SHULE YA SEKONDARI YA ALMUNTANZIR YA JIJINI DAR ES SALAAM YATOZWA FAINI KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA
Shule ya sekondari ya Almuntazir
iliyopo upanga jijini Dae es salaam imetozwa faini ya shilingi milioni ishirini
na tano kwa kosa la uchafuzi wa mazingira kwa kutirirsha maji taka ya chooni
katika mto msimbazi ndani eneo la mikoko katika eneo la daraja la salenda na
kujenga uzio wa ukuta bila kuzingatia mita sitini zinazotakiwa kisheria.
Faini hiyo inatakiwa kulipwa ndani ya
wiki moja imetokana na ziara ya Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano
na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina iliyofuatia malalamiko ya wakazi wa Upanga
iliyompelekea Naibu Waziri kufanya ziara yakwenda kujionea uchafuzi huo.
Akiongea kwa Niaba ya shule meneja wa
shule hiyo Bw. Serialis Rwechungura amesema kuwa, watalipa faini hiyo kama
ilivyoelekezwa na serikali na hakuwa tayari kuongelea swala la ukuta wa shule
hiyo.
Naibu Waziri Mpina amesisitiza kuwa
serikali haitakuwa tayari kuwavumila wawekeajia wakiukaji wa sheria hasa ya
mazingira, na kuweka rehani maisha ya watanzania.
Aidha Naibu Waziri alitembelea
maeneo ya mwenge kijijini na kuonea
uchafu wa mazingira uliotokana na kuvuja kwa maji taka ya choo kutoka kwenye
miundombinu ya majitaka ya DAWASCO hali inayosababibsha wakazi na wafanyabiashara
wa maeneo ya mwenge kushindwa kustahimili hali hiyo na kuwa hatarini kupata
magonjwa ya maambukizi kama kipindupindu na homa ya matumbo.
Akiikemea DAWASCO kwa mara nyingine
kwa kutokuonyesha uwajibikaji na utii kwa mamlaka za juu, Naibu Waziri Mpina
ameita NEMC kuiandikia DAWASCO faini ya shilingi milioni ishirini na tano kwa
kutelekeza miundombinu yao na kutakiwa kulipa adhabu hiyo kwa muda wa wiki
mbili.
Na, EVELYN MKOKOI
DAR ES SALAAM
27/10/2016
SHULE YA SEKONDARI YA ALMUNTANZIR YA JIJINI DAR ES SALAAM YATOZWA FAINI KWA UCHAFUZI WA MAZINGIRA
Reviewed by WANGOFIRA
on
14:21:00
Rating:
No comments: