POLISI WAZUNGUMZA BOMU LILILORUSHWA KWENYE NYUMBA YA KAMISHINA WA JESHI LA POLISI ZANZIBAR
March 15 2016 kituo cha ITV kiliripoti taarifa kutoka visiwani Zanzibar ambapo ilidaiwa kuwa na taarifa za watu wasiojulikana kurusha bomu nyumbani kwa Kamishna wa jeshi la polisi Visiwani Zanzibar eneo la Kijichi.
Sasa taarifa niliyoipata ni kwamba nyumba ya Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame imeripuliwa na kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu na watu wasiojulikana majira ya saa 5.00 usiku huko Kijichi nje kidogo ya mji wa Zanzibar.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Ofisini kwake Makao Makuu ya Polisi Kilimani, Kamishna Hamdani amesema tukio hilo limeathiri sehemu ya paa la nyumba na dari na kujeruhi baadhi ya watu waliokuwa wamelala na kusababisha hasara kubwa.
Amesema tukio hilo linafanana lile lililotokea tarehe 03 mwezi huu katika Maskani ya CCM Kisonge Unguja hivyo polisi inaendelea kufanya uchunguzi ikiwa ni pamoja na kuwasaka wahalifu wanaofanya uhalifu huo.
Akizungumzia matukio mengine ya uhalifu na kuchoma moto nyumba, maskani na kituo cha Afya huko Pemba, alisema Jeshi la Polisi limeanza msako mkali na kuwatia mbaroni watu 31 ambao wanaendelea kuhojiwa na watakaohusika watafikishwa katika vyombo vya sheria.
Kamishna Hamdani amewatoa hofu wananchi kuhusu usalama wao na mali zao kuelekea uchaguzi wa marudio utakaofanyika tarehe 20 mwezi huu na kuwepo kwa ongezeko la askari katika maeneo mengi ya mijini na vijijini ni moja ya juhudi za kuimarisha ulinzi na kuhakikisha uchaguzi huo utakuwa salama na amani.
Source:Full Shangwe
POLISI WAZUNGUMZA BOMU LILILORUSHWA KWENYE NYUMBA YA KAMISHINA WA JESHI LA POLISI ZANZIBAR
Reviewed by WANGOFIRA
on
09:16:00
Rating:
No comments: