MWANAMKE USIPOTHAMINI MTOTO, HAKUNA ATAKEYEMTHAMINI
.
na Baraka ngofira
( picha za watoto waliofanyiwa vitendo vya kikatili. picha kwa Hisani ya IIP MEDIA)
Mwanamke ni mama wa familia, na kiimani amebeba uponyoji wa mwanaume kwa kuwa ametokana na ubavu wa mwanaume. Hivyo mwanaume amebeba vidonda kwa ajili ya mwanamke na kwa sababu hiyo basi wawili huishi pamoja kwa kushirikiana katika kutekeleza majukumu mbalimbal
i.
( picha za watoto waliofanyiwa vitendo vya kikatili. picha kwa Hisani ya IIP MEDIA)
Mwanamke ni mama wa familia, na kiimani amebeba uponyoji wa mwanaume kwa kuwa ametokana na ubavu wa mwanaume. Hivyo mwanaume amebeba vidonda kwa ajili ya mwanamke na kwa sababu hiyo basi wawili huishi pamoja kwa kushirikiana katika kutekeleza majukumu mbalimbal
i.
Ukiachilia mbali nafasi mbalimbali ambazo baadhi ya waandishi wa kazi za
kifasihi kumwandika na kumchora mwanamke katika mitazamo hasi, lakini bado
mwanamke atabaki kuwa, ni jasiri kwani
naamini kuwa kama ingekuwa mimba ina zamu ya kulea na kuibeba, sina shaka kuwa
wanaume wengi wasingekubali kukaa nayo hata kwa siku moja. Na hivyo ingemlazimu
mama kuibeba tena mpaka atakapojifungua. Na hapo kidogo ndipo mwanamme
angejifunza thamani ya kubeba mimba na kuilea kwa muda wote wa miezi tisa mpaka
kuijifungua na kuendeleza malezi ya mtoto wake.
Pia, ni mchapakazi, mchumi, mwalimu yaani waswahili wanasema katika kila
sekta yuko vizuri. Na kama hauamini angalia wanawake wengi wakienda kufanya
manunuzi sokoni, wanavyopiga bajeti ili pesa aliyopewa hata kama ni kidogo
itoshe kununua mahitaji na ikiwezekana ibaki walau salio kidogo la kuanzia
kesho au akanunue vocha.
Huyu ndiye mwanamke ambaye baadhi ya wanaume umdharau bila kugeuka nyuma
na kuangalia upande wa pili wa sarafu, kwa haya anapaswa pongezi kubwa kwani si
jambo la kawaida kwa shughuli anazozifanya.
Ukienda kijijini utamkuta mwanamke kabeba mtoto mgongoni, ndoo ya maji
kichwani, bado kuni juu ya ndoo ya maji, jembe mkononi na mengine kibao. Huku mme
wake akitembea tena kwa ujasiri kabisa na jembe lake moja bila hata wasiwasi
wowote. Na mara tu wafikapo nyumbani bado mwanamke huyu huyu anashughulika na
kuwasha moto wa kuni au mkaa ili aandae chakula cha familia huku baba akiwa
amestarehe kabisa. Na pengine akimfokea mwanamama huyu kwa nini chakula hakiivi
haraka.
Lakini pamoja na kuwa na sifa zote hizo baadhi yao siku hizi wamegeuka
na kuwa zaidi ya simba au chui kwa vitendo ambavyo vimekuwa vikilipotiwa na
vyombo vya habari na matukio mengine kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii.
Siku hizi imekuwa ni kawaida sana kusikia mtoto kawekwa kwenye jokofu na
wengine kubanikwa kwenye “oven” na baadhi ya wadada wa kazi, mara utasikia
mtoto kachomwa na pasi ya umeme eti kisa kaiba shilingi mia tano. Hii inasikitisha
sana kwa watu ambao jamii inawaamini lakini kwa sasa imani imeanza kupungua kwa
wadada hawa wa kazi.
Ukiachilia mbali wadada wa kazi wapo baadhi ya wakina mama ambao naweza
kusema hawaujui uchungu na pia naweza kusema kwao watoto ni kama waliwaokota tu
na hawakuingia kwenye chumba cha kujifungulia maarufu kama leba. Kwani karibu
kila mwezi utasikia mtoto katupwa mtaroni au karibu na jaa la taka. Na hapa
ndipo najawa na wasiwasi kama huyu mtu aliyefanya kitendo hiki ana akili timamu
au kidogo waswahili usema zimempita kushoto.
Hii inasikitisha sana na huleta hisia kali mkiongoni mwa wanajamii na
baadhi ya mashirika ya kutetea haki za kibinadamu na watoto kuhusu ukatili huu
wanaofanyiwa. Labda kidogo niwakumbushe
video ambayo ilikuwa maarufu sana mwishoni mwa mwaka 2014, ambayo ilikuwa
ikimwonyesha mfanyakazi wa ndani huko
nchini Uganda alivyokuwa akimpiga mtoto ambacho kwangu naweza sema ni kipigo
kitakatifu. Ilikuwa ni video ya kusikitisha na baada ya maamuzi ya mahakama ya
kumfunga miaka mitatu jela lakini bado wanaharakati wa haki xza watoto bado
hawajaridhika na adhabu hiyo.
Na hapo ndipo usemi usemao uchungu wa mwana haujuaye mama lakini cha
ajabu baadhi ya mama hawaujui kiukweli uchungu
na thamani ya mtoto au watoto wao. Chonde chonde dada zangu mtatia aibu
na heshima na thamani yenu inashuka kwani hakuna mwanaume yeyote anayependa
kuwa na mwanamke katili, kwani wengi wao wafanyao vitendo hivi ni wale hata
bado kwenye ndoa hawajaingia.
Namalizia kwa msemo mmoja wa Kiswahili usemao “ Usipoziba Ufa utajenga
ukuta” na “ Mchelea mwana hulia mwenyewe” kwa maana uchungu wa mwana aujuaye
mama hivyo Napata ujasiri wa kusema kama mama asipothamini uchungu wake kwa
mwanaye hakuna atakaye weza kuthamini na kamwe baba hatojali mtoto kama mama
ukishindwa kumtunza mwanao.
MWANAMKE USIPOTHAMINI MTOTO, HAKUNA ATAKEYEMTHAMINI
Reviewed by WANGOFIRA
on
23:19:00
Rating:
No comments: