WINNIE MANDELA AIBIWA BILION 13
Aliyekuwa mke wa Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Winnie Mandela ameibiwa dola 6000 (Sh 13milioni) nyumbani kwake. Polisi nchini Afrika kusini wanasema wanachunguza tukio hilo.
Msemaji wa polisi amesema kuwa hawajamkamata mshukiwa yeyote lakini wanaendelea na uchunguzi.
Mtandao wa News24 ulisema kuwa Winnie Mandela aligundua kuwa dola 6,000 ambazo alikuwa amepewa kama zawadi wakati ya sherehe ya siku ya kuzaliwa kwake zilikuwa zimetoweka
Mtandao huo unasema aligundua kuwa hazikuwepo wakati alienda kutafuta pesa kumtuma mtu anunue mkate.
WINNIE MANDELA AIBIWA BILION 13
Reviewed by WANGOFIRA
on
07:58:00
Rating:
No comments: