Theresa May kuwa waziri mkuu mpya wa Uingereza
Hii ni baada ya mpinzani wake mkuu katika kinyanganyiro ya kuwania kiti cha uaziri mkuu mbunge Andrea Leadsom, kujiondoa.
Uingereza kupata waziri mkuu mwanamke
Andrea Leadsom ameamua kumuunga mkono mpinzani wake, Theresa May kuwania kiti hicho, huku akisema kuwa anatakiwa kutimiza uungwaji wake mkono wa kujiondoa kwa Uingereza kutoka muungano wa jumuia ya mataifa ya EU na kutoa fursa kupatikana kwa haraka kwa waziri mkuu mpya.
Wakuu wa chama cha Conservative kwa sasa wanajadiliana ili
kumuidhinisha Bi May, kuchukua nafasi hiyo na kuwa waziri mkuu wa pili
wa kike nchini Uingereza baada ya Bi Margaret Thatcher.
Wakati huo huo, Mbunge Angela Eagle ametangaza rasmi nia ya kumn’goa Jeremy Corbyn kama kinara mkuu wa chama cha Leba.
Source: BBC
Theresa May kuwa waziri mkuu mpya wa Uingereza
Reviewed by WANGOFIRA
on
20:48:00
Rating:
No comments: