STEVE NYERERE:NAOMBA RADHI KWA VIONGOZI WOTE NILIOWATAJA KWENYE MAZUNGUMZO YANGU NA MAMA SEPETU
Steve Nyerere
.Video ya Steve Nyerere
akizungumza na waandishi wa Habari hii leo.
Msanii wa Filamu nchini Steve
Nyerere, leo amekutana na Waandishi wa Habari, ambapo katika mkutano huo
amekanusha kuwa Wasanii nchini hawakidai Chama Cha Mapinduzi fedha kwa ajili ya
Mradi wa Mama Ongea na Mwanao, wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka
2015.
Katika Mkutano huo STEVE
NYERERE amesisitiza kuwa kilichosemwa na WEMA SEPETU kuwa anaidai CCM fedha ni
uongo, kwani walilipwa huku akisema Msanii aliyelipwa fedha nyingi katika kazi
hiyo ni Wema Sepetu, hivyo anashangaa kusikia akidai kuwa hajalipwa.
Mradi wa Mama Ongea na
Mwanao uliratibiwa na Steven Nyerere huku akisaidiwa na Wema Sepetu na kazi
yake ilikuwa ni kutoa elimu kwa wazazi kuwa karibu zaidi na vijana wao wakati
wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Hata Hivyo, Steve Nyerere,
ametumia mkutano huo kukiri kuwa Sauti iliyotumwa kwenye Mitandao ya Kijamii
inayohusisha mazungumzo yake na Mama yake Wewa Sepetu ni ya kwake, hivyo
amewaomba radhi viongozi wote aliowataja katika mazungumzo hayo.
STEVE NYERERE:NAOMBA RADHI KWA VIONGOZI WOTE NILIOWATAJA KWENYE MAZUNGUMZO YANGU NA MAMA SEPETU
Reviewed by WANGOFIRA
on
19:31:00
Rating:
No comments: