RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 34



Mtunzi:Enea Faidy

...Lakini cha ajabu kila alipomsogelea binti yule naye alikaza mwendo zaidi. Mama Dorice alishuhudia jinsi ambavyo mwanaye alitembea kwa madaha sana.

"Doriiiice!" Aliita kwa sauti lakini yule msichana alipogeuka hakuwa Dorice tena ilikuwa ni sura ya msichana mwingine kabisa. Mama Dorice alichanganyikiwa sana, ni kwanini hali inakuwa vile? Lakini hakupata jibu. Kaka yake alimfata haraka na kumshika mkono.
"Dada utagongwa na magari... Kwani unamfata nani?" Aliuliza kwa mshangao kwani yeye hakumwona MTU yeyote.
"Namfuata Dorice..."
"Huyo Dorice yuko wapi maana tangu tupo kule unamfuata tu?"

"Sio yeye.. Nimemfananisha...."
"Dada bwana usiwaze sana.... Ona sasa mpaka watu wanakushangaa ujue.. Unaita kila mtu Dorice..."
"Lakini Mimi nilimwona kabisa kaka...."
"Haya tuondoke"
Mama Dorice alikuwa bado anaifikiria ile hali, akajua lazima kuna kitu kinaebdelea kuhusu Dorice, kwanini amfananishe kiasi kile lakini bado hakuwa na jibu sahihi.

Wakati wa safari ulipowadia, waliingia kwenye basi na kukaa kwenye siti zao.Walisafiri kwa mwendo kidogo, ndipo macho ya mams Dorice yalipotua kwenye sura ya yule binti aliyemwona toka wakiwa kituo cha mabasi Jana yake. Na alikuwa amevaa nguo zile zile, alikaa Pembeni yake. Moyo ulimpasuka kwa mshtuko akafikinya macho yake na kumtazama tena binti yule aliyeachia tabasamu mwanana. Akamsalimu mama Dorice. Mama Dorice alishangaa, kilichomshangaza zaidi ni kwamba alipoingia kwenye gari hakumwona MTU yule na hata alipokaa hakukaa na binti yule. Sasa imekuaje yupo nae?
 
"Mama nilikuona sehemu!"
"Mh hata Mimi nilikuona!" Alisema mama Dorice.
"Kwanini ulikuwa unanifata?" Aliuliza binti yule ambaye kila wakati alipenda kutabasamu.
"Nilikuwa na kufananisha na mwanangu" alisema mama Dorice.

"Mwanao? Anaitwa Dorice?"
"Ndio... Umemjuaje?"aliuliza mama Dorice lakini msichana yule alicheka sana kitendo kilichomshangaza mama Dorice.
"Mama we si uliniita Dorice?"
"Eeh ndo jina lake.." Wakati wakiendelea na mazungumzo Yale mjomba wake Dorice alimshangaa sana dada yake.
"Dada mbona unaongea peke yako? Unajibizana na nani?"


                                            ******

Mama Pamela alimtazama binti yake na kumsikiliza kwa umakini.
"Niliota nipo hapa sebuleni... Halafu nikakuona wewe ukiwa haujavaa nguo... Ukanifata na kunishika kifuani kwa muda kisha ukaniachia.... Halafu ulikuwa unatisha sana usoni...." Alisema Pamela.

Mama Pamela hakutaka kuamini kile alichokisikia, alipigwa na butwaa sana na kubaki kinywa wazi akimshangaa mwanaye.

"Mimi? Pamela! Mbona sikuelewi?"
"Ndio mama nilikuona wewe ukichukua titi langu.. Mama kwanini umenifanyia hivyo?" Pamela alisema kwa msisitizo huku akilia. Mama Pamela alizidi kuchanganyikiwa maana hakutegemea kusikia maneno Yale kutoka kwa mwanaye. 

"Ina maana unataka kusema mimi ni mchawi? Pamela kweli unanisingizia hivyo?" Mama Pamela alikuwa haamini lakini hivyo ndivyo Pamela alivyoota. Kwani wakati Doreen akichukua titi lake, pamela hakuiona sura ya Doreen ila alions sura ya Mama yake hivyo aliamini kuwa mama yake ndiye aliyemfanyia vile.

"Mama! Sikujua kuwa wewe ni mchawi! Kumbe ndivyo ulivyo?  Nilikuamini sana mama yangu... Kwanini umenifanyia hivi? Kwanini mama?" Alilalama Doreen na kuonesha ni jinsi gani alivyopoteza uaminifu tena kwa mama yake. Ilikuwa vigumu sana kwa Mama  Pamela kumuamisha mwanaye kuwa sio yeye aliyefanya kitendo kile cha ukatili.

"Pamela mwanangu... Wewe ndo mwanangu wa pekee, sina mtoto  mwingine zaidi yako Leo hii mimi nikufanyie hivyo? Haiwezekani..." Alijitetea mama Pamela.
"Lakini mama... Ili yote yaishe lazima unirudishie titi langu... Na usipofanya hivyo nampigia simu baba namwambia kila kitu.... Na sio baba tu nawaambia ukoo mzima..."

"Pamela... Sio mimi mwanangu... Nisemeje unielewe?" Mama Pamela alijitahidi kujitetea kadri awezavyo lakini bado ilikuwa vigumu kueleweka. Pamela alilia sana huku akimbebesha mama yake mzigo wa lawama. Alichukua simu na kumpigia baba yake, hofu ikamvaa mama Pamela akiifikiria aibu kubwa ambayo angeipata kwenye ukoo wake na wa mumewe. Mpaka muda ule hakujua kinachoendelea kwa Doreen, kwani alidhani yupo chumbani kwake bila kujua Doreen alishaondoka muda mrefu. Kibaya zaidi kilichompa hofu ni kwamba mumewe angeamini maneno ya Pamela kutokana na jinsi mama Pamela alivyokuwa akimtetea Doreen.

"Lazima aamini... Na atajua ni kweli nimefanya hivyo ndio maana nilimkatalia sana Doreen... Haya majanga ya kupewa uchawi wakati mimi so mchawi!" Aliwaza mama Pamela bila kujua hatma ya tatizo lile.
"Daddy!" Alisema Pamela baada ya simu kupokelewa.
"Yes Pamela... Eti nini kimekupata mwanangu...?" Aliuliza Baba Pamela. Pamela akaongeza kilio huku akimtazama mama yake.

"Daddy! Fanya haraka uje... Kuna mambo mazito sana baba.. " alisema Pamela.
"Nakuja Leo jioni na ndege...."
"Uje tu baba yangu... Uje haraka.." Alisema Pamela huku akishindwa kuyazuia machozi yake.
Mama yake alibaki kimya huku machozi yakimdondoka. Alishindwa afanyeje.
"Unalia nini na huo uchawi wako?" Alisema Pamela kwa hasira huk
Oy...

ITAENDELEA.....
RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 34 RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 34 Reviewed by WANGOFIRA on 21:06:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.