RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi ( A Wizard Student ) - Sehemu ya Kwanza



MTUNZI:ENEA FAIDY


Ilikuwa ni majira ya saa moja jioni ambapo mkuu wa while ya Mabango alikuwa ofisini kwake akiwa amechanganyikiwa sana kwani hali ya shule hiyo ilizidi kutisha sana hasa baada ya kutokea kwa vifo vya wanafunzi kumi na tano mfululizo ndani ya wiki moja tu. Tena vifo vya ghafla tu.

Mkuu wa shule mama Dayana Mbeshi alikuwa kwenye wakati mgumu sana kubaini chanzo cha tatizo lakini bado hakupata majibu.Mara ghafla mlango wa ofisi ukagongwa, akaingia mwalimu wa malezi wa shule hiyo akiwa na USO wa huzuni sana hali iliyomshtua sana mkuu wa shule

"vipi kulikoni?"
"hali mbaya mkuu.. wanafunzi wawili wamefariki tena bwenini" mwalimu wa malezi alizungumza kwa huzuni iliyochanganyika na hofu.
"what? mmh! sio bure.. kuna kitu hapa..!" alisikika mwalimu Mbeshi huku akiinamisha kichwa chake chini na kukiegemeza kwenye kiganja chake.

******
Wanafunzi wengi walionekana kuwa na hofu sana baada ya vifo visivotarajiwa kuzidi kutokea katika shule yao. Kila MTU aliwaza sana juu ya vifo vile huku kila mmoja akihisi zamu yake IPO karibu. Nyuso za huzuni ndizo zilizotawala kwa wanafunzi wote si wa kike wala wa kiume. Hakuna aliyetamani kulala wala kukaa mbali na kundi la watu kwani hofu iliwajaa mioyoni mwao, hawakuweza hata kusoma.

Lakini hali ilikuwa tofauti sana kwa binti Doreen ambaye alikuwa na wiki tu toka ahamie shuleni hapo. Alionekana kutoogopa chochote wala kuguswa na misiba ya wanafunzi wenzake. Kila Mara alionekana akiwa na furaha, hali hii iliwatisha wanafunzi wenzake na kuwafanya wawe na maswali mengi juu yake.

Doreen alikuwa msichana mrembo, sura yake nyembamba iliyopambwa na macho makubwa legevu, kope ndefu nyeusi tii, pua nyembamba iliyochongoka vyema na midomo mizuri yenye mvuto wa aina yake vilimfanya awe tishio kila kona kwani alikuwa ni mzuri kupindukia lakini Tabia  ilikuwa tofauti na uzuri wake.

Wakati wanafunzi wengine wakiwalilia wenzao Doreen alikuwa amejitenga peke take nyuma ya bweni alilokuwa anakaa na kulikuwa na Giza totoro. Alikuwa uchi wa mnyama huku mikono yake ikiwa imeshikilia vitu fulani huku akitamka maneno ambayo aliyaelewa mwenyewe....  

Itaendelea.......

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi ( A Wizard Student ) - Sehemu ya Kwanza RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi ( A Wizard Student ) - Sehemu ya Kwanza Reviewed by WANGOFIRA on 20:25:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.