AUAWA KWA KUCHOMWA KISU BAADA YA KUFUMANIWA NA MKE WA MTU
Mtu mmoja anayejulikana kwa jina la Idd
Selemani, (40), Mkazi wa Jineri katika Manispaa ya Singida ameuwa kwa
kuchomwa na kisu sehemu mbalimbali za mwili wake na Mtuhumiwa aitwaye
Khalid Rajabu, (45), fundi viatu na Mkazi wa Jineri baada ya mtuhumiwa
huyo kumkuta akiwa na mke wake chumbani kwake.
Akiongea na waandishi wa habari ofisini
kwake leo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida SSP Isaya Mbughi
amesema tukio hilo limetokea jana majira ya saa majira ya saa 9:30
alasiri.
Ameeleza kuwa mbinu
aliyoitumia mtuhumiwa kufanya tukio hilo kuwa ni kumvizia marehemu
akiwa na mke wa mtuhumiwa aitwaye Mariam Ibrahimu, (25) mkazi wa Jineri
wakiwa chumbani kwa mtuhumiwa ambapo mtuhumiwa huyo aliingia chumbani
kwake kisha kufunga mlango na kuanza kumshambulia Marehemu na
kumsababishia majeraha kisha kufariki muda mfupi wakati akipelekwa
Hospitali ya Mkoa Singida.
Amesema chanzo cha mauaji hayo kuwa ni wivu wa kimapenzi.
Jeshi la Polisi linawashikilia
watuhumiwa Khalid Rajabu na mke wake kwa mahojiano na baada ya
mahojiano kukamilika watuhumiwa watafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma
zinazowakabili.
Kaimu Kamanda ametoa wito kwa Wananchi
wote kwa kuwataka kuacha kujichukulia sheria mkononi bali watoe taarifa
vituo vya Polisi pindi wanapopata migogoro yenye utata ili kuchukua
hatua za kisheria na kuongeza kuwa wazazi/wanandoa wanatakiwa kuwa
waaminifu katika ndoa zao ili kuepusha migogoro inayoweza kuleta athari.
Chanzo-MACHIBYA blog
AUAWA KWA KUCHOMWA KISU BAADA YA KUFUMANIWA NA MKE WA MTU
Reviewed by WANGOFIRA
on
22:12:00
Rating:
No comments: