Mrema Amtaka Lowassa Akae Kimya Hadi Mwaka 2020

Mwenyekiti wa Bodi ya Parole ambaye pia ni Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema amemtaka Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa akubali kwamba alishindwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na akae kimya hadi mwaka 2020.


Mrema ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam na kusisitiza kwamba alimtaka Waziri Mkuu Mstaafu watoke CCM pamoja kwa kuwa nguvu ya upinzani ilikuwa kubwa sana. 

‘’Mimi nitamuuliza 1995 wakati natoka nilikuambia tutoke sasa maji yamechemka tukiweka unga tutakula ugali ukagoma ukasema unaendelea kula kidogo hadi alipojiuzulu akaendelea na CCM hadi alipotaka kugombea Urais akakataliwa na wenzake ndipo akaja upinzani’’ 

Mrema ameongeza kwamba Chama cha Mapinduzi kilitakiwa kuondoka madarakani mwaka 1995 ambapo yeye ndiye alikuwa na nguvu kubwa ya kisiasa nchini. 

Aidha Mrema amewataka vijana kuwa makini na upinzania kwa kuwa Lowassa alijiunga na upinzani baada ya kunyimwa nafasi ya kugombea Urais ndani ya CCM hivyo wajiepushe na maandamano kwani hayana faida kwao. 
Mrema Amtaka Lowassa Akae Kimya Hadi Mwaka 2020 Mrema Amtaka Lowassa Akae Kimya Hadi Mwaka 2020 Reviewed by WANGOFIRA on 20:03:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.