Papa: Kuwatumikisha watoto ni utumwa mamboleo
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani amesema kuwa kitendo cha kuwatumikisha watoto kama vibarua ni utumwa mamboleo.
Papa Francis ameitaka jamii ya kimataifa kutokomeza vanzo vya
utumikishaji watoto kama vibarua katika maeneo mbalimbali duniani na
kukitaja kitendo hicho kuwa ni utumwa mamboleo. Amesema jitihada kubwa
zinapaswa kufanywa ili kutokomeza suala hilo.
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani ameongeza kuwa walimwengu wanapasa
kufanya juhudi kubwa ili kutokomeza utumwa huo. Papa Francis amesema
kuwa mamilioni ya watoto katika pembe mbalimbali duniani wanakosa haki
zao za kimsingi na wanakabiliwa na hatari kubwa.
Papa: Kuwatumikisha watoto ni utumwa mamboleo
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:41:00
Rating:
No comments: