Tusinunue ndege kwa 'madesa'
Neno
desa au kuchota ujuzi, taarifa au majibu bila kuyafanyia kazi na
kuyatumia kwenye kazi yako au kunakiri bila kufuata sheria au kukwepa
sheria–kabla ya kuchaguliwa kwa rais John Pombe Magufuli–lilikuwa
limefungiwa kwenye kuta za madarasa na vyumba vya mihadhara ya Chuo
Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM). Hata hivyo, baada ya kuchaguliwa
Magufuli ambaye ni mhitimu wa shahada tatu zote toka UDSM, neno desa
limeingia kwenye msamiati tawala (mainstream).
Hivi
karibuni vyombo vya habari vilimkariri Magufuli si zaidi ya mara moja
akitumia neno desa kuanzia alipohutubia jumuia ya wana UDSM hadi
alipomkaribisha rais wa Rwanda Paul Kagame aliyesema amempa desa au
mbinu ya kununua ndege mbili kwa mpigo. Magufuli alisema, “Mwezi wa tisa
tutakuwa tumepata ndege mbili mpya, nimepewa namna nzuri ya kupata
ndege hizo na Rais Kagame baada ya kuwatuma maofisa wake ambao ni
wataalam wa ndege waje na kunipa desa.”
Si
vibaya kwa viongozi kupeana mbinu za kufanya mambo ingawa hili linatia
shaka kwa namna moja au nyingine. Pia linaacha maswali mengi kuliko
majibu. Je Tanzania–pamoja na kupata uhuru zaidi ya miaka hamsini
iliyopita–haina wataalamu wake wenye ujuzi na wa kuaminika kufanya kazi
hiyo hadi tukope wataalamu toka Rwanda?
Kwa mujibu wa matamshi ya
Magufuli ni kwamba Tanzania haina wataalamu wa kutafuta na kununua ndege
jambo ambalo ni aibu kwake na taifa. Vyema,
kuwa Magufuli amepewa desa; je amepewa na wataalamu wa kuendesha ndege
husika? Je wataalamu wetu wanaolipwa kumshauri Magufuli wanalipwa kwa
kazi gani kama rais analazimika kukopa washauri na wataalamu toka nje? Je hilo shirika litaendeswa na hao wataalamu wa Kagame?
Kisa
cha Magufuli kupewa “desa” kinanikumbusha kisa cha jamaa mmoja
aliyeomba ng’ombe kwa rafiki yake ili naye akafuge na kupata maziwa,
mbolea na nyama. Hata hivyo, jamaa huyu alikuwa na kasoro nyingi; hakuwa
na uwezo wala ujuzi wa kumtunza ng’ombe aliyezawadiwa. Hivyo,
alipoletewa ng’ombe alisema, “Asante sana rafiki yangu. Hata hivyo,
naomba mtu wa kumswaga huyu mnyama.” Mwenyeji wake alimjibu, “Umepata.
Je una jingine?” mgeni alijibu, “Je nitapata wapi mtu wa kumkamua,
kumlisha na kumtunza?” mwenyeji alisita kidogo na kusema, “Ngoja kidogo”
alimwambia yule mtumishi aliyekuwa ameleta ng’ombe, “mrudishe huyo
ng’ombe kwa wenzake hadi jamaa atapopata ujuzi na uwezo wa kumtunza
atajua jinsi ya kuja kumchukua na kummilki.”
Jamaa alibaki kujishangaa
na kushangaa namna alivyojiaibisha. Kwa
ufupi ni kwamba; sitashangaa ndege husika zikaishia kuuzwa kwa hao hao
manoadesa kwao. Hili liko wazi na wenzetu wanalijua. Kwani wengi
wamezaliwa na kukulia na kusomea Tanzania. Mbali na hili, hata
ukiangalia tulivyoinga kwenye Jumuia ya Afrika Mashariki kijinga, kuna
uwezekano Tanzania ikaishia kuwa kimbilio la watu wasio na ardhi au kuja
kuchuma na kurejea kwao. Mimi huwa siamini katika mashirikisho na
jumuia za kimajimbo bali muungano wa haraka na moja kwa moja wa Afrika.
Je muungano wa Afrika unawezekana wakati kila rais anang’ang’ania ulaji
wake? Hili humu si mwake leo.
Japo
Magufuli anasherehekea na kujisifia kupewa desa, anapaswa kufikiri na
kuangalia mbali zaidi hasa usawa huu ambapo kila nchi inatafuta kila
fursa kuwanufaisha watu wake baada ya nchi za kiafrika–kwa ujinga,
uroho, upogo na kongwa za kikoloni zilikataa kuungana na kuwa nchi moja
kama Marekani au China. Watanzania
kukiri kuwa hamna ujuzi na kuwaamini hawa watoa madesa, mmewapa
kishawishi cha kuanga kujiandalia kurejesha ng’ombe zizini hadi
mtakapopata uwezo na kuwa tayari kummlilki na kumtunza ng’ombe husika.
kama shida ni wataalamu, kwanini Magufuli hakuwatuma wataalamu wake
kwenda Rwanda kujifunza badala ya kuwaamini kazi wanyarwanda ambao
hawako chini ya kiapo chochote wala uwajibikaji kisheria wa kuitumikia
Tanzania? Kwanini hatutaki kujifunza tokana na wale tuliwatengeneza
tukidhani ni watanzania wakaishia kutuacha Solemba? Kwanini
watanzania tunakuwa wepesi kufanya mambo muhimu kuwa ya mzaa kama
kuamini uchumi wetu kuwa mikononi mwa wageni kama inavyozidi kubainika
ambapo matapeli wa kigeni huja nchini wakijifanya wawekezaji wakiwa
mikono mitupu na kuondoka na utajiri wa kutisha wakati watu wetu wakiwa
maskini?
Kama
tutakuwa wakweli, nchi iliyopata uhuru zaidi ya nusu karne ahitaji
msaada hata wa namna ya kununua ndege. Hii maana yake–kama inashindwa
kuwa na wataalamu wa kununa ndege–maana yake haina hata wataalam wala
mipango madhubuti ya kuendesha shirika la ndege linalokusudiwa
kuanzisha? Je tatizo ni wataalamu au uzalendo na mfumo bora? Mbona
baadhi ya wataalamu wa Rwanda wamesoma tena bure hapa Tanzania
wakijionyesha kama watanzania wakati ni wanyarwanda? Ajabu
hatukuwachukulia hatua ikizingatiwa kuwa nchi yetu hairuhusu uraia wa
nchi mbili. Je hawa waliotukimbia wataweza kutusaidia kweli? Mjinga ni
yule anayeng’atwa na nyoka mara mbili kwenye shimo moja.
Tumalizie
kwa kumshauri rais Magufuli kufikiria upya kuhusiana na mpango wake wa
kuazima wataalamu toka Rwanda au kwingineko. Kununua ndege hakuna
haraka. Anapaswa kutuma wataalamu kujifunza si Rwanda tu bali Kanada
zinakotengenezwa ndege husika. Kama tunashindwa na jambo dogo ambalo
makampuni ya watu binafsi kama lile la bilionea Richard Bronson
yamefanya, nini maana ya kuwa huru akiri
bila kufuata sheria au kukwepa sheria–kabla ya kuchaguliwa kwa rais
John Pombe Magufuli–lilikuwa limefungiwa kwenye kuta za madarasa na
vyumba vya mihadhara ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM). Hata hivyo,
baada ya kuchaguliwa Magufuli ambaye ni mhitimu wa shahada tatu zote
toka UDSM, neno desa limeingia kwenye msamiati tawala (mainstream).
Hivi
karibuni vyombo vya habari vilimkariri Magufuli si zaidi ya mara moja
akitumia neno desa kuanzia alipohutubia jumuia ya wana UDSM hadi
alipomkaribisha rais wa Rwanda Paul Kagame aliyesema amempa desa au
mbinu ya kununua ndege mbili kwa mpigo. Magufuli alisema, “Mwezi wa tisa
tutakuwa tumepata ndege mbili mpya, nimepewa namna nzuri ya kupata
ndege hizo na Rais Kagame baada ya kuwatuma maofisa wake ambao ni
wataalam wa ndege waje na kunipa desa.”
Si
vibaya kwa viongozi kupeana mbinu za kufanya mambo ingawa hili linatia
shaka kwa namna moja au nyingine. Pia linaacha maswali mengi kuliko
majibu. Je Tanzania–pamoja na kupata uhuru zaidi ya miaka hamsini
iliyopita–haina wataalamu wake wenye ujuzi na wa kuaminika kufanya kazi
hiyo hadi tukope wataalamu toka Rwanda? Kwa mujibu wa matamshi ya
Magufuli ni kwamba Tanzania haina wataalamu wa kutafuta na kununua ndege
jambo ambalo ni aibu kwake na taifa. Vyema,
kuwa Magufuli amepewa desa; je amepewa na wataalamu wa kuendesha ndege
husika? Je wataalamu wetu wanaolipwa kumshauri Magufuli wanalipwa kwa
kazi gani kama rais analazimika kukopa washauri na wataalamu toka nje? Je hilo shirika litaendeswa na hao wataalamu wa Kagame?
Kisa
cha Magufuli kupewa “desa” kinanikumbusha kisa cha jamaa mmoja
aliyeomba ng’ombe kwa rafiki yake ili naye akafuge na kupata maziwa,
mbolea na nyama. Hata hivyo, jamaa huyu alikuwa na kasoro nyingi; hakuwa
na uwezo wala ujuzi wa kumtunza ng’ombe aliyezawadiwa. Hivyo,
alipoletewa ng’ombe alisema, “Asante sana rafiki yangu. Hata hivyo,
naomba mtu wa kumswaga huyu mnyama.” Mwenyeji wake alimjibu, “Umepata.
Je una jingine?” mgeni alijibu,
“Je nitapata wapi mtu wa kumkamua,
kumlisha na kumtunza?” mwenyeji alisita kidogo na kusema, “Ngoja kidogo”
alimwambia yule mtumishi aliyekuwa ameleta ng’ombe, “mrudishe huyo
ng’ombe kwa wenzake hadi jamaa atapopata ujuzi na uwezo wa kumtunza
atajua jinsi ya kuja kumchukua na kummilki.” Jamaa alibaki kujishangaa
na kushangaa namna alivyojiaibisha. Kwa
ufupi ni kwamba; sitashangaa ndege husika zikaishia kuuzwa kwa hao hao
manoadesa kwao. Hili liko wazi na wenzetu wanalijua. Kwani wengi
wamezaliwa na kukulia na kusomea Tanzania.
Mbali na hili, hata
ukiangalia tulivyoinga kwenye Jumuia ya Afrika Mashariki kijinga, kuna
uwezekano Tanzania ikaishia kuwa kimbilio la watu wasio na ardhi au kuja
kuchuma na kurejea kwao. Mimi huwa siamini katika mashirikisho na
jumuia za kimajimbo bali muungano wa haraka na moja kwa moja wa Afrika.
Je muungano wa Afrika unawezekana wakati kila rais anang’ang’ania ulaji
wake? Hili humu si mwake leo.
Japo
Magufuli anasherehekea na kujisifia kupewa desa, anapaswa kufikiri na
kuangalia mbali zaidi hasa usawa huu ambapo kila nchi inatafuta kila
fursa kuwanufaisha watu wake baada ya nchi za kiafrika–kwa ujinga,
uroho, upogo na kongwa za kikoloni zilikataa kuungana na kuwa nchi moja
kama Marekani au China.
Watanzania
kukiri kuwa hamna ujuzi na kuwaamini hawa watoa madesa, mmewapa
kishawishi cha kuanga kujiandalia kurejesha ng’ombe zizini hadi
mtakapopata uwezo na kuwa tayari kummlilki na kumtunza ng’ombe husika.
kama shida ni wataalamu, kwanini Magufuli hakuwatuma wataalamu wake
kwenda Rwanda kujifunza badala ya kuwaamini kazi wanyarwanda ambao
hawako chini ya kiapo chochote wala uwajibikaji kisheria wa kuitumikia
Tanzania?
Kwanini hatutaki kujifunza tokana na wale tuliwatengeneza
tukidhani ni watanzania wakaishia kutuacha Solemba? Kwanini
watanzania tunakuwa wepesi kufanya mambo muhimu kuwa ya mzaa kama
kuamini uchumi wetu kuwa mikononi mwa wageni kama inavyozidi kubainika
ambapo matapeli wa kigeni huja nchini wakijifanya wawekezaji wakiwa
mikono mitupu na kuondoka na utajiri wa kutisha wakati watu wetu wakiwa
maskini?
Kama
tutakuwa wakweli, nchi iliyopata uhuru zaidi ya nusu karne ahitaji
msaada hata wa namna ya kununua ndege. Hii maana yake–kama inashindwa
kuwa na wataalamu wa kununa ndege–maana yake haina hata wataalam wala
mipango madhubuti ya kuendesha shirika la ndege linalokusudiwa
kuanzisha? Je tatizo ni wataalamu au uzalendo na mfumo bora? Mbona
baadhi ya wataalamu wa Rwanda wamesoma tena bure hapa Tanzania
wakijionyesha kama watanzania wakati ni wanyarwanda? Ajabu
hatukuwachukulia hatua ikizingatiwa kuwa nchi yetu hairuhusu uraia wa
nchi mbili. Je hawa waliotukimbia wataweza kutusaidia kweli? Mjinga ni
yule anayeng’atwa na nyoka mara mbili kwenye shimo moja.
Tumalizie
kwa kumshauri rais Magufuli kufikiria upya kuhusiana na mpango wake wa
kuazima wataalamu toka Rwanda au kwingineko. Kununua ndege hakuna
haraka. Anapaswa kutuma wataalamu kujifunza si Rwanda tu bali Kanada
zinakotengenezwa ndege husika. Kama tunashindwa na jambo dogo ambalo
makampuni ya watu binafsi kama lile la bilionea Richard Bronson
yamefanya, nini maana ya kuwa huru na kupoteza fedha kusomesha wataalamu
ambao hawawezi hata kununua ndege?
Tusinunue ndege kwa 'madesa'
Reviewed by WANGOFIRA
on
23:17:00
Rating:
No comments: