DC MAKONDA ATOA WIKI MBILI UKARABATI BARABARA KINONDONI.
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mheshimiwa Paul Makonda akizungumza na waandishi wa Habari.(picha na Mtapa Wilson.)
Na, Mtapa Wilson,
picha kwa hisani ya Milard Ayo blog
“Halmashauri yetu ina magari ambayo yanweza kubeba vifusi ambavyo vinaweza kuwekwa katika mashimo yaliyojitokeza katika barabara zetu kutokana na mvua. Hii itasaidia angalau kurahisiha barabara zetu kupitika wakati serikali kupitia halmashauri ya Kinondoni ikijipanga kuziboresha zaidi.” Alisema Makonda.
Na, Mtapa Wilson,
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mheshimiwa
Paul Makonda amewapa wiki mbili watendaji wa halmashauri ya Kinondoni kuanza na
kumaliza ukarabati wa mashimo yaliyopo katika barabara zilizoko wilaya ya
Kinondoni.
Makonda ametoa agizo hilo mara baada ya
kutembelea barabara ya Mwananyamala hospitali, Makumbusho Stand mpaka Akachube
ambapo amewataka watendaji wa halmashauri kulekebisha maeneo ya barabara ambayo
yameharibika vibaya kutokana na mvua.
picha kwa hisani ya Milard Ayo blog
“Halmashauri yetu ina magari ambayo yanweza kubeba vifusi ambavyo vinaweza kuwekwa katika mashimo yaliyojitokeza katika barabara zetu kutokana na mvua. Hii itasaidia angalau kurahisiha barabara zetu kupitika wakati serikali kupitia halmashauri ya Kinondoni ikijipanga kuziboresha zaidi.” Alisema Makonda.
Aidha Makonda alipata fursa ya kuongea na madereva daladala ili kuona zoezi la kubeba walimu bure linavyoendelea ambapo wamemhakikishia kuendelea nalo vizuri kama alivyoagiza..
DC MAKONDA ATOA WIKI MBILI UKARABATI BARABARA KINONDONI.
Reviewed by WANGOFIRA
on
08:58:00
Rating:
No comments: