Home
Unlabelled
Jinsi ya kutawala mafanikio yako -
Jinsi ya kutawala mafanikio yako -
Kwa ufupi
Hatua ya pili, nikaelezea jinsi ya kuimarisha kumbukumbu, ikiwa ni moja ya mambo muhimu katika kuharakisha maendeleo ya haraka katika mpango kazi. Hatua ya tatu ikawa ni jinsi ya kupangilia mambo. Hapa nikaonyesha ni namna gani jambo likifanyika hatua kwa hatua linavyoimarisha msingi mzuri wa mafanikio.
Kwa muda mrefu nimezungumzia juu ya namna ya kupata mafanikio. Nilianza kwa kueleza namna mtu anavyoweza kutumia muda vizuri ili kupata mafanikio. Hapa nikasisitiza juu ya kuwa mshindi au bingwa wa kutumia muda na siyo kusema; ‘muda si rafiki.’
Hatua ya pili, nikaelezea jinsi ya kuimarisha kumbukumbu, ikiwa ni moja ya mambo muhimu katika kuharakisha maendeleo ya haraka katika mpango kazi. Hatua ya tatu ikawa ni jinsi ya kupangilia mambo. Hapa nikaonyesha ni namna gani jambo likifanyika hatua kwa hatua linavyoimarisha msingi mzuri wa mafanikio.
Sikuishia hapo, niliendelea kuchambua mbinu za kuelekea kwenye mafanikio kwa kutazama jinsi fikra makini zinavyomwezesha mtu kuyaendea mafanikio. Hapa, nikaelimisha jinsi ya kutekeleza mkakati huo kwa kufanya tafakari inayochambua shughuli zako na jinsi ya kuzitekeleza kwa usahihi.
Kwa kuwa nimeelezea juu ya mipango kuelekea kwenye mafanikio naamini msomaji uliyekuwa na kiu ya mafanikio, umekuwa na mwelekeo sasa. Kwa siku ya leo, hebu tuchukulie sasa tayari una mafanikio.
Je, unajua namna ya kusimamia mafanikio ili usirudi nyuma? Hili ni jambo la muhimu kwa sababu limewafanya wengi kuingia kwenye matatizo. Ni moja ya mambo ambayo yamewafanya watu wengi kukata tamaa, kuwa na msongo wa mawazo, kuugua shinikizo la damu, kiharusi na hata kisukari.
Maana kila wakikumbuka jinsi walivyo kuwa na mafanikio waliyoyatengeneza kwa muda mrefu na jinsi walivyoanguka ghafla na pengine kufilisika kabisa, wanachanganyikiwa.
Kwa kawaida mtu aliyezoea kuishi maisha ya juu kwa muda mrefu inakuwa ni vigumu kuyakubali maisha ya chini. Ni vizuri nikakusimulia kisa hiki cha mwanariadha pengine waweza kunieleza zaidi.
Miaka ya tisini, katika mashindano ya riadha mjini London, raundi ya mwisho, jamaa mmoja alikuwa anaongoza mbio muda mrefu na kweli alikuwa kawaacha wenzake mbali.
Ilikuwa imebaki mita ishirini kukaribia mstari wa mwisho. Jamaa alianza kushangilia ushindi na kuwapungia mashabiki mikono. Ikiwa ni mita tano kumaliza huku akiwa mwingi wa furaha, walitokea wanariadha wengi kwa kasi kubwa na kumpita.
Kwa kuwa wenzake walikuwa na kasi ya ajabu, alijikuta akimaliza akiwa mshindi wa tano. Hakika ilikuwa huzuni kwake, baada ya kupoteza mwelekeo dakika za mwisho. Hii ina mantiki kubwa katika maisha yetu ya biashara.
Muda mrefu umepigania biashara yako ndogo hadi ilipo na kupanda hatua ya juu. Umepanga, umetangaza, umeuza na umefanya mazungumzo ya kibiashara na wengi. Umetumia muda mwingi kwa kazi, mapumziko kidogo sana. ghafla unaanguka. Mtu atajiuliza; ni kwa nini?
Wenye mafanikio wanapaswa kujiuliza; je, nina malengo juu ya mafanikio yangu? Mafanikio huambatana na matatizo chungu nzima ya kibiashara. Vilevile, kazi chungu nzima za kuandika na kumaliza kwa muda mfupi, ongezeko la wateja na kadhalika.
Kama umefanikiwa au unaelekea kwenye njia ya mafanikio sasa, hapa nimejaribu kuweka dondoo za jinsi ya kutawala mafanikio yako kwa busara zaidi. Hapa nitachambua mambo 11.
Moja, Sheherekea mafanikio yako. Yawe madogo au makubwa, yanatakiwa yasherehekewe. Haijalishi umetangaza kwa umma au umealika marafiki wachache na kuwashirikisha. Kusherehekea mafanikio ndiyo msingi wa kufanya kwa mafanikio mengine makubwa zaidi. Dunia ina jinsi na sisi tuna jinsi ya kuwasiliana na dunia kiasilia.
Pili, Usifiche hisia zako za kweli kuhusu hayo mafanikio. Usijituhumu na kusema ulikuwa hustahili hayo mafanikio. Badala yake jieleze ulikuwa unastahili mafanikio hayo madogo au makubwa kwa kuwa uliyahangaikia na kuyafanyia kazi na hiyo siyo bahati.
Wengi hupenda kujihami juu ya mafanikio waliyopata kwa kusema ilikuwa bahati lakini wanasahau kuwa nguvu ya akili iliyofichika, utendaji wake na kufanyia kazi mikakati kwa akili iliyo makini ambayo ni asilimia 10 ya akili yote ya mwanadamu.
Tatu, weka dhamira ya kuhitaji zaidi ya hapo usiridhike: Hatua ya mafanikio uliyofikia ndogo ya mafanikio, usione umefika mwisho na kushindwa kuweka juhudi zaidi. Ng’ang’ania na fuatilia ndoto na malengo yako ya kukua kibiashara. Fuatilia pia maisha yako ambayo kila siku unayatafuta. Chukua muda wa kujifunza mambo mengine mapya kuhusu kiwanda ambacho upo (sekta) au jifunze biashara mpya ambayo itakunufaisha baadaye.
Jifunze kutoka katika mafanikio yako. Kama tunavyoambiwa tujifunze kupitia makosa yetu, chukua muda kujifunza katika mafanikio yako. Kipi sahihi ulifanya mpaka kikakufanya uwe hapo leo? Ni kwa kiwango au sehemu gani ya hayo mafanikio yamekufanya uwe na furaha?
Wiki ijayo nitakamilisha kwa kufafanua juu ya mambo mengine manane ya kudumisha mafanikio.
Jinsi ya kutawala mafanikio yako -
Reviewed by WANGOFIRA
on
03:02:00
Rating: 5
No comments: