Maghembe: Tanzania Haitegemei Kenya Kupanga Kodi Zake
Wakati Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amesema Tanzania haitegemei
Kenya kupanga kodi kwa maendeleo ya wananchi, amebainisha kuwa Serikali
inafuatilia taarifa kuwa baadhi ya mawakala wa utalii nchini, wanafungua
akaunti nchini humo kukwepa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).
Profesa
Maghembe alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki kufuatia malalamiko ya
mawakala wa Utalii wanaodai hatua ya Serikali kutoza VAT kwenye utalii
kutaathiri sekta hiyo.
Mawakala hao wamekaririwa na vyombo vya habari
vya ndani na nje ya nchi, wakidai watalii wengi wamesitisha safari zao
na wengi wameamua kwenda Kenya kwa vile nchi hiyo imeondoa VAT.
Taarifa
hizo zilidai hatua hiyo ya Serikali imesababisha watalii 8,000 kusitisha
safari zao na kufanya Tanzania kupoteza mapato ya Sh13 bilioni.
Mtendaji Mkuu wa chama cha mawakala wa Utalii Tanzania (Tato), Cyril Arko alisema wanachama wao walishapokea maombi ya safari (bookings) mwaka mzima nyuma na wengine kulipwa kabisa, hivyo ni vigumu kurudi kumwambia mteja kuwa kuna mabadiliko, ndio sababu wakaenda Kenya.
Mtendaji Mkuu wa chama cha mawakala wa Utalii Tanzania (Tato), Cyril Arko alisema wanachama wao walishapokea maombi ya safari (bookings) mwaka mzima nyuma na wengine kulipwa kabisa, hivyo ni vigumu kurudi kumwambia mteja kuwa kuna mabadiliko, ndio sababu wakaenda Kenya.
Arko
alisema watalii wameamua kwenda Kenya kwa sababu nyumbu ni wale wale
wanaotoka Serengeti na kuingia Masai Mara, Kenya, lakini faida ya Kenya
ni kwamba hakuna kodi ya VAT.
Kauli ya Profesa Maghembe
Akijibu
malalamiko hayo, Waziri Maghembe alisema Tanzania si koloni la Kenya,
kwamba kila mipango yake ya maendeleo itegemee taifa hilo.
“Kenya siyo
sehemu ya Tanzania na sisi (Tanzania) si koloni la Kenya. Kenya ni
nchi tofauti, Uganda ni nchi tofauti, Uingereza ni
nchi tofauti,” alisema Profesa Maghembe na kuongeza;“Hizi ni kodi ndani
ya Tanzania. Kenya ina mazingira tofauti kabisa na Tanzania. Hatuwezi
kupanga kodi kwa maendeleo ya nchi yetu tukiwatazama wao,” alisema.
Kwa
mujibu wa Profesa Maghembe, katika kipindi cha miaka minne
mfululizo, idadi ya watalii wanaotembelea Kenya imeendelea kupungua
kutoka milioni mbili hadi milioni 1.3 mwaka jana.
“Na katika kipindi
hicho huku kwetu wamekuwa wakiongezeka kutoka 800,000 hadi 1.2 milioni,”
alisema.
“Kule (Kenya) wana sababu ya kuondoa VAT ili waone kama watavutia
watalii wasiendelee kupungua. Hapa tulikuwa hatuna kodi hata siku moja.
Hili jambo linapotoshwa sana,” alisisitiza.
Profesa Maghembe alisema
kinachoonekana ni kama kuna propaganda na mgomo baridi kutoka kwa baadhi
ya mawakala wanaotaka kuihadaa dunia ili ione Tanzania kutoza VAT ni
tatizo.
Hata hivyo alisema Serikali inafuatilia kuangalia mwenendo kwa
mwezi mmoja, miezi miwili ili kuona hali inakwendaje na baada ya
kufanya tathmini ya kina, Serikali itatoa taarifa kwa umma.
Alitolea
mfano kuwa kuingia hifadhi ya Arusha ni Dola 45 za Marekani na
Serikali ikitoza asilimia 18 ya VAT, ada ya kuingia katika hifadhi hiyo
kwa siku inakuwa Dola 53.10, ambayo bado ni ndogo.
“Sasa kusema kati ya
Dola 45 na Dola 53 basi itafanya mtalii kutoka Marekani asije Tanzania
hii ni dhana ngumu kuelewa. Serikali itafuatilia jambo hilo kwa kina,”
alisema Waziri.
Maghembe: Tanzania Haitegemei Kenya Kupanga Kodi Zake
Reviewed by WANGOFIRA
on
21:47:00
Rating:
No comments: