Vyeti FEKI vya vifo Vyatumika Kupata mikopo Elimu ya Juu
Bodi ya Mikopo ya
Elimu ya Juu (HESLB) imebaini kuwepo kwa baadhi ya wanafunzi ambao
wamewasilisha vyeti feki vya vifo vya wazazi wao ili waonekane kama ni watoto
yatima; hivyo wapewe kipaumbele cha kupatiwa mkopo.
Kuwepo kwa vyeti hivyo
vya bandia kumegunduliwa na bodi hiyo baada ya kupeleka nakala za vyeti vyote
vya vifo ofisi ya Msajili wa Vizazi na Vifo (Rita) kwa ajili ya uthibitisho
ndipo ikagundulika kuwepo kwa kasoro hizo.
Mkurugenzi Mtendaji wa
HESLB, Abdul- Razaq Badru, amesema kuwa wahusika wote ambao
wamewasilisha vyeti hivyo feki suala lao limekabidhiwa kwa mamlaka
zinazoshughulika na makosa ya jinai.
Hata hivyo, Badru
hakutaka kuingia kwa undani kuhusu suala hilo kwa maelezo kuwa bado wanaendelea
na ukaguzi.
“Bado tunaendelea
kuchunguza na idadi yao hapa sina, tukikamilisha tutawaita kuwaambia idadi
yao,” alisema Badru na
kuongeza kuwa kutokana na kasoro hizo, ndio maana kuna baadhi ya watu
wanaolalamika kuwa ni yatima, lakini hawakupata mkopo.
“Hayo malalamiko ya kwamba kuna yatima wamekosa mikopo tumeyasikia, lakini na sisi tunajiridhisha kuwa huyu ni yatima baada ya kupata uthibitisho wa vyeti vya vifo kutoka Rita,” alisema Badru.
“Hayo malalamiko ya kwamba kuna yatima wamekosa mikopo tumeyasikia, lakini na sisi tunajiridhisha kuwa huyu ni yatima baada ya kupata uthibitisho wa vyeti vya vifo kutoka Rita,” alisema Badru.
Aliongeza kuwa hata
wale ambao ni wanafunzi wenye ulemavu, bodi hiyo haiwezi kuwaamini kama ni
walemavu, bali hadi wapate uthibitisho kutoka kwa daktari wa wilaya (DMO)
kuthibitisha ulemavu wa mwombaji.
Alisema baadhi ya
wanafunzi ambao wanalalamika kuwa wamekosa mikopo ni wale ambao maombi yao
yalikaguliwa na kukutwa na dosari kadhaa, na wakaombwa wazirekebishe kasoro
hizo, lakini baadhi yao hawakufanya hivyo.
Badru alisema bodi
yake baada ya kuchambua maombi ya waombaji wote; hadi sasa imeshatoa mikopo kwa
wanafunzi wote wanaostahili wakiwemo yatima, walemavu, wanafunzi wanaosoma kozi
za kipaumbele na wahitaji wanaosoma kozi zingine.
Akizungumzia suala la
baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) ambao wamekosa mikopo na
kulazimika kurudi makwao, Badru alisema wanafunzi hao yawezekana ni miongoni
mwa wale ambao hawakukidhi vigezo vya kuweza kupewa mkopo.
“Pale Dodoma tumetoa
mkopo kwa wanafunzi wapya takribani 3,000, hivyo hao wanaoondoka kurudi
nyumbani yawezekana wako kwenye kundi la wanafunzi ambao hawakukidhi vigezo vya
kupewa mkopo,” alisema Badru.
Alisema sio rahisi
kutoa mkopo kwa wanafunzi wote, kwani Serikal inaendeshwa kwa bajeti na mwaka
huu wamechagua kusomesha wanafunzi 25,000 kulingana na bajeti iliyopo pamoja na
kulingana na mahitaji ya wataalamu wanaotakiwa na kutokana na vipaumbele vyake.
Alisema anatambua kuna
wanafunzi zaidi ya 10,000 ambao wamekosa mikopo na kuongeza; “lakini
bajeti ya mwaka huu imeishia hapo, mwaka kesho tunaweza kuishauri Serikali
iongeze fedha baada ya kuwa tumefanya tathmini uhitaji wa mikopo hiyo.”
Hata hivyo, Badru
alisema kuna wanafunzi ambao wanasoma kozi za kipaumbele, lakini wazazi wao
wana uwezo, hao nao hawakupatiwa mikopo licha ya kuwa kwenye kundi la
wanaostahili mkopo.
“Kuna mtu anasomea
udaktari, lakini wazazi wake wana uwezo, na kuna mwanafunzi anasomea sayansi ya
jamii na wazazi wake ni watu wasio na uwezo, hapo lazima tuangalie mhitaji ni
yupi kati ya hao wawili na ndiye tunampatia mkopo,” alisema Badru.
Alisema kuna wanafunzi
wanasoma kozi za kipaumbele baadhi yao hawakupata mkopo kabisa na baadhi yao
wamepatiwa mkopo kidogo baada ya bodi hiyo kufanya tathmini ya hali ya uchumi
ya wazazi au walezi wa mwombaji.
Vyeti FEKI vya vifo Vyatumika Kupata mikopo Elimu ya Juu
Reviewed by WANGOFIRA
on
19:22:00
Rating:
No comments: