Meli ya mizigo yazama Bahari ya Hindi
MELI ya Mizigo ya Mv. Happy iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kwenda
Zanzibar imezama katika Bahari ya Hindi ikiwa imebeba mbao zaidi ya
1090 na magunia 450 ya viazi mviringo.
Hata hivyo, mabaharia 12 ambao ni wafanyakazi katika meli ya mizigo
ya hiyo wamesalimika kufa maji kwa vile meli hiyo haikuzama yote
katika eneo la Kizingo kisiwani Zanzibar.
Tukio hilo lilitokea jana alfajiri kisiwani Unguja. Mkuu wa Operesheni baharini, Msilimiwa Idd, alisema tukio hilo
lilitokea saa 8.00 usiku baada ya meli hiyo kuyumba kutokana na dhoruba
kali ya upepo.
Alisema ilipotimu saa saa 9.00usiku nahodha wa meli hiyo alipoona
hali imezidi kuwa mbaya akaelekea katika Kisiwa Mchanga ambako
alijikuta akikwama kwa vile upande mmoja wa meli ulikuwa unapitisha
maji.
Meli ya mizigo yazama Bahari ya Hindi
Reviewed by WANGOFIRA
on
11:55:00
Rating:
No comments: