CHAMA CHA WAFANYAKAZI WA TAASISI YA ELIMU YA JUU (THTU) CHATOA MSAADA HOSPITALI YA SINZA PALESTINA.
Kaimu mganga mkuu Hospitali ya Sinza Palestina,Dr. Kayola (kushoto) akipokea msaada kutoka kwa Mwenyekiti wa THTU Bwana Salifius G. Mligo( mwenye koti). picha na Perus Benson
Na, Mtapa Wilson
Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za
Elimu ya Juu (THTU) tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Mlimani wametoa msaada wa vifaa mbalimbali katika Hospitali ya Sinza Palestina
kitengo cha wodi ya wazazi wenye gharama ya shilingi 2.5 kama sehemu ya
kuzingatia umuhimu na mchango wa mwanawake katika taifa na kuadhimisha siku ya
wanawake duniani.
Akizungumza na waandishi wa habari mara
baada ya kukabidhi msaada huo.
Mwenyekiti tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tawi la Mlimani, bwana
Salifius G. Mligo amesema kuwa kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakumba
wahudumu wa sekta ya afya nchini na wanawake wakati wa kujifungua, THTU imeamua
kutoa msaada huo ili kupunguza matatizo hayo
“Tumeziona juhudi za Viongozi wa Mikoa
na Wilaya katika kuunga juhudi za Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli katika
kuboresha huduma za afya katika vituo vya afya, zahanati na hospitali. Na sisi kama THTU tumefanya haya kama sehemu
ya kuunga juhudi hizo”
Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu
hospitali ya Sinza Palestina, Dk. Crispin Kayola amewashukuru THTU kwa msaada
walioutoa kwani imesaidia kuongeza baadhi ya vifaa ambavyo hupungua kulingana
na idadi kubwa ya kina mama wanaojifungua hospitalini hapo.
“Kwa wastani hospitali ya Sinza
Palestina huzalisha mpaka kina mama 40.
Msaada huu walioutoa THTU utasaidia angalau upungufu wa vifaa vya
kujifungulia uliokuwepo awali kama vile mipira (gloves)” Alisema Dk. Kayola.
Nae Elina Sisian, ambae ni mzazi
ameziomba taasisi na mashirika mbalimbali kutoa msaada katika vituo vya afya
kwani bado kuna changamoto nyingi zinazowakabili kina mama wakati wa kujifungua
katika vituo vya afya.
“bado tunakabiliwa na changamoto nyingi
ikiwemo upungufu wa vitanda na wodi kwa ajili ya kujifungulia. Tunaomba taasisi, mashirika na serikali kwa
ujumla wasaidie katika hilo.” Alisema
Elina.
CHAMA CHA WAFANYAKAZI WA TAASISI YA ELIMU YA JUU (THTU) CHATOA MSAADA HOSPITALI YA SINZA PALESTINA.
Reviewed by WANGOFIRA
on
08:27:00
Rating:
No comments: