CHAKUA yapinga ongezeko tozo ya abiria UBT
CHAMA cha Kutetea Abiria Tanzania (Chakua) kimesema hakikubaliani na
ongezeko la tozo ya abiria katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo
mikoani na nchi jirani cha Ubungo (UBT) iliyoanza Julai mosi mwaka huu.
Akizungumza na gazeti hili jana, Mwenyekiti wa Chakua, Haasan
Mchanjama alisema, kuongezeka kwa tozo kabla ya kituo kuboreshwa ni
kuwaumiza wananchi na abiria wanaotumia kituo hicho.
“Hatukubaliani na hatujapendezewa na kitendo cha ongezeko la tozo
huku kituo kikiwa hakina huduma za msingi, mantiki ya ongezeko la tozo
inamaanisha huduma za msingi zinapatikana,” alisema Mchanjama.
Alisema licha ya kuongezeka kwa tozo hiyo bado abiria wanapoingia
katika kituo hicho wanalipia huduma za msingi ikiwemo choo, huku abiria
na wananchi wakiendelea kuumia kwa kukosa sehemu za kupumzika pindi
wawapo katika kituo hicho.
“Tunajaribu kuwasiliana na wadau wengine kuona namna tunaweza kufanya
kuhusu ongezeko hili, tozo katika kituo hicho ilianza muda mrefu lakini
hakuna maboresho yoyote, tunahoji fedha hizo walizipeleka wapi?”
alisisitiza.
Hivi karibuni Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam iliongeza tozo
katika kituo hicho, akizungumza Mkuu wa kitengo cha itifaki na uhusiano
wa Halmashauri ya Jiji, Gaston Makwembe alisema awali kituo hicho
kilikuwa kikisimamia uendeshaji wa shughuli zote za kituo kwa kutumia
Sheria Ndogo ya Mwaka 2004 ya Kituo Kikuu cha Mabasi, hivyo kwa sasa
inaanza kutumika Sheria Ndogo ya Mwaka 2009 ambayo imefuta matumizi ya
sheria ya Mwaka 2004.
Alisema sheria hiyo ndogo ya mwaka 2009 inawataka wasindikizaji wote
wa abiria watakaoingia katika kituo hicho kulipia Sh 300 badala ya Sh
200 iliyokuwepo awali.
Chanzo HABARI LEO
CHAKUA yapinga ongezeko tozo ya abiria UBT
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:16:00
Rating:
No comments: