STEVE NYERERE:NAOMBA RADHI KWA VIONGOZI WOTE NILIOWATAJA KWENYE MAZUNGUMZO YANGU NA MAMA SEPETU


Steve Nyerere
 
.Video ya Steve Nyerere akizungumza na waandishi wa Habari hii leo.

Msanii wa Filamu nchini Steve Nyerere, leo amekutana na Waandishi wa Habari, ambapo katika mkutano huo amekanusha kuwa Wasanii nchini hawakidai Chama Cha Mapinduzi fedha kwa ajili ya Mradi wa Mama Ongea na Mwanao, wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Katika Mkutano huo STEVE NYERERE amesisitiza kuwa kilichosemwa na WEMA SEPETU kuwa anaidai CCM fedha ni uongo, kwani walilipwa huku akisema Msanii aliyelipwa fedha nyingi katika kazi hiyo ni Wema Sepetu, hivyo anashangaa kusikia akidai kuwa hajalipwa.

 Mradi wa Mama Ongea na Mwanao uliratibiwa na Steven Nyerere huku akisaidiwa na Wema Sepetu na kazi yake ilikuwa ni kutoa elimu kwa wazazi kuwa karibu zaidi na vijana wao wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.


Hata Hivyo, Steve Nyerere, ametumia mkutano huo kukiri kuwa Sauti iliyotumwa kwenye Mitandao ya Kijamii inayohusisha mazungumzo yake na Mama yake Wewa Sepetu ni ya kwake, hivyo amewaomba radhi viongozi wote aliowataja katika mazungumzo hayo.
STEVE NYERERE:NAOMBA RADHI KWA VIONGOZI WOTE NILIOWATAJA KWENYE MAZUNGUMZO YANGU NA MAMA SEPETU STEVE NYERERE:NAOMBA RADHI KWA VIONGOZI WOTE NILIOWATAJA KWENYE MAZUNGUMZO YANGU NA MAMA SEPETU Reviewed by WANGOFIRA on 19:31:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.