuri pia.....Eddy nikuambie kitu?”
“Niambie”
“Mungu akipenda nahitaji unioe kwa ndoa ya kanisani”
“Nikimaliza kusoma tuu nafunga ndoa na wewe”
“Kwelu mume wangu?”
“Kweli kwani nahitaji kuyaanza maisha mapema”
“Kweli mume wagu...Alafu nilikuwa nimesahau,Vipi shuleni kwenu hali inaendeleaje?”
“Mmmm hata mimi sijui inaendeleaje alafu sina namba ya simu ya mtu wa shule nikamuuliza”
 
“Mume wangu ninahitaji usome na mimi baada ya kukuzalia tu mtoto nitarudi shule kusoma kwa maana nahitaji familia yetu iwe ya wasomi zaidi hata ukimuhimiza mtoto asome kweli awe anasoma kweli.....Sio mama unamumbia mtoto nenda shule wakati wewe mwenyewe shule hukuipenda”
“Kweli mke wangu ila vipi umeshakula?”
“Baby nilionja onja kwani muda ule nilipopiga simu na ikapokelewa na mwanamke ndio muda ambao nilikuwa ninakula chakula na baada ya simu ile hamu ya kula yote ikapotea”
“Ngoja nikanunue chispi tuje tule...Tena nimekubuka nikakununulie na simu kabisa sipendi hivi unavyo azima azima simu za watu”
 
“Sawa baby ila nakuomba usichelewe na kama unakwenda tumia gari usipande kwenye hizo ndubwasha zinazo endeshwa na wavuta bangi na ukapata ajali bure”
“Sawa baby...ila kwa mbali ninaanza kuhisi kichwa kinaniuma”
“Pole baby nenda ukanywe dawa kwanza ndio uende huko unaotaka kwenda”
“Hapa dawa nitazipatia wapi?”
“Mume wangu hospitali nzima ukose dawa za kunywa.....Sikia nenda kwenye ofisi iliyopo pale chini ya ngazi kuna masister utawakuta waombe na watakusaidia”
“Sawa baby”
 
Nikambusu Sheila mdomoni na kufungua mlango na kutoka na moja kwa moja nikashuka hadi kwenye chumba alicho nielekeza  Sheila.Nikagonga mlango mara tatu na suti ya kike iliyopo ndani ya chumba hicho ikaniruhusu niingie.Nikafungua mlango na kuwakuta manesi watatu wakiwa wameshika mashavu yao huku wakionekana wanyongea na macho yao wameyaelekezea kwenye kioo cha Tv iliyopo ndani ya chumba hicho.
Na mimi ikanibidi ninagalie wanacho kitazama na kukuta mipigo ya moyo yakiende kwa kasi baada ya kuiona ndege kubwa ikiwa imeanguka huku inawaka moto na kutoa moshi mwingi na mweusi huku kikosi cha zima moto ambacho sikujua ni cha nchi gani wakijitahidi kuzima moto kwa kutumia magari yao maalumu ya kuzimia moto huku baadhi ya miili inayoonekana kuwa imefariki ikitolewa ndani ya ndege hiyo
 
 ITAENDELEA....
RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 23 & 24 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea ) RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 23 & 24 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea ) Reviewed by WANGOFIRA on 21:38:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.