Wizara ya Afya Kuzindua Kondomu Mpya Jijini MWANZA


Baada ya juzi Agost 30,2016 Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, kuzindua aina mpya ya Kondomu iitwayo Zana Kondomu mkoani Mbeya, Uzinduzi kama huo unatarajiwa kufanyika mkoani Mwanza Septemba 05,mwaka huu.

Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza, Atley Kuni (pichani), jana alisema mkoa wa Mwanza unatarajia kupokea ugeni kutoka wizara hiyo ambao utajumuisha wataalamu mbalimbali wa afya watakaokuwa wakitoa semina na elimu kwa njia mbalimbali ikiwemo kutumia vyombo vya habari, wakielezea juu ya uzinduzi wa kondomu hiyo.

Alisema miongoni mwa dhumuni la kuzindua aina hiyo mpya ya Kondomu, ni kusaidia katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Ukwimwi ambapo Wizara itakuwa ikigawa bure kondomu hizo zenye ubora kwa wananchi, kote nchini.

Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza, Atley Kuni.

Baadhi ya Wanahabari mkoani Mwanza, wakimsikiliza Afisa Habari Sekretarieti ya Mkoa wa Mwanza.
Wizara ya Afya Kuzindua Kondomu Mpya Jijini MWANZA Wizara ya Afya Kuzindua Kondomu Mpya Jijini MWANZA Reviewed by WANGOFIRA on 21:43:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.