PICHA: Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Daraja Wa Waenda Kwa Miguu La Furahisha Pamoja Na Upanuzi Wa Barabara Ya Mwanza Airport
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katikati akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mitambo itakayotumika katika ujenzi wa Daraja la waenda kwa miguu la Furahisha pamoja na upanuzi wa barabara ya Mwanza-airport.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli pamoja na Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani, Mbunge wa Sumve Richard Ndassa wakipiga makofi mara baada ya tukio la uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Daraja la waenda kwa miguu la Furahisha pamoja na Upanuzi wa barabara ya Mwanza-airport.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS, Mhandisi Patrick Mfugale akitoa maelezo ya namna daraja la Furahisha litakavyokuwa mara baada ya kukamilika.
PICHA: Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Daraja Wa Waenda Kwa Miguu La Furahisha Pamoja Na Upanuzi Wa Barabara Ya Mwanza Airport
Reviewed by WANGOFIRA
on
21:20:00
Rating:
No comments: