Aliyeondolewa Ukuu wa wilaya Lushoto ajitetea,adai hakubebwa.
Siku
moja baada ya Rais John Pombe Magufuli kutangaza upya nafasi za wakuu
wapya wa wilaya nchini, aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Lushoto mwenye umri
mdogo kuliko wenzake ambaye jina lake limeondolewa katika orodha hiyo
Mariam Juma,amedai kuwa nafasi aliyokuwa ameipata sio kwamba
alichaguliwa kwa upendeleo,na badala yake elimu ndio iliyosababisha
kupata hadhi ya kumuwakilisha Rais wa awamu ya nne.
Amezungumza
hayo na wazazi,viongozi wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri Dayosisi ya
Kaskazini Mashariki,pamoja na viongozi wa serikali ngazi ya wilaya
katika harambee ya kuchangia maendeleo katika chuo cha mafunzo ya
ujasiriamali kilichopo vuga wilayani Lushoto.
Awali
akielezea shughuli zinazofanywa katika Chuo maalum cha kujifunza
ujasiriamali ikiwemo kutengeneza mizinga ya nyuki kwa kutumia udongo wa
mfanyanzi,elimu ya mazingira pamoja na kilimo cha mboga mboga ili
kuwapunguzia vijana changamoto za maisha,Mkuu wa chuo hicho Mchungaji
Yohana Mmaka amesema elimu ya ujasiriamali imekuwa na mafanikio makubwa
kwa kuwawezesha vijana kujitambua.
Kufuatia
hatua hiyo,diwani wa kata ya Vuga wilayani Lushoto Jumaa
Dhahabu,ameiomba serikali kuu kuwahisha mafungu ya fedha za shughuli za
maendeleo katika halmashauri ya wilaya hiyo,kufuatia miradi tofauti
ikiwemo ujenzi wa maabara iliyoanzishwa na rais wa awamu ya nne
kusitishwa.
Aliyeondolewa Ukuu wa wilaya Lushoto ajitetea,adai hakubebwa.
Reviewed by WANGOFIRA
on
11:51:00
Rating:
No comments: