Wachungaji wa PPFT Waiomba Serikali Kufuta Usajili wa Kanisa la Askofu Gwajima
Askofu Josephat Gwajima |
Ushirika wa wachungaji wa Kanisa la
Kipentekoste Tanzania (PPFT) umeiomba serikali ifute usajili wa Kanisa
la Ufufuo wa uzima la Askofu Josephat Gwajima kwa kukiuka maadili ya
kanisa kwa kutoa kauli za uchochezi na kuzisambaza kwenye mitandao ya
kijamii.
Mwenyekiti
wa ushirika wa wachungaji hao Askofu Pius Ikongo mwenye makao yake
katika Halmashauri ya wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro amesema,kauli
hizo zinaweza kubadili fikra za wananchi na kuzaa chuki dhidi ya
serikali yao na kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani.
Askofu Ikongo ametoa tamko hilo katika taarifa yake kwa vyombo vya habari na kueleza kuwa kitendo kilichofanywa na Askofu Gwajima kinapaswa kulaaniwa na wapenda amani wote waliopo ndani na nje ya nchi.
Mwenyekiti huyo wa PPFT amesema, kosa kubwa ambalo limewaumiza wachungaji wa Kipentekoste ni kitendo cha Askofu Gwajima kutumia Kanisa kama jukwaa la kisiasa kwa kuleta uchonganishi kati ya serikali ya awamu ya nne na iliyopo madarakani.
Via>>ITV
Wachungaji wa PPFT Waiomba Serikali Kufuta Usajili wa Kanisa la Askofu Gwajima
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:39:00
Rating:
No comments: