RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 28


Mtunzi: ENEA FAIDY

.... Leyla alikuwa amechanganyikiwa sana baada ya mumewe kuwa katika Hali ile. Alishindwa kuelewa atafanyaje ili kujimudu katika familia yake kwani Mwalimu John ambaye ni mumewe asingeweza kurudi tena kazini. Kilichomfanya anyong'onyee zaidi ni hali ya Judith kwani hakuweza kuongea wala kusikia. Leyla alikosa raha sana, akakaa kitini akiwa na mawazo mengi sana. Alijiuliza afanye nini ili aweze kuwaokoa wahanga wa tatizo asilojua limetona na nini. 
Akiwa katika kutafakari hayo yote ghafla wazo muhimu lilimjia kichwani mwake. Leyla alichukua simu yake na kutafutw namba fulani kisha akapiga. Simu iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa kisha ikakakata. Leyla hakukata tamaa akapiga tena lakini majibu yakabaki Yale Yale, simu haikupokelewa akajaribu tena na tens simu ikapokelewa.

"Bwana asifiwe mchungaji.." Alizungumza Leyla kwa sauti ya unyenyekevu sana kwani aliyempigia alikuwa ni mchungaji wake.
"Amen.. Unasemaje?" Alijibu mchungaji yule kama vile hataki kuzungumza.
"Samahani mchungaji nina shida... Naomba msaada wako!" Alisema Leyla.
"Shida gani"
"Kuhusu familia yangu!".

"Kama ni mumeo mama... Chukua imani hapo ulipoanza maombi Mimi sina muda... Nina mambo mengi ya kufanya.." Alisema mchungaji yule kwa ukali kiasi jambo lililomtisha sana Leyla kwani hakutegemea kama mchungaji wake angemjibu vile. 

"Pastor! Tafadhali nisaidie.." Leyla alimbembeleza mchungaji lakini hakumuelewa. Na mchungaji huyu ndiye aliyefanya mazishi ya mwalimu John.

"Kwasasa sipo nyumbani.. Nipo mbali kikazi..." Alisema Mchungaji yule. Kiukweli ilikuwa vigumu kwa Leyla kuamini maneno ya mchungaji wake kwani Siku zote aliamini mchungaji wake angekuwa ndiye mfariji lakini haikuwa hivyo.
"Cha kukusaidia labda nitawaita wanamaombi waje kukusaidia" alisema mchungaji na kukata simu. 
Leyla alishindwa afanye nini kwani hata ndugu zake walimtenga. Ilipita nusu SAA nzima , mlango wake ukagongwa. Alifurahi sana kwani alijua tayari mchungaji amewasiliana na wanamaombi ili waje kuombea familia yake. Alinyanyuka kitini na kwenda moja kwa moja kufungua mlango.
*****
Mama Pamela alizidi kutetemeka kwa woga sana, alijikunyata kama mgonjwa kitandani kwake. Lakini alizidi kuisikia sauti ya mwanae ikiendelea kumwita. Mama Pamela akazidi kupata hofu, japo aliogopa sana lakini aliamua kuinuka kitandani na kunyata taratibu kuelekea chumbani kwa Pamela. Na hii ni kwa sababu damu nzito kuliko maji . 
Nyumba ilitawaliwa na kiza kizito sana, hivyo ilimpa shida sana Mama Pamela kuelekea chumbani kwa mwanae. Aliingia chumbani kwa Pamela na kuita taratibu "Pamela! Pamela!" Lakini Pamela hakuitikia. Mama Pamela alisogelea kitanda cha Pamela na kuanza kupapasa papasa lakini cha ajabu hakuona dalili zozote za uwepo wa mtu kitandani pale. Mama Pamela alizidi kuchanganyikiwa sana. 
Akaita tena "Pamela! Pamela!" Lakini bado hakukuwa na sauti yoyote iliyoitikia. Mama Pamela alihisi akili yake inavurugika. Akauvua woga wake na kumuita Pamela kwa sauti kubwa lakini bado hakuitikia. 

Mama Pamela alirudi chumbanu kwake na kupapada sehemu ilipokuwepo simu yake na baada ya kuipata alimshukuru Mungu. Kisha akawasha tochi na kuanza kumulika kila chumba. 

Aliingia chumba cha kwanza akamulika lakini hakuona MTU, akamulika, cha pili, cha tatu na kisha akaingia jikoni lakini bado hakumuona Pamela. Roho ya Mama Pamela iliingiwa simanzi, akajua mwanaye amepotea kwa mazingira ya kutatanisha . akaingia bafuni na kumulika lakini Hakumkuta Pamela. Mama Pamela alizidi kuchanganyikiwa zaidi.

"We Mungu bora wangenichukua Mimi sio mwanangu Pamela," alisema Mama Pamela akiingia chooni.
Mama Pamela alistaajabu sana alichokutana nacho. Alimkuta Pamela akiwa amelala chooni huku kajifunika blanketi lake vizuri."
"Pamelaa!" Aliita mama Pamela kwa mshangao na mpaka wakati huo mama Pamela hakujua Doreen anaendeleaje.
****

Mr Alloyce alibaki njia panda, alikuwa haelewi cha kufanya juu ya mwanamke yule. Alijiuliza amkubalie kama mkewe au asimwamini? Mawazo yake hayo mawili yalimezwa na ukarimu wa mwanamke yule kwa jinsi alivyoonesha kumjali Mr Aloyce.

"Mime wangu... Mbona hunichangamkii? Baba Eddy jamani" alisema mwanamke yule na kumsogelea Mr Aloyce "hivi kweli we ni Mke wangu? Mama Eddy?" Aliuliza Mr Alloyce kwa wasiwasi.

"Kha! Kumbe huniamini mume wangu?" Alisema
"Mbona ulitokea kama Chatu?"
"Hahahah unatakiwa kuniamini mume wangu!" Alisema mwanake yule na kumsogelea Baba Eddy kisha akamkumbatia.

Mr Aloyce alitamani kumwamini mwanamke yule kama ndo mkewe lakini moyo wake ulisita. Alimsogelea na kumkumbatia lakini moyoni make alikuwa na mashaka sana.
"Nakupenda mume wangu.. Naomba tuwahi nyumbani ili nikamwone mwanangu" alisema mama Eddy.

"Sawa" alisema Baba Eddy huku akifungua mlango wa gari.
"Lakini unanishangaza mume wangu?"
"Nakushangaza na nini?"
"Huna amani moyoni mwako.. Kwanini?"
"Usijali Niko sawa..." 

Wallingia kwenye gari kisha Mr Aloyce aliwasha gari na kuanza kuendesha. Aligeuka kumtazama mkewe yule aliyekuwa ameketi pembeni yake, lakini kuna kitu kilimshangaza.....
ITAENDELEA....
RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 28 RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 28 Reviewed by WANGOFIRA on 22:34:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.