JESHI LA KUJENGA TAIFA(JKT):TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKANUSHA VIJANA WA KUJITOLEA KURIPOTI KAMBINI

Image result for jkt


  TAARIFA KWA UMMA

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) linapenda kukanusha taarifa potofu zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi kwenye baadhi ya simu za mkononi na mitandao ya kijamii inayoeleza kuwa” JKT linawataka vijana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa Kujitolea mwaka 2016, waripoti ofisi za wakuu wa mikoa kati ya terehe 03 – 07 Septemba 2016, tayari kwa kupelekwa kwenye Makambi ya mafunzo ya JKT”.

Taarifa hiyo siyo sahihi na wananchi wanatakiwa kuzipuuza. Utaratibu utakapokamilika wa kuwachukua Vijana hao, JKT itawatangazia kupitia vyombo rasmi vya habari na siyo kwa njia ya simu za mkononi.

Aidha JKT kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Nchini inafuatilia kujua ni mtu gani au kikundi gani kimehusika na upotoshaji huo wa taarifa ili hatua kali za kisheria kuchukuliwa.


Imetolewa na:
Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya JKT
27 Agosti 2016
JESHI LA KUJENGA TAIFA(JKT):TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKANUSHA VIJANA WA KUJITOLEA KURIPOTI KAMBINI JESHI LA KUJENGA TAIFA(JKT):TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKANUSHA VIJANA WA KUJITOLEA KURIPOTI KAMBINI Reviewed by WANGOFIRA on 08:52:00 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.