Mrema Aunga Mkono kauli ya Rais Magufuli ya kusitisha Mikutano ya siasa
Mwenyekiti
wa TLP taifa Dkt. Augustine Lyatonga Mrema amesema kwamba kitendo cha
Rais Dkt. John Magufuli kusema kwamba siasa ziachwe hadi miaka mitano
iishe kunatokana na tabia ya upinzani kugomea kila kitu bila kuweka
maslahi ya taifa mbele.
Dkt.
Mrema ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumzia kuhusu kauli hiyo ya
Rais na kama haitaviathiri vyama kikiwemo chama anachokiongoza cha TLP.
''Kwa
maoni yangu binafsi hii imetokana na tabia yetu sisi wapinzani kugomea
kila kitu hata mambo ambayo yana maslahi kwa taifa, kwa mfano ukiangalia
wakati Rais Dkt. John Magufuli anazindua bunge la bajeti wapinzani
walimgomea na kutoka nje, hapa walianza kumhukumu kabla hajaanza kazi''- Amesema Mrema.
Mrema
ameongeza kuwa hata bunge la bajeti linaloendelea wabunge wa upinzani
wametoka vikao karibu vyote wakati bajeti inayojadiliwa siyo ya Naibu
Spika ni bajeti ya serikali na kwamba wangetumia kanuni za bunge kuweza
kumuondoa kama hawamtaki kuliko kuacha kuwakilisha wananchi wao.
Aidha
Mrema ameenda mbali na kusema kuwa nchi hii haiwezekani kila siku ikawa
ni maandamano kwani wananchi wanatakiwa wafanye kazi na kama wapinzani
walikuwa na nia ya dhati wangebakia bungeni wajadili kwanza bajeti.
Kuhusu
chama chake pia kutofanya siasa Mrema amesema yeye hana maandamano ya
kila mara hivyo anaamini atakuwa na mikutano halali muda ukifika lakini
kwa sasa wananchi wafanye kazi kwanza.
Mrema Aunga Mkono kauli ya Rais Magufuli ya kusitisha Mikutano ya siasa
Reviewed by WANGOFIRA
on
21:58:00
Rating:
No comments: