NMB Yazindua Tawi Katika Jengo La Rock City Jijini Mwanza


Benki ya NMB imeendelea kutanua mtandao wa matawi yake nchini ili kuwa karibu zaidi na wateja wake. Mwishoni mwa wiki iliyopita, NMB ilizindua tawi jipya la NMB Rock City lililopo ndani ya jengo jipya la kibiashara la Rock City jijini Mwanza.

Tawi hili linafanya jumla ya matawi ya NMB kwa Mwanza mjini kufikia matano na 28 kwa kanda nzima ya ziwa ni imani ya NMB zinduzi huu unaleta tumaini jipya kwa wateja wa NMB jijini Mwanza na kanda ya ziwa kwa ujumla. 

Huduma zinazotolewa na tawi hili jipya ni pamoja na kufungua akaunti, mikopo, huduma ya fedha za kigeni, huduma za kuweka na kutoa fedha.

Katika kuhakikisha kuwa NMB inahudumia makundi mbalimbali ya wateja wake kulingana na mahitaji yao ya kifedha, wiki iliyopita, benki iliendesha mkutano wa Klabu ya Biashara uliowakutanisha pamoja zaidi ya wateja 300 wanaohudumiwa na matawi ya NMB ya jijini Mwanza.

 Baadhi ya faida zilizopatikana katika mkutano huo ni pamoja na mafunzo ya jinsi ya kukuza biashara, elimu ya mlipa kodi, jinsi ya kutunza daftari la biashara na njia mbalimbali za kuboresha biashara.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela (katikati) akikata utepe kuzindua tawi la Rock City Mall la benki ya NMB jijini Mwanza, wa tatu kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa NMB Bi Magreth Ikongo na wa tano kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa NMB Ineke Bussemaker.

Meneja wa NMB kanda ya ziwa- Abraham Augustino akiongea katika mkutano wa klabu ya biashara uliofanyika jijini Mwanza wiki iliyopita. Zaidi ya wateja 300 walihudhuria mkutano huo ambapo pamija na mambo mengine walipata mafunzo ya jinisi ya kukuza biashara, elimu ya mlipa kodi na njia mbalimbali za kuboresha biashara.

Mjumbe wa Bodi ya Wakurungezi ya NMB- Margaret Ikongo akizungumza katika mkutano wa Klabu ya Biashara jijini Mwanza.
NMB Yazindua Tawi Katika Jengo La Rock City Jijini Mwanza NMB Yazindua Tawi Katika Jengo La Rock City Jijini Mwanza Reviewed by WANGOFIRA on 21:08:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.