FIKRA ANGAVU; Magufuli usihamie Dodoma kabla hujatembelea Bahi
NA GORDON KALULUNGA
MHESHIMIWA Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr John Pombe Magufuli, ameutangazia ulimwengu kuwa anakusudia kuhamia mkoani Dodoma ili kutimiliza kauli ya aliyekuwa Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alipoutangaza mkoa huo kuwa ndiyo makao makuu ya Chama na Serikali mwaka 1973.
Uamuzi huo baadhi waliushangilia na baadhi kuutilia mashaka kwasababu mbalimbali zikiwemo sababu za kiuchumi, kiusalama na kimazoea.
Fikra zangu Angavu zimeona zimpe mtihani Rais Magufuli. Tena mtihani wa kuchagua kati ya A. au B.
Sehemu (A) ni kwamba Rais Magufuli achague kutohamia Dodoma kwa usalama wa Afya za viongozi na wananchi kwa ujumla na sehemu (B) ni kwamba asihamie mpaka hapo atakapotoa tamko la kufuta vibali vya uchimbaji wa madini hatari aina ya URANI yaliyopo katika wilaya ya Bahi mkoani humo.
Madini haya yakichimbwa, vumbi lake lenye gesi ya radon litasafiri na kuleta madhara makubwa Dodoma ambapo kwa taarifa za kitaalamu, gesi ya radon husafiri kilomita zaidi ya 59 na umbali wa kutoka Bahi mpaka Dodoma mjini ni mfupi.
Bahi District
District | |
Bahi District's location within Dodoma Region. | |
Coordinates: 05°57′10″S 35°18′43″ECoordinates: 05°57′10″S 35°18′43″E | |
Country | Tanzania |
Region | Dodoma Region |
Population (2012) | |
• Total | 221,645 |
Katika mtihani huo binafsi naanza kumwonesha jibu moja wapo ambalo linaweza kumfaa yeye pamoja na Taifa kwa ujumla kwamba ni vema kuchagua kutoa tamko la kupiga marufuku uchumbani wa madini hayo.
Sababu moja wapo ni kwamba vumbi la urani liko katika mfumo wa gesi inayoitwa RADON 222, lenye mionzi hatari inayosababisha kansa kwa wanyama na binadamu, linaua mimea na lina uwezo mkubwa wa kusafiri kwa njia ya upepo na hivyo kuna uwezakano mkubwa kudhuru wakazi wa makao yetu hayo makuu ya nchi yetu.
Fikra Angavu kutoka hapa Nyikani haielezi haya kwasababu ya Rais Dkt. Magufuli kukusudia kuhamia Dodoma, la hasha, bali madhara ya madini hayo yanaweza kuwakumba hata wananchi wa kawaida endapo tu yakiruhusiwa kuchimbwa hata kama Rais hatohamia huko.
Kwa taarifa za Nyikani ni kwamba, kuna kampuni moja iliyokuwa na nia ya kuchimba madini ya hayo kule Bahi inayoitwa URANEX kutoka nchini Australia. Inasemekana kuwa kampuni hiyo ilijitoa katika sekta hiyo ikidai kuwa imegundua madini ya graphite.
Kampuni hiyo ilibadilisha jina lake na sasa inajulikana kwa jina la
“Magnis Resources.” Kampuni nyingine ambayo imekuwa ikijihusisha na
utafutaji wa urani katika eneo hilo hilo ni MANTRA ambayo pia
inatoka nchini Australia. Itakumbukwa kuwa ni kampuni hii hii ya
MANTRA iliyogundua urani katika eneo la Mto Mkuju ndani ya hifadhi ya Pori la Selous na baadaye kuiuzia kampuni nyingine ya uchimbaji wa
urani kutoka nchini Urusi.
Kwa mfano, kampuni ya MANTRA kutoka Australia ndiyo inayodai
kugundua urani katika eneo la Mto Mkuju ndani ya Hifadhi ya Pori la
Selous. Kama wote tunavyofahamu, pori hili ni Eneo la Urithi wa Dunia uliotangazwa na UNESCO mwaka 1982.
Hata hivyo, mwaka 2014 shirika la UNESCO lilitahadharisha
kuwa kuna hatari ya wanyama kutoweka na hadhi ya hifadhi hiyo kushuka kutokana na ongezeko la kutisha la matukio ya ujangili.
Shirika hilo la Umoja wa Mataifa, lilionyesha kuwa wakati fulani
hifadhi ya Selous iliongoza kwa kuwa na tembo wengi zaidi duniani. Kwa mfano, katika mwaka 1976, Pori la Akiba la Selous lilikuwa na tembo 110,000.
Hata hivyo, kutokana na ujangili kupamba moto, ilipofika mwaka 2014,
idadi ya tembo katika pori hilo ilipungua kwa karibu asilimia 90
na kufikia tembo 15,000! Hivi sasa katika eneo hilo, tayari kuna
kampuni kutoka Urusi ambayo ina mpango wa kuanza kuchimba urani katika eneo la Mto Mkuju.
Ikiwa uchimbaji utaanza,ni wazi utakuwa na changamoto kubwa kwa pori hilo . Kwa kifupi, kama ilivyo hatari kwa Bahi, uchimbaji wa urani
katika Mto Mkuju utakuwa ni hatari kwa watu, wanyama na mimea katika Pori la Akiba la Selous.
Pia, kutokana na uwepo wa maeneo makubwa yenye maji chini ya ardhi, maji ambayo ni urithi mkubwa kwa Tanzania, maji hayo yanaweza kuharibiwa ikiwa uchimbaji huo wa urani utaruhusiwa.
Sanjari na hayo, taarifa za utafiti wa uchumi zinabainisha wazi kuwa hakuna nchi ambayo imeweza kuendelea kutokana na uchimbaji wa madini. Madalali pamoja na matajiri wao wanawekeza katika kampuni wakijifanya wanafanya utafiti wa madini wakati ukweli wanaujua nyuma ya pazia. Madini hayaozi.
Kampuni hiyo ilibadilisha jina lake na sasa inajulikana kwa jina la
“Magnis Resources.” Kampuni nyingine ambayo imekuwa ikijihusisha na
utafutaji wa urani katika eneo hilo hilo ni MANTRA ambayo pia
inatoka nchini Australia. Itakumbukwa kuwa ni kampuni hii hii ya
MANTRA iliyogundua urani katika eneo la Mto Mkuju ndani ya hifadhi ya Pori la Selous na baadaye kuiuzia kampuni nyingine ya uchimbaji wa
urani kutoka nchini Urusi.
Kwa mfano, kampuni ya MANTRA kutoka Australia ndiyo inayodai
kugundua urani katika eneo la Mto Mkuju ndani ya Hifadhi ya Pori la
Selous. Kama wote tunavyofahamu, pori hili ni Eneo la Urithi wa Dunia uliotangazwa na UNESCO mwaka 1982.
Hata hivyo, mwaka 2014 shirika la UNESCO lilitahadharisha
kuwa kuna hatari ya wanyama kutoweka na hadhi ya hifadhi hiyo kushuka kutokana na ongezeko la kutisha la matukio ya ujangili.
Shirika hilo la Umoja wa Mataifa, lilionyesha kuwa wakati fulani
hifadhi ya Selous iliongoza kwa kuwa na tembo wengi zaidi duniani. Kwa mfano, katika mwaka 1976, Pori la Akiba la Selous lilikuwa na tembo 110,000.
Hata hivyo, kutokana na ujangili kupamba moto, ilipofika mwaka 2014,
idadi ya tembo katika pori hilo ilipungua kwa karibu asilimia 90
na kufikia tembo 15,000! Hivi sasa katika eneo hilo, tayari kuna
kampuni kutoka Urusi ambayo ina mpango wa kuanza kuchimba urani katika eneo la Mto Mkuju.
Ikiwa uchimbaji utaanza,ni wazi utakuwa na changamoto kubwa kwa pori hilo . Kwa kifupi, kama ilivyo hatari kwa Bahi, uchimbaji wa urani
katika Mto Mkuju utakuwa ni hatari kwa watu, wanyama na mimea katika Pori la Akiba la Selous.
Pia, kutokana na uwepo wa maeneo makubwa yenye maji chini ya ardhi, maji ambayo ni urithi mkubwa kwa Tanzania, maji hayo yanaweza kuharibiwa ikiwa uchimbaji huo wa urani utaruhusiwa.
Sanjari na hayo, taarifa za utafiti wa uchumi zinabainisha wazi kuwa hakuna nchi ambayo imeweza kuendelea kutokana na uchimbaji wa madini. Madalali pamoja na matajiri wao wanawekeza katika kampuni wakijifanya wanafanya utafiti wa madini wakati ukweli wanaujua nyuma ya pazia. Madini hayaozi.
Taarifa za kisayansi kutoka Ujerumani, kwa zaidi ya miaka 20 iliyopita, imetumia zaidi ya Euro bilioni saba kusafisha eneo la machimbo ya urani katika iliyokuwa Ujerumani ya Mashariki.
Machimbo hayo ya urani yalikuwa yakichimbwa na kampuni ya Kirusi na
baada ya Ujerumani Mashariki na Magharibi kuungana Oktoba 3, 1990,
kazi ya kusafisha ardhi ya maeneo ya machimbo hayo ilianza.
Machimbo hayo ya urani yalikuwa yakichimbwa na kampuni ya Kirusi na
baada ya Ujerumani Mashariki na Magharibi kuungana Oktoba 3, 1990,
kazi ya kusafisha ardhi ya maeneo ya machimbo hayo ilianza.
Hata hivyo wataalamu wa urani wanasema mionzi ya urani bado iko ijapokuwa imepunguzwa sana.Ikumbukwe kuwa suala hili linahusu nchi tajiri, yenye teknolojia na sayansi ya juu sana hapa duniani tofauti na Tanzania.
Kwasababu Rais, Dkt. Magufuli ni mtaalam wa masuala ya sayansi naamini atakuwa ameisikia na kuielewa sauti hii kutoka hapa Nyikani.
Kwasababu Rais, Dkt. Magufuli ni mtaalam wa masuala ya sayansi naamini atakuwa ameisikia na kuielewa sauti hii kutoka hapa Nyikani.
FIKRA ANGAVU; Magufuli usihamie Dodoma kabla hujatembelea Bahi
Reviewed by WANGOFIRA
on
13:36:00
Rating:
No comments: