ASSUMPTER MSHAMA AANZA KWA KASI YA MAGUFULI
NA Omary Mngindo, Kibaha
MKUU wa wilaya
ya Kibaha Mkoa wa Pwani Assumpter Mshama ameianza kazi yake kwa kasi ya
Rais Dkt. John Magufuli ya kuchapakazi papo kwa hapo huku akisema
Serikali hiyo imedhamilia kuwatumikia watu wa hali ya chini.
Mkuu huyo
amefanya mkutano wa kwanza kwa kukutana na wafanyabiashara wa soko Kuu
la Mailimoja ambapo alipokea kero malimbali ikiwemo ya Mwentekiti wa
soko hilo Ally Gongi kukaa madarakani kwa miaka minane huku akiwa pia
Mwenyekiti wa SACCOS iloyopo sokoni hapo ambapo wafanyabiashara hao
wamesema hatua hiyo inachangia kukwamisha maendeleo ya soko.
Katikakutaka
kuondokana na hali hiyo, wafanyabiashara hao walimtaja Mkuu huyo
awapatie ridhaa ili wafanye uchaguzi papo hapo ili waoate viongozi
wataoliongiza soko baada ya Mwenyekiti wao kukaa adarakani kwa miaka
minane pasiookuitisha uchaguzi, ambapo Mkuu huyo alisema jukumu hilo ni
lao na kama wataweza kufanya hivyo haba pingamizi katika kusimamia zoizi
hilo.
Baada ya kauli
hiyo ikafuatia hatua ya kuoendekeza majina ya watu watano kisha kupigiwa
kura kwa kunyoosha vidole ambapo Ramadhani Maulid alifanikiwa kushinda
kinyang'anyiro hicho hivyo kuchukua nafasi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa
awali Ally Gongi " Mzee wa Shamba".
Baada ya
kufanyika kwa zoezi hilo Mkuu huyo alifanya ziara ya kukagua soko ambapo
alijionea wafanyabiashara wa gari ndogo za kubeba mizigo na baadhi ya
wafanyabiashara wakufanyia shughuli zao chini ya Transfoma ya Umeme
hatua ambayo ni hatari kwa naisha yao.
Alipokuwa
anapita katika soko hilo nderemo, vifijo na vigeregere vilidikika kutoka
kwa akina mama huku wakisema wanaikubali Serikali ya awamu ya Tano
chini ya Rais Dkt. John Magufuli huku wakiuliza siku zote Mshsma alikuwa
wapi, kwa maana ya kuonesha kuridhishwa na kadi yake ya kazi.
"Serikali hiiya
awa u yaTano chuni ya Rais wetu Dkt. John Magufuli imedhamilia
kuwatumikiawananchi kwa kuwaondolea adha zinazowakabili, hivyo tupatie
ili ushirikiano ili tuchapekazi mkiyokuwa mnaihutaji," alimalizia
Mshama.
Pichanini
matukio tofauti ya ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani
Assumoter Mshama akiookuwa anazungumza na wafanyabiashara wa soko Kuu la
Mailimija mjini hapa. Nyingine akiwa anazungukia naeneo ya soko hilo.
ASSUMPTER MSHAMA AANZA KWA KASI YA MAGUFULI
Reviewed by WANGOFIRA
on
21:11:00
Rating:
No comments: