Mwaka Mmoja Wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Leo na mimi nipaze sauti yangu imfikie Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli kwa Mafanikio Makubwa
aliyoyapata ktk kipindi cha Mwaka mmoja wa utawala wake tangu aingie madarakani
mnano Novemba 05, 2015.
Rais Magufuli kwa kiasi kikubwa amerudisha nidhamu
kwa watumishi wa umma. Leo ofisi nyingi za utumishi wa umma zina nidhamu ya
hali ya juu sana, watu wanatambua vizuri nini wanapaswa kufanya na nini
hawapaswi kufanya ktk Utumishi wao. Huduma zenye kukidhi matakwa ya wananchi
zimerejea.
Rais Magufuli amefanikiwa kwa kiasi
kikubwa kudhibiti matumizi ya fedha za Serikali kwa kuzuia na kufuta
matumizi yasiyokuwa ya lazima kama safari za nje ambapo ktk kila safari kwa
sasa ni lazima Ikulu ibariki kwa kutoa Kibali na kuruhusu idadi ndogo tu ya
watu na mara nyingine mabalozi kuiwakilisha Tanzania, kuondoa posho zisizo za
lazima n.k
Rais Magufuli alielekeza fedha mbalimbali
ambazo zilitengwa kwa matumizi Maalum Mfano Fedha kwa ajili ya Semina kwa
Baraza la Mawaziri, Fedha kwa ajili Sherehe ya Kitaifa ya Maadhimisho ya Uhuru
- 09 Desemba 2015 n.k Mh. Rais alielekeza zikafanye Shughuli za
Kimaendeleo ikiwemo kununua Vitanda vya Hospitali ya Taifa Muhimbili na
kutengeneza Madawati kwa ajili ya Shule za msingi ili kuboresha Elimu.
Rais Magufuli alituahidi endapo
atachaguliwa Elimu ya msingi na Sekondari itakuwa ni BURE ambapo
ametimiza sasa Elimu kwa Shule za Msingi na Sekondari ni BURE kabisa.
Rais Magufuli aliahidi atafufua Shirika la Serikali
la Ndege la ATCL kwa kununua Ndege Mpya ambapo tayari Mheshimiwa Rais ametimiza
Ahadi yake kwa Kununua Ndege Mbili Mpya na leo ameahidi kutuletea Ndege
Kubwa aina ya Boeing yenye uwezo wa Kubeba abiria zaidi ya 240 ili kukuza
uchumi wa Nchi kupitia Sekta ya Utalii.
Rais Magufuli amefanikiwa kusimamia ipasavyo
Ukusanyaji wa Mapato ya serikali na Kudhibiti Matumizi yake. Hongera pia
Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kumsaidia Mheshimiwa Rais ktk hili.
Rais Magufuli alituahidi kupambana na Ufisadi na
Kuendeleza Vita dhidi ya Wala Rushwa kwa Kuanzisha Mahakama ya Kushughulikia
Ufisadi na Rushwa na tayari mahakama ya Kushughulikia Ufisadi & Rushwa
inaishi na leo naamini imesikiliza Kesi moja.
Rais Magufuli ameendelea kuboresha barabara kwa
Kukijenga kwa Kiwango cha lami mfano kama ile ya Mwenge Dar es Salaam &
Mwanza.
Mheshimiwa Rais aliahidi kuhamishia Serikali yake
Makao Makuu ya Tanzania Mjini Dodoma na tayari amekwisha anza kutekeleza kwa
kuhamisha Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara mbalimbali.
Rais Magufuli aliahidi kukuza Uchumi wa Nchi yetu
kwa kuifanya Tanzania ya Viwanda na wote tumeshuhudia Juhudi za Mheshimiwa Rais
za Kutafuta wawekezaji kutoka Mataifa mbalimbali duniani ili yawekeze nchini.
Ndugu zangu yako Mengi sana aliyofanya Rais
Magufuli mwenye macho haambiwi tazama ila naomba niishie hapo.
Ijapokuwa Bado Changamoto ni nyingi na watu wataona Maisha yamekuwa magumu
lakini tutambue na kuelewa hali hiyo haina budi kuja kwani Nchi iko
katika kipindi cha Mabadiriko ya kiuchumi kitaalamu tunaita " TRANSITION
PERIOD " ambapo kutokana na Juhudi za Mheshimiwa Rais kuujenga uchumi wa
Nchi yetu ni lazima mwanzoni tutaona Mabadiriko fulani fulani hivyo Watanzania
wenzangu tuvute subira kwa maisha Mazuri yaja. Tumpe nafasi Mh. Rais apambane
kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi yetu na sisi kwa nafasi zetu tumpe ushirikiano
wa kutosha kwa kufanya kazi kwa Bidii sana.
Ama Kwa Hakika Rais wetu anastahili pongezi nyingi
sana na Mimi Robert PJN Kaseko Mjumbe Baraza Kuu UVCCM Mkoa wa Arusha nichukue
nafasi hii kukupongeza Rais wangu na Mwenyekiti wangu CCM Taifa Mh. DKT. John
Pombe Magufuli kwa kutuletea Maendeleo makubwa na Mabadiriko ya kweli kwa
kipindi cha Mwaka mmoja tunashirikiana toka tukuchague utuongoze,
Mabadiriko ambayo kiukweli sisi Wananchi wa Tanzania tulisubiri kwa Muda
mrefu sana na nizidi kukutia moyo Mh. Rais usirudi nyuma endelea mbele
tunatambua vikwazo ni vingi na Kazi ni ngumu lakini namuomba Mwenyezi Mungu
azidi kukutia nguvu, akupe afya njema na ulinzi wake ili uendelee vyema
kuwaletea Maendeleo Wananchi wako maana wewe ni Mchapa Kazi Kwelikweli
tunakufahamu vizuri. HAPA KAZI TU. CCM Hoyeeeeeee.
Robert PJN Kaseko
Mjumbe Baraza Kuu UVCCM Mkoa wa Arusha
November 04, 2016.
Mwaka Mmoja Wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:27:00
Rating:
No comments: