MAKAHABA 287, WAMETIWA MBARONI NA JESHI LA POLISI JIJINI DSM



Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limefanikiwa kuwakamata jumla ya watu 287 ambao ni dada poa pamoja na kaka poa katika operation maalum iliyofanyika maneo mbalimbali ya Jiji hilo.

Operation hiyo ilitangazwa na kamishna wa kanda maalum mnamo Tarehe 7 mwezi wa 3 na kuazimia kuwakamata madada poa na makaka poa pamoja na wateja wao ambao watakutwa wakiwanunua.

Katika mkoa wa kipolisi wa ilala operation hii imefanikiwa kuwakamata jumla ya madada poa 51 kutoka katika maeneo mbalimbali yakiwemo msimbazi,Buguruni,na stakishari,pia imewakamata jumla ya makaka poa 12 ambapo 11 wanatokea Buguruni na mmoja kutoka msimbazi.

Mkoa wa kipolisi wa temeke umefanikiwa kuwakamata jumla ya madada poa 22,ambapo changombe walipatikana 12,na mbagala walipatikana madada poa 10.
 
Aidha katika mkoa wa kipolisi wa kinondoni operation hiyo imefanikiwa kuwakamata madada poa 76 kutoka maeneo ya osyterbay madada poa 49,magomeni 23,na kawe madada poa 4,pamoja na makaka poa 4.

Akizungumza na wanahabari jana makao makuu ya polisi kanda maalum ya Dar es salaam ,Kamishna wa kanda hiyo CP Simon Sirro aliwataka watu wenye tabia kama hizo kuacha mara moja kwani ni kinyume na mila na desturi za mtanzania ambapo amewataka kutafuta biashara nyingine halali za kufanya.
MAKAHABA 287, WAMETIWA MBARONI NA JESHI LA POLISI JIJINI DSM MAKAHABA 287, WAMETIWA MBARONI NA JESHI LA POLISI JIJINI DSM Reviewed by WANGOFIRA on 09:00:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.