Watuhumiwa wa Mauaji Jijini Mwanza na Tanga Wauawa Dar es Salaam Seebait.com 2016SeeBait MTU mmoja anayedaiwa kuhusika katika mauaji yaliyotokea katika Msikiti wa Rahma, jijini Mwanza ameuawa. Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam leo limeeleza kumuua Salum Saidi Muhangwa (30) kwa madai ya kuwa miongoni mwa waliofanya mauaji kwenye msikiti huo. Akizungumza na wanahabari Simon Siro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam amesema, mtu huyo ameuawa leo asubuhi wakati akijaribu kuwakimbia polisi kupitia dirishani. “Baada ya kufanya mauaji kule Mwanza na kikundi chake walikimbilia huku Dar es Salaam, taarifa za raia wema zimetuonesha jambazi huyo alikua anaishi Buguruni,” amesema. Mauaji hayo yalifanyika tarehe 19 Mei mwaka huu katika msikiti huo uliopo kwenye Kata ya Mkolani wilayani Nyamagana ambapo watu watatu, waumini wa msikiti huo waliuawa wakati mwingine mmoja akijeruhiwa. Kamanda Sirro amesema, mtu huo baada ya kugundua kuwa askari wamezunguka jengo alilokuwemo, alijaribu kujihami kwa kuwarushia askari bomu la mkono ambapo askari walifanikiwa kumpiga risasi ya mguu hatimaye kufariki wakati akipelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). “Tunashukuru askari hawakufanywa lolote katika tukio hilo na tunashukuru kwa sababu wapo makini,”amesema Kamanda Sirro. Hata hivyo amesema, mtu huyo amefanya matukio mengi pale Mwanza yakiwemo kufanya unyang’anyi katika vituo vya M-Pesa, Tigo Pesa, uchinjaji watu msikitini pamoja na maduka makubwa. “Kuna timu yake imebaki hapa Dar es Salaam lakini tuwahakikishie wana Dar es Salaam kwamba, tutawakamata na haki itatendeka lakini wakikaa vibaya wasilaumu serikali. “Kwa sababu silaha wanazozitumia hawajanunua madukani, wanakaa nazo visivyokua halali wabadilike wawe raia wema itawasaidia lakini kwa staili hii niwaambie wataacha familia zao kwa sababu ukamataji wa mtu mwenye silaha sisi ndio tunajua namna ya kukamata,”amesema. Katika tukio jingine, Jeshi hilo limefanikiwa kumkamata jambazi sugu aliyefahamika kwa jina la Mohamed Abdallah akiwa na bastora aina ya nolinko, risasi 19 na bomu la kutupa kwa mkono. “Baada ya kufanya mauaji Tanga na kikundi chake walikimbilia hapa Dar es Salaam, naye akachomoka na kuanza kupambana na polisi, na askari wetu waliweza kumjeruhi vibaya sana naye wakati akipelekwa hospitali alifariki dunia." Kamanda Siro amesema mtu huyo ni kiongozi mkubwa aliyebaki katika kundi la majambazi mkoani Tanga na amehusika katika mauaji ya watu wanane pamoja na ujambazi uliofanyika katika kituo cha mafuta mjini humo. “Wananchi na hasa raia wema waendelee kutupa taarifa kwa watu wanaowatilia mashaka,” amesema. Advertisement == Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana ) Newer Post Older Post Home My Blog List DAR ES SALAAM WIRE New Fastjet Boss plans to relocate head office to Tanzania or SA - *Fastjet’s CEO Nico Bezuidenhout* Fastjet Plc’s new chief executive officer said he may replace the African discount carrier’s planes with smaller ones a... GUMZO LA JIJI Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Manunuzi Wasomwa .....Waliohukumiwa kwa Rushwa Kunyimwa Zabuni, Mikataba yote Kuwa na Mashuhuda - MUSWADA wa Marekebisho ya Sheria ya Manunuzi wa Mwaka 2016, umesomwa kwa mara ya kwanza bungeni jana na kuwekwa wazi kwa umma, na moja ya vifungu vinavyop... NEWZ XTRA Kenyan Wednesday Newspaper Front Pages - Habari Mpya HABARI MPYA Zilizosomwa Zaidi Breaking News: Orodha Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Na Kidato Cha Tano Na Vyuo Vya Ufundi Kwa Mwaka 2016 Majina ya Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano, 2015/ 2016 Breaking News: Rais Magufuli Afanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya na Afanya Mabadiliko Madogo ya Wakuu wa Mikoa Zitto Kabwe Amjibu Rais Magufuli Magufuli Ashusha Nyundo 7.....Apasua makampuni ya madini, Mafao hewa na miamala ya simu Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 24 Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya June 26 Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya June 27 Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya June 21 Rais Magufuli Atengua Uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo My Blog List Advert Seebait.com 2016SeeBait Ungana Nasi Facebook Followers Blog Archive
MTU mmoja anayedaiwa kuhusika katika mauaji yaliyotokea katika Msikiti wa Rahma, jijini Mwanza ameuawa.
Jeshi
la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam leo limeeleza kumuua Salum
Saidi Muhangwa (30) kwa madai ya kuwa miongoni mwa waliofanya mauaji
kwenye msikiti huo.
Akizungumza
na wanahabari Simon Siro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es
Salaam amesema, mtu huyo ameuawa leo asubuhi wakati akijaribu kuwakimbia
polisi kupitia dirishani.
“Baada
ya kufanya mauaji kule Mwanza na kikundi chake walikimbilia huku Dar es
Salaam, taarifa za raia wema zimetuonesha jambazi huyo alikua anaishi
Buguruni,” amesema.
Mauaji
hayo yalifanyika tarehe 19 Mei mwaka huu katika msikiti huo uliopo
kwenye Kata ya Mkolani wilayani Nyamagana ambapo watu watatu, waumini wa
msikiti huo waliuawa wakati mwingine mmoja akijeruhiwa.
Kamanda Sirro amesema, mtu huo baada ya kugundua kuwa askari wamezunguka jengo alilokuwemo,
alijaribu kujihami kwa kuwarushia askari bomu la mkono ambapo askari
walifanikiwa kumpiga risasi ya mguu hatimaye kufariki wakati akipelekwa
katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
“Tunashukuru askari hawakufanywa lolote katika tukio hilo na tunashukuru kwa sababu wapo makini,”amesema Kamanda Sirro.
Hata
hivyo amesema, mtu huyo amefanya matukio mengi pale Mwanza yakiwemo
kufanya unyang’anyi katika vituo vya M-Pesa, Tigo Pesa, uchinjaji watu
msikitini pamoja na maduka makubwa.
“Kuna
timu yake imebaki hapa Dar es Salaam lakini tuwahakikishie wana Dar es
Salaam kwamba, tutawakamata na haki itatendeka lakini wakikaa vibaya
wasilaumu serikali.
“Kwa sababu silaha
wanazozitumia hawajanunua madukani, wanakaa nazo visivyokua halali
wabadilike wawe raia wema itawasaidia lakini kwa staili hii niwaambie
wataacha familia zao kwa sababu ukamataji wa mtu mwenye silaha sisi ndio
tunajua namna ya kukamata,”amesema.
Katika
tukio jingine, Jeshi hilo limefanikiwa kumkamata jambazi sugu
aliyefahamika kwa jina la Mohamed Abdallah akiwa na bastora aina ya
nolinko, risasi 19 na bomu la kutupa kwa mkono.
“Baada
ya kufanya mauaji Tanga na kikundi chake walikimbilia hapa Dar es
Salaam, naye akachomoka na kuanza kupambana na polisi, na askari wetu
waliweza kumjeruhi vibaya sana naye wakati akipelekwa hospitali
alifariki dunia."
Kamanda
Siro amesema mtu huyo ni kiongozi mkubwa aliyebaki katika kundi la
majambazi mkoani Tanga na amehusika katika mauaji ya watu wanane pamoja
na ujambazi uliofanyika katika kituo cha mafuta mjini humo.
“Wananchi na hasa raia wema waendelee kutupa taarifa kwa watu wanaowatilia mashaka,” amesema.
Watuhumiwa wa Mauaji Jijini Mwanza na Tanga Wauawa Dar es Salaam Seebait.com 2016SeeBait MTU mmoja anayedaiwa kuhusika katika mauaji yaliyotokea katika Msikiti wa Rahma, jijini Mwanza ameuawa. Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam leo limeeleza kumuua Salum Saidi Muhangwa (30) kwa madai ya kuwa miongoni mwa waliofanya mauaji kwenye msikiti huo. Akizungumza na wanahabari Simon Siro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam amesema, mtu huyo ameuawa leo asubuhi wakati akijaribu kuwakimbia polisi kupitia dirishani. “Baada ya kufanya mauaji kule Mwanza na kikundi chake walikimbilia huku Dar es Salaam, taarifa za raia wema zimetuonesha jambazi huyo alikua anaishi Buguruni,” amesema. Mauaji hayo yalifanyika tarehe 19 Mei mwaka huu katika msikiti huo uliopo kwenye Kata ya Mkolani wilayani Nyamagana ambapo watu watatu, waumini wa msikiti huo waliuawa wakati mwingine mmoja akijeruhiwa. Kamanda Sirro amesema, mtu huo baada ya kugundua kuwa askari wamezunguka jengo alilokuwemo, alijaribu kujihami kwa kuwarushia askari bomu la mkono ambapo askari walifanikiwa kumpiga risasi ya mguu hatimaye kufariki wakati akipelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). “Tunashukuru askari hawakufanywa lolote katika tukio hilo na tunashukuru kwa sababu wapo makini,”amesema Kamanda Sirro. Hata hivyo amesema, mtu huyo amefanya matukio mengi pale Mwanza yakiwemo kufanya unyang’anyi katika vituo vya M-Pesa, Tigo Pesa, uchinjaji watu msikitini pamoja na maduka makubwa. “Kuna timu yake imebaki hapa Dar es Salaam lakini tuwahakikishie wana Dar es Salaam kwamba, tutawakamata na haki itatendeka lakini wakikaa vibaya wasilaumu serikali. “Kwa sababu silaha wanazozitumia hawajanunua madukani, wanakaa nazo visivyokua halali wabadilike wawe raia wema itawasaidia lakini kwa staili hii niwaambie wataacha familia zao kwa sababu ukamataji wa mtu mwenye silaha sisi ndio tunajua namna ya kukamata,”amesema. Katika tukio jingine, Jeshi hilo limefanikiwa kumkamata jambazi sugu aliyefahamika kwa jina la Mohamed Abdallah akiwa na bastora aina ya nolinko, risasi 19 na bomu la kutupa kwa mkono. “Baada ya kufanya mauaji Tanga na kikundi chake walikimbilia hapa Dar es Salaam, naye akachomoka na kuanza kupambana na polisi, na askari wetu waliweza kumjeruhi vibaya sana naye wakati akipelekwa hospitali alifariki dunia." Kamanda Siro amesema mtu huyo ni kiongozi mkubwa aliyebaki katika kundi la majambazi mkoani Tanga na amehusika katika mauaji ya watu wanane pamoja na ujambazi uliofanyika katika kituo cha mafuta mjini humo. “Wananchi na hasa raia wema waendelee kutupa taarifa kwa watu wanaowatilia mashaka,” amesema. Advertisement == Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana ) Newer Post Older Post Home My Blog List DAR ES SALAAM WIRE New Fastjet Boss plans to relocate head office to Tanzania or SA - *Fastjet’s CEO Nico Bezuidenhout* Fastjet Plc’s new chief executive officer said he may replace the African discount carrier’s planes with smaller ones a... GUMZO LA JIJI Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Manunuzi Wasomwa .....Waliohukumiwa kwa Rushwa Kunyimwa Zabuni, Mikataba yote Kuwa na Mashuhuda - MUSWADA wa Marekebisho ya Sheria ya Manunuzi wa Mwaka 2016, umesomwa kwa mara ya kwanza bungeni jana na kuwekwa wazi kwa umma, na moja ya vifungu vinavyop... NEWZ XTRA Kenyan Wednesday Newspaper Front Pages - Habari Mpya HABARI MPYA Zilizosomwa Zaidi Breaking News: Orodha Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Na Kidato Cha Tano Na Vyuo Vya Ufundi Kwa Mwaka 2016 Majina ya Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano, 2015/ 2016 Breaking News: Rais Magufuli Afanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya na Afanya Mabadiliko Madogo ya Wakuu wa Mikoa Zitto Kabwe Amjibu Rais Magufuli Magufuli Ashusha Nyundo 7.....Apasua makampuni ya madini, Mafao hewa na miamala ya simu Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya June 24 Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya June 26 Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya June 27 Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya June 21 Rais Magufuli Atengua Uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Magesa Mulongo My Blog List Advert Seebait.com 2016SeeBait Ungana Nasi Facebook Followers Blog Archive
Reviewed by WANGOFIRA
on
11:46:00
Rating:
No comments: