News Alert: Mwandishi wa Habari Mwanadada,Elizabeth Mayemba afariki dunia ghafla
TANZIA:
Mwandishi Mwandamizi wa Habari za michezo na burudani wa gazeti la
Majira, Elizabeth Mayemba amefariki dunia usiku wa leo baada ya kuanguka
ghafla nyumbani kwake eneo la Tabata kwa Swai jijini Dar es Salaam.
Taaifa
za awali zinaeleza kuwa, tukio hilo limetokea majira ya saa mbili usiku
huu wa Julai 9.2016,ambapp inaelezwa alikuwa akijisikia kizunguzungu na
ndipo alipopatwa na umauti huo licha ya kukimbizwa Hospitali.
Aidha,
Taarifa kutoka kwa mume wa marehemu, Eliza, Bwana Rogers amebainisha
kuwa…, alipigiwa simu saa mbili usiku na kuambiwa Eliza alisikia
kizunguzungu ghafla na kuanguka chini, alichukuliwa na kupelekwa
hospital baada muda mtu aliyempeleka Eliza hospital alimpigia tena na
kumpa taarifa za Eliza kufariki.
Taarifa nyingine zitatolewa baada ya ndugu wa marehemu kukutaana.
RIP Elizabeth Mayemba.
Blog hii ya WANGOFIRA inatoa pole kwa ndugu na jamaa wote popote pale walipo. Ni pigo kubwa katika tasnia ya Habari.
Marehemu Elizabeth Mayemba enzi za uhai wake..
Meneja
Mkuu wa Kampuni ya Business Times Limited, Aga Mbuguni, akimkabidhi
kombe la bandari Chalenji Meneja wa timu ya netiboli ya Business Times,
Elizabeth Mayemba (Enzi za Uhai wake) baada ya timu hiyo kushinda kombe
hilo. Jijini Dar es Salaam.
News Alert: Mwandishi wa Habari Mwanadada,Elizabeth Mayemba afariki dunia ghafla
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:18:00
Rating:
No comments: