Canada: Mtuhumiwa mwingine wa mauaji ya kimbari arejeshwa Rwanda


mediaMtuhumiwa wa mauaji ya Rwanda, Jean Claude Seyoboka, wakati alipowasili KIgali.http://rwandaeye.com/
Afisa wa zamani kwenye jeshi la Rwanda, amewasili jijini Kigali baada ya kusafirishwa kutokea nchini Canada, akituhumiwa kuwa alihusika kwenye mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, ambayo watu laki 8 waliuawa.

Mwendesha mashtaka wa Rwanda, Jean-Bosco Mutangana, amethibitishwa kurejeshwa nchini humo kwa mtuhumiwa Jean Claude Seyoboka, usiku wa kuamkia leo, ambapo sasa atajibu tuhuma za mashataka ya mauaji yanayomkabili.
Seyoboka, ambaye alikuwa ni Luteni wa pili kwenye jeshi la Rwanda, anatuhumiwa kuhusika na mauajiya watusi zaidi ya 72 jijini Kigali na pia anadaiwa kuwa alihudhuria vikao vilivyoidhinisha mauaji hao.
Machafuko hayo yaliyodumu kwa miezi minne, ambapo watu zaidi ya laki 8 waliuawa wengi wakiwa watusi, yalichangiwa baada ya kudunguliwa kwa ndege iliyokuwa imembeba rais wa nchi hiyo Juvenal Habyarimana ambaye alikuwa Muhutu, mwezi April mwaka 94.
Seyoboka aliwasili nchini Canada mwaka 1995, ambako alipatiwa hifadhi ya kudumu nchini humo mwaka mmoja baadae.
Hata hivyo kibali cha hifadhi yake kilitenguliwa miaka kumi baadae, baada ya kutolewa ushahudi kwenye mahakama ya kimataifa ya mauaji ya kimbari ya Rwanda iliyokuwa jijini Arusha, Tanzania na kumuhusisha na mauaji hayo.
Mamlaka nchini Rwanda zilitoa waranti ya kukamatwa kwa Seyoboka mwaka huu, lakini alipigana kupinga kurejeshwa nchini mwake kwa kile alichosema anahofia usalama wake na mateso.
Seyoboka anakuwa mtuhumiwa wa pili wa mauaji ya kimbari kusafirishwa kutoka nchini Canada, baada ya mwanasiasa wa zamani wa nchi hiyo Leon Mugesera kurudishwa nchini Rwanda mwaka 2012.
Mugesera alihukumiwa kifungo cha maisha jela, mwezi April mwaka 1994 kwa madai ya kuhusika kwenye mauaji ya maelfu ya raia.
Juma lililopita pia, mwendesha mashtaka wa Uholanzi, alithibitisha kuwa raia wawili wa Rwanda ambao ni watuhumiwa wa mauaji hayo, nao watarejeshwa nchini mwao.
Nchi ya Rwanda iliomba kurejeshwa nchini humo kwa raia wake Jean-Claude Lyamuremye na Jean-Baptiste Mugimba, mwaka 2012 na 2013, ili warudi kukabiliana na tuhuma za kesi za mauaji na uhalifu dhidi ya binadamu.
Canada: Mtuhumiwa mwingine wa mauaji ya kimbari arejeshwa Rwanda Canada: Mtuhumiwa mwingine wa mauaji ya kimbari arejeshwa Rwanda Reviewed by WANGOFIRA on 05:56:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.