KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO SHINYANGA LAKARABATI JENGO LA WAZEE KITUO CHA KOLANDOTO

Kanisa la Waadventista Wasabato mjini Shinyanga kupitia idara ya vijana limekarabati jengo moja lenye vyumba sita katika kambi ya kulelea Wazee Kolandoto katika manispaa ya Shinyanga baada ya kufika katika kituo hicho na kujionea changamoto ya ubovu wa majengo ambayo ni hatari kwa maisha ya wazee hao ambao sasa wapo 18.

Akizungumza wakati wa kukabidhi jengo hilo leo Jumamosi June 24,2017,Mratibu wa Idara ya Vijana Kanisa Waadventista Wasabato Kanda ya Shinyanga Wilson Mjinja alisema jengo hilo lilikarabatiwa kuanzia Mwaka 2016 hadi 2017 kwa gharama ya shilingi milioni 1.8 ambapo vijana wa kanisa hilo walishiriki kwenye ukarabati ili kupunguza gharama za ukarabati. 

Akipokea jengo hilo kwa niaba ya serikali ,Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amelilipongeza kanisa hilo kwa moyo waliouonyesha kukarabati jengo hilo kutokana na wazee hao kukabiliwa na ubovu wa majengo ambayo ni hatari kwa maisha ya wazee hao. 

Matiro alitoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kujitokeza kuwatatulia changamoto mbalimbali zinazowakabili wazee hao ikiwamo na kukarabati majengo mengine yaliyosalia ili waishi mahali salama. 

Naye Askofu Kanisa la Wasabato Jimbo Kuu Kaskazini Mwa Tanzania, Dk. Godwin Yakundaya alisema dini safi ni ile ya kusaidia watu wenye uhitaji na siyo kuwa na majengo mazuri na vyombo vizuri vya muziki bali ni kusaidia pia watu ambao wanaishi maisha magumu. 

Dk. Yakundaya alisema dhana ya dini safi ndiyo sababu iliyowapelekea kuguswa kuwasaidia wazee hao kwa kuwakarabatia majengo ili waishi mahali salama na kubainisha kuwa huo ni mwanzo tu wataendelea kutoa huduma kwa wazee hao zaidi. 

Mbali na kanisa hilo kukabidhi jengo walilokarabati kwenye kambi hiyo ya wazee pia wametoa zawadi ya chakula ambayo ni mchele kilo 120, Mbuzi mmoja,mafuta ya kupikia,boksi la sabuni la kufulia pamoja na vitabu vya kidini kwa ajili ya kusoma neno la Mungu.
Askofu wa kanisa la Wasabato jimbo Kuu Kaskazini mwa Tanzania Dk. Godwin Yakundaya akisoma neno la Mungu katika kambi ya wazee Kolandoto ambapo alisema dini safi ni ile ya kusaidia watu wenye uhitaji.
Askofu wa kanisa la Wasabato jimbo Kuu Kaskazini mwa Tanzania Dk. Godwin Yakundaya akizungumza katika kambi ya wazee Kolandoto.
Mratibu wa idara ya vijana kanisa la Wasabato kanda ya Shinyanga Wilson Mjinja akizungumza katika kambi ya wazee Kolandoto ambapo alisema jumla ya shilingi milioni 1.8 zimetumika kukarabati jengo hilo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akifungua mlango wa chumba kimoja katika kituo cha kulelea wazee Kolandoto katika manispaa ya Shinyanga lililokarabatiwa na kanisa la Waadventista Wasabato kama ishara ya kulipokea jengo hilo kwa niaba ya serikali mkoani Shinyanga .Mkuu huyo wa wilaya alipongeza jinsi lilivyokarabatiwa.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akitoka ndani ya chumba kimoja cha jengo hilo
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akikagua jengo hilo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza baada ya kupokea jengo hilo ambapo aliwaomba wadau wengine wa maendeleo kujitokeza kukarabati majengo yaliyosalia katika kituo hicho
Hili miongoni mwa majengo yaliyochakaa katika kituo cha kulelea wazee Kolandoto,ambalo linahitaji kukarabatiwa au kubomolewa lijengwe jengo jingine
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akikabidhi zawadi ya chakula msimamizi wa kambi hiyo ya wazee Sophia Kang'ombe ambavyo vimetolewa na waumini wa kanisa la Wasabato mjini Shinyanga.
Wazee wa kambi hiyo na watu mbalimbali waliofika katika kambi hiyo wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea
Mwenyekiti wa kambi ya wazee Kolandoto Samwel Maganga akipokea zawadi ya mbuzi kwa niaba ya wazee wa kambi ya Kolandoto
Mwenyekiti wa kambi ya wazee Kolandoto Samwel Maganga akipokea zawadi ya mbuzi ambapo alilishukuru kanisa la Wasabato kwa kuwakarabatia jengo hilo na zawadi ya chakula ambacho watakitumia hasa kwenye sikukuu ya Eid mwezi huu.
 
Picha zote kwa hisani ya Marco Maduhu
KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO SHINYANGA LAKARABATI JENGO LA WAZEE KITUO CHA KOLANDOTO KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO SHINYANGA LAKARABATI JENGO LA WAZEE KITUO CHA KOLANDOTO Reviewed by WANGOFIRA on 20:42:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.