Watu 3 wamepoteza maisha na 2 kunusurika baada ya kula Mihogo yenye sumu.
Katika
hali ya kusikitisha watu watatu wakazi wa kijiji cha Kauzeni wilaya ya
Mvomero mkoani Morogoro wamekufa baada ya kula mihogo inayosadikiwa kuwa
na sumu huku wengine wawili wakilazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa
wa Morogoro na mmoja kupata nafuu na kuruhusiwa.
Akizungumza
na ITV akiwa hospitalini hapo mara baada ya kunusurika kifo Joshua
Msiani amesema anachokumbuka walikuwa katika shughuli zao za kufyatua
tofali ndipo wenzake wakamkaribisha mihogo ya kuchemsha na baada ya kula
ndipo ghafula hali ikawa mbaya na kujikuta yupo hospitalini.
Kwa
upande wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Ulrich Matei amethibitisha
kutokea kwa vifo hivyo ambapo amesema mamlaka husika zimechukua sampuli
ya mihogo na uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo cha vifo hivyo .
Waliofariki dunia kwa tukio hilo ni Daudi Hermani mkazi wa Kauzeni, Omary Mohamed pamoja na Hamisi Mohamed ambao ni mapacha.
Watu 3 wamepoteza maisha na 2 kunusurika baada ya kula Mihogo yenye sumu.
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:40:00
Rating:
No comments: