KAMATI YA MAADILI TFF YAMPIA PINI JERRY MURO, KUTOJISHUGHULISHA NA MASWALA YA SOKA KWA MWAKA MMOJA
MKUU wa
Idara ya Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Yanga, Jerry Muro (pichani)
amefungiwa mwaka mmoja kujihusisha na masuala ya soka pamoja na kutozwa
faini ya Sh. Milioni 3, baada ya kikao cha Kamati ya Maadili ya
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kilichokaa leo kwenye Makao Makuu ya
Shirikisho hilo, chini ya Mwenyekiti wake, Wakili Wilson Ogunde
Muro
amefungiwa baada ya kukutwa na hatia katika mashitaka mawili kati ya
matatu yaliyowasilishwa na TFF mbele ya Kamati ya hiyo, ambayo ni
kudharau maamuzi ya Kamati ya Nidhamu ya TFF mwaka 2015 alipotakiwa
kulipa faini ya Sh. Milioni 5 baada ya kufanya makosa, lakini amekaidi
kulipa hadi leo, akahukumiwa kutengana na kutojihusisha na masuala ya
soka kwa mwaka mmoja, wakati shitaka lingine ni kuchochea vurugu na
kuhatarisha amani kuelekea mchezo wa Kundi A Kombe la Shirikisho kati ya
Yanga na TP Mazembe ya DRC.
Katika
shitaka hilo, Jerry alidaiwa kuwashawishi mashabiki wa Yanga kujitokeza
kwa wingi kuishangilia timu yao na kutowapa nafasi watani wao wa jadi
(Simba) kuingia kwenye mchezo huo ambao timu yake ilifungwa bao 1-0 na
Mazembe Juni 28, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hata
hivyo, Jerry Muro alifanikiwa kuishinda TFF katika shitaka la kupingana
na maamuzi ya shirikisho hilo juu ya masuala ya utoaji wa haki za
matangazo ya Televisheni.
“Kamati
ilisikiliza kwa makini taarifa zake alipokuwa anazungumza na vituo vya
Redio na kugundua alikuwa sahihi, hivyo hapa hana hatia,”kimesema
chanzo.Hata hivyo, Jerry Muro amehukumiwa wakati mwenyewe hakuwepo
kwenye kikao na inadaiwa hakutoa taarifa ya maandishi juu ya
kutohudhuria kwake.
Badala
yake, imeelezwa Katibu wa Yanga, Baraka Deusdedit alifika mapema leo
kabla ya kikao kwa ajili ya kutoa taarifa ya mdomo kwamba Muro amekwenda
kwao Kilimanjaro kusafisha makaburi ya wazee wake.
Lakini
Kamati ikaamua kuendelea na kikao kwa mujibu wa kanuni na hatimaye
kuchukua hatua ilizochukua. Hata hivyo, Muro ana haki ya kukata rufaa
Kamati ya Rufaa ya TFF.
KAMATI YA MAADILI TFF YAMPIA PINI JERRY MURO, KUTOJISHUGHULISHA NA MASWALA YA SOKA KWA MWAKA MMOJA
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:19:00
Rating:
No comments: