TULITAKA MABADILIKO YA CHAMA AU MTU?
Na
Adrian Mgaya.
Waswahili
husema ukweli unauma, sikuwahi kuufikiria kwa umakini msemo huu,
lakini utendaji wa 'mwendokasi' rais Dkt John Pombe Magufuli
unanifanya nianze kuelewa kinagaubaga maana halisi ya msemo huu.
Wakati
wa kampeni za kujinadi kuamua nani ashike usukani wa kuliongoza taifa
kulikuwa na ahadi kemkem, nyingi zikileta matumaini kwa watanzania wa
hali ya chini, huku zikiwa tishio kwa waliozoea kutumia vibaya mali
za umma.
Tumeshuhudia
vyama vyote, vilivyokuwa na nia ya kungoza nchi hasa chama
tawala(CCM) na Chadema chini ya UKAWA, ACT wazalendo vilitoa ahadi
zilizotoa mwanga kumkwamua mtanzania, hata vile vyama vilivyoonekana
vidogo navyo havikuwa nyuma katika kumwahidi mtanzania hali nzuri.
Ni
wazi kwamba hali ya mambo Tanzania haikuwa shwari, na ndio maana
tukashuhudia majukwaa ya kisiasa yakiahidi neema kwa wananchi.
Si
Lowasa wala Magufuli au mama Anna Mghwira waliokuwa wakipendezwa na
hali ya mambo ilivyokuwa ikiendelea nchini, ahadi zao zilithibitisha
haya.
Wakati
wa kampeni, mkoani Tanga watanzania walimsikia Magufuli akiwaahidi
Tanzania yenye viwanda, huku akiahidi mabadiliko, moja ya maneno
alisema "Tanzania yetu inahitaji mabadiliko, na mabadiliko yawe
bora, sio bora mabadiliko..."
Maneno
hayo yalikosolewa na watu wengi, wakidai Magufuli ameiba maneno ya
mpinzani wake mkubwa kutoka ukawa, ambaye alipendwa na wengi kwa
kusisitiza mabadiliko.
Ilifikia
wakati tukaamini na kufurahishwa na hamasa za wanasiasa wetu, kuwa na
jicho la kuona mizizi iliyojikita ndani ya serikali, iliyohitaji
nguvu ya kweli isiyo na soni kuing'oa mizizi hiyo.
Swali
likaja ni nani ataleta mabadiliko ya kweli Tanzania?
Ni
kama panya waliokuwa wakijiuliza nani atamfunga paka kengele? Ni
busara na umakini wa hali ya juu uliofanywa na watanzania kuamua ni
nani aliongoze taifa lenye kiu ya mabadiliko.
Vijana
ambao wengi walikuwa na hamu ya mabadiliko hayo walihitaji elimu
kubwa kuamua nani anawafaa, katika moja ya makala nilizowahi kuandika
ilisomeka kwa kichwa "watanzania chagueni mnaemtaka"
ikatolewa na gazeti la Tanzania daima.
Makala
hiyo ilikuwa na lengo kuwataka watanzania wamchague kiongozi
atakaewafaa na sio kukaa vijiweni wakisubiri kubishana nani anawafaa
nani hawafai.
Wingi
wa wapiga kura waliojitokeza mwaka 2015 inathibitisha watanzania
walichoka na wanahitaji mabadiliko, kura zikapigwa, mshindi
akatangazwa.
Utendaji
ukaanza, Magufuli akiwa rais chini ya utawala wake nchi ikaanza
kunyooshwa na taratibu shilingi ikageuka, utumbuaji majipu ukiwaumbua
wale waliokuwa wakila keki ya taifa kwa uchoyo, huku ugumu wa maisha
ukiwa ni kwa watu wa hali ya chini.
Ukwepaji
kodi uliwahumiza wengi, nikiwa mmoja wa walioumizwa, sikuacha kutumia
kalamu yangu kuwakumbusha watawala, katika gazeti la majira la
disemba 15 2015, toleo na. 8011, yenye kichwa "Imetosha sasa
tusiruhusu mianya ya ukwepaji kodi"
Ujumbe
huo ulikuwa ni salamu tosha kwa rais Magufuli kumkumbusha moja ya
ahadi zake.
Utendaji
wa magufuli umetoa mwanga wa safari ndefu aliyonayo rais wetu, kuleta
yale mabadiliko yaliyokuwa yakiharibiwa na wanasiasa wakati wa
kampeni.
Ubanaji
wa matumizi katika serikali hii, ni moja ya mabadiliko yaliyokuwa
yakitajwa na Magufuli na sasa anatimiza.
Lakini
hofu imetawala mitaani, wengi wakidai shilingi 'imeadimika' na ugumu
wa maisha unaongezeka, tunapaswa tukumbuke kuwa subira yavuta heri,
wengine watasema ngoja ngoja yaumiza tumbo, lakini tukumbuke pia
haraka haraka haina baraka.
Tusubiri
'kheri' na 'baraka' katika kipindi hiki ambacho wafanyakazi hewa
wanaondosha, mapato ya kodi yanaongezeka huku neema ya viwanda ikija
Tanzania.
Rais
Magufuli anatakiwa asimamie maneno yake wakati wa kampeni, huku
watanzania tukiwa nyuma yake.
Kuna
maisha baada ya uchaguzi, na haya ndio maisha yenyewe sasa, siasa za
kujinadi ziachwe ulipoishia uchaguzi, na sasa ziendelee siasa za
kukumbushana.
Maisha
baada ya uchaguzi ni kuacha itikadi za vyama vyetu na kuwaunga mkono
viongozi waliopo madarakani wafanye kazi zao, tunachopaswa ni
kuwakumbusha tu pale wanapoenda tusipopataka.
Tuanze
kuelewa sasa Magufuli anaposema siasa marufuku, ni zile siasa za
kukwamisha utendaji kazi, tusipotoshe wala kupotoshwa juu ya kuacha
siasa katika kipindi hiki.
Ni
mabadiliko yapi ambayo watanzania tulikuwa tukiyatamani? Kubadilisha
chama, mtu au hali ya mambo ilivyokuwa ikiendeshwa na wachache
waliojilimbikizia mali kwa njia zisizo halali?
Ni
ukweli usiopingika, kiu ya wengi ilikuwa ni mabadiliko yaliyokuwa
yakihubiriwa na kina Lowasa na Magufuli.
Tuache
unafiki, hakuna aliyekuwa anapendezwa na wachache kujilimbikizia mali
ilhali mama wajawazito vijijini wanajifungua katika mazingira magumu,
huku watoto wetu wakichafua sare zao kwa kukaa katika madarasa yasiyo
na madawati wala sakafu.
Nchi
iliyokuwa imeoza kwa rushwa, haikutoa taswira nzuri kwa wageni
waliotutambua kwa amani na upendo tulionao.
Ni
aibu kila kona, unapogusa kuna jipu, safari bado ni ndefu rais wetu
watanzania wamekuamini, si wa upinzani wala chama chako, kazi kwako
kukata kiu ya walalahoi.
Ukweli
unauma, hasa pale ambapo ukweli huu unamuumbua asiyependa
kilichowekwa kweli, kusemwa kweli, lakini ukweli huo huo humweka mtu
huru, ahadi zako tamu kipindi cha kampeni usiache kuzitimiza hata
moja.
Mwandishi
wa makala haya ni mwanafunzi wa cho kikuu cha Dar es salaam
anapatikana kwa namba 0656110670 au barua pepe mgayaadrian@gmail.com
TULITAKA MABADILIKO YA CHAMA AU MTU?
Reviewed by WANGOFIRA
on
00:32:00
Rating:
No comments: