UVCCM: Hakuna mwenye ubavu wa kuzuia mkutano wa CCM.
Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) umesema kuwa hakuna mtu au kundi la watu au taasisi yenye ubavu wala uthubutu wa kuuzuia au kuukwakisha kwa namna yoyote mkutano mkuu wa CCM unaoitarajiwa kufanyika Julai 23 mwaka huu .
Aidha umoja huo umesisisitiza kwamba mkutano huo utafanyika vile vile kama ilivyopangwa hivyo kuwataka *Bavicha* waache kupiga kelele hovyo na kutoa vitisho vya kitoto.
Msimamao huo umetangazwa jana na Kaimu katibu mkuu wa UVCCM *Shaka Hamdu Shaka* alipozungumza na baadhi ya wajumbe wa kamati ya utekelezaji UVCCM mkoa Iringa katika jengo la CCM akiwa njiani kuelekea Ihemi mkoani hapa.
Shaka alisema UVCCM wako tayari kuidhihirishia dunia kwa kuwatia adabu Bavicha ikiwa siku moja watajaribu kufanya jambo lolote linalotishia kuhatarisha usalama au ustawi wa maendeleo ya kisiasa ya CCM kwa saa, siku, wakati na mahali popote.
Alisema siku moja ikitokea Bavicha kutenda jambo lolote la hujuma au kudhuru, UVCCM haitaomba kibali au ruhusa ya viongozi wa juu wa CCM badala kitakachotokea dhidi yao ni matokeo mabaya ambayo yatakayongia katika vitabu vya historia ya kuogofya .
Alisema siku moja ikitokea Bavicha kutenda jambo lolote la hujuma au kudhuru, UVCCM haitaomba kibali au ruhusa ya viongozi wa juu wa CCM badala kitakachotokea dhidi yao ni matokeo mabaya ambayo yatakayongia katika vitabu vya historia ya kuogofya .
"Tunalaani tishio la kipuuzi la Bavicha , tunataka kuona jeuri yao, ubavu na misuli yao ili kuuuzuia mkutano maalum wa CCM Julai 23 mwaka huu, watakavyokuja sivyo watakavyorudi, wajaribu ili wakione kipurepure cha marombe siku watakapojaribu."alisema Shaka.
Tamko hilo la Shaka linafuatia kauli iliotolewa hivi karibuni na viongozi wa Bavicha wakitishia kufanya lolote ili kuhakikisha mkutano mkuu maalum wa CCM hautafanyika mkoani Dodoma mwezi ujao.
Aidha Kaimu huyo Katibu mkuu alisisitiza ikiwa Bavicha na Chadema wameshindwa kuendesha siasa za kiungwana zinazoheshimu na kufuata misingi ya kikatiba na kisheria , UVCCM haitashindwa kutia ndimi zake puani au kubadili kurasa za historia mwanana iliopo .
Shaka aliwataka Bavicha kuacha siasa za mikwara, vitisho, kutishia usalama na amani ya nchi kwa kuijifanya vijogoo wakati hawana lolote wanaloweza aidha kuzuia, kujenga au kubomoa .
Shaka alisema Bavicha lingekuwa Baraza makini, lenye vijana wa kisasa wenye maarifa, upeo na upembuzi wa kisiasa lingewakemea wabunge wanaosusia vikao vya bunge.
"Wasingekaa bila ya kuwaasa au kuwaonya wabunge wao wanaoshinda kwenye viwanja vya bunge wakipuuzia dhamana ya kuchaguliwa au kujua maana na mantiki ya misingi ya uwakilishi bungeni " alieleza
Alisema kukaa kimya kwa Bavicha bila kuonyesha na kutowaelekeza viongozi wao ni wazi Baraza hilo limefiisika, halina vijana wenye ujasiri, maamuzi wala weledi hivyo ni sawa na mbwa anayebweka nyakati za usiku akiwa hana meno ya kuuma .
Hata hivyo Shaka aliwataka makatibu wote wa makao makuu UVCCM na wilaya kuendelea na maandalizi ya kuwanoa kiitifaki *Green Guard* ambao watakuwa macho kwa kazi malum za kulinda mali za chama na usalama wa viongozi toka sasa hadi kumalizika kwa mkutano maalum Julai 23 mwaka huu .
Hapa ndipo utakapoona tafauti ya CCM na Vyama vingine.
"sisi ni chama cha Siasa wenzetu wana mashirika ya kisiasa lazima tuwaoneshe wananchi utofauti wetu endeleeni kujiandaa vizuri kimkakati ili tufanikishe mkutano mkuu wetu kwa mafanikio makubwa ili tuzidi kuidhihirishia dunia kuwa CCM ni chuo cha democrasia hakuna mwenye ubavu wa kuzuwia mkutano mkuu maalum Dodoma."
Huku akiongeza; "kama yuko anaetaka kuijaribu UVCCM tunamwambia ajaribu aone ifike pahala kuwe na kikomo paka hachewi sharubu kirahisi rahisi."
alionya shaka Hamdu.
alionya shaka Hamdu.
UVCCM: Hakuna mwenye ubavu wa kuzuia mkutano wa CCM.
Reviewed by WANGOFIRA
on
07:13:00
Rating: 5
No comments: