KAMPUNI YA TRUMARK YATOA ZAWADI YA EID EL-FITR KWA WATOTO YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM


 Keki maalumu ya hafla hiyo ikikatwa kwa pamoja. Kushoto ni Makamu Mkurugenzi wa Kituo hicho, Theobald Truphone na katikati ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo. Wengine ni maofisa wa Kampuni ya Trumark.

Na Dotto Mwaibale

JAMII imetakiwa kujenga moyo wa kusaidia watu waliopo katika makundi yenye uhitaji ili nao wajisikie kama watu wengine waliopo katika familia.

Mwito huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark inayojishughulisha na uwezeshaji  jamii, Agnes Mgongo wakati kampuni hiyo  ilipokuwa ikitoa zawadi ya Sikukuu ya Eid El-Fitr katika Kituo cha watoto Yatima  cha Mtoto Wetu Tanzania kilichopo Kimara Suca jijini Dar es Salaam leo hii.

"Ni vizuri jamii ikajenga tabia ya kuwakumbuka watoto na watu wengine waliopo  katika makundi maalumu kwa kuwafariji badala ya kuiachia serikali ambayo ina mambo mengi ya kufanya" alisema Mgongo.

Alisema kampuni yake iliguswa na changamoto walizonazo watoto waishio katika kituo hicho ikaona ni vizuri katika kipindi hiki cha sikukuu ya Eid El-Fitr wakajumuike nao kwa kula na kucheza pamoja na kuwapa zawadi mbalimbali.

Mgongo alitaja zawadi walizotoa kupitia wadau wengine marafiki wa taasisi hiyo kuwa ni nguo, vinywaji na chakula ambacho kilipikwa katika kituo hicho.

Akizungumzia changamoto wanazokumbana nazo watoto waliopo katika makundi yenye  uhitaji, Wanswekula Zacharia alisema ni pamoja na vitabu, karo, sare za shule na  mahitaji mengine.

Alisema pamoja na kuwepo kwa changamoto hizo mwanafunzi anapaswa kujua wajibu wake akiwa shuleni ni kusoma na si vinginevyo.

Alisema kupokea misaada ni jambo moja lakini hata mtu kufika tu kituoni hapo na  kuwajulia hali bila ya kuwa na kitu chochote ni jambo la heri kwani wanachohitaji  zaidi ni kujumuika na jamii na kupata faraja.

Mwanafunzi wa kidato cha sita, Shafii Hassan ambaye analelewa katika kituo hicho  tangu akiwa mdogo anasema misaada wanayoipata imekuwa ikiwafanya wapate faraja  ukizingatia ukubwa wa changamoto walizonazo.

Makamu Mkurugenzi wa Kituo hicho,Theobald Tryphone aliishukuru kampuni hiyo kwa  msaada huo na kueleza changamoto kubwa walizonazo ni ada za wanafunzi, chakula,  ulipaji wa umeme na kuwa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad) wameweka alama za x  katika majengo yao waondoke lakini suala hilo linashughulikiwa na Manispaa ya  Ubungo kuona jinsi itakavyowasaidia kuwasaidia kupata eneo jingine kwa ajili ya 
kujenga kituo hicho.

Mtoto analelewa katika kituo hicho, Godwin Steven alitoa shukurani kwa kampuni  hiyo kwa niaba ya wenzake kwa msaada huo.
KAMPUNI YA TRUMARK YATOA ZAWADI YA EID EL-FITR KWA WATOTO YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM KAMPUNI YA TRUMARK YATOA ZAWADI YA EID EL-FITR KWA WATOTO YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM Reviewed by WANGOFIRA on 21:50:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.