Wanafunzi wa Kiume Wavaa Sketi Shuleni Kupinga Adhabu ya Mwalimu Wao
Wavulana
wanne katika shule moja nchini Uingereza wamefika shuleni wakiwa
wamevaa sketi kwa muda wa siku mbili kulalamikia hatua ya mwalimu
kuwaadhibu kwa kuvaa kaptura siku yenye joto kali zaidi nchini humo.
Wanafunzi hao wa darasa la mwaka wa tisa katika shule ya Longhill eneo la
Rottingdean, Sussex Mashariki, walikuwa miongoni mwa wanafunzi 20
wavulana waliovalia kaptura za kuvaliwa wakati wa mazoezi badala ya
suruali ndefu.
Baadhi walifukuzwa shuleni Jumanne na wengine kutengwa hadi siku
iliyofuata. Waliokubali kuvua kaptura hizo na kuvalia suruali ndefu
hawakuadhibiwa.
Lakini badala ya kuvalia sare kamili ya wakati wa masomo, kama
walivyokuwa wameagizwa, wanafunzi wanne walirejea shuleni Alhamisi
wakiwa wamevalia sketi.
Watatu waliambiwa wavue sketi hizo lakini wote kwa pamoja wakakataa na ndipo wakaruhusiwa kuendelea kukaa shuleni.
Mwalimu mkuu Kate Williams aliwaambia wanaweza kuvalia mavazi yoyote, mradi yawe ni sehemu ya sare iliyokubalika shuleni.
Wanafunzi wa Kiume Wavaa Sketi Shuleni Kupinga Adhabu ya Mwalimu Wao
Reviewed by WANGOFIRA
on
22:43:00
Rating:
No comments: