MWANDISHI WA HABARI ALIYETEKWA APATIKANA
Mwandishi anayewakilisha kituo cha redio cha Sauti ya Ujerumani (Deutsche Welle) visiwani Zanzibar Salma Said na gazeti la Mwananchi aliyetekwa na watu wasiojulikana siku ya ijumaa wiki hii, amepatikana.
Kamanda wa polisi wa Dar es salaam Simon Siro amethibitisha kupatikana kwa mwanahabari huyo.
Mume wa Salma Said, Bw Ali Salim Khamis, ambaye amesema kwa sasa Salma yumo anatoa maelezo polisi Dar es Salaam.
Taarifa zaidi tutawaletea kadiri zinavyopatikana..
MWANDISHI WA HABARI ALIYETEKWA APATIKANA
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:31:00
Rating:
No comments: